Wapangaji walalamika kubaguliwa
Wakati serikali imesitisha zoezi la kuandikisha nyumba na mali za watu walioathirika kwa mabomu yaliyolipuka katika kambi ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Mbagala, jijini Dar es Salaam, baadhi ya watu waliokuwa wamepanga katika nyumba hizo wamelalamika kuwa mali zao hazijaorodheshwa kwa ajili ya kufanyiwa tathmini.
Tangu mabomu ya JWTZ yalipolipuka Aprili 29, mwaka huu na kuua raia 20 na wanajeshi sita, nyumba zipatazo 7,241 zimekwishafanyiwa tathmini na Kamati ya Kutathmini Mali za Waathirika, iliyoundwa kufanya kazi hiyo. Watu wapatao 200 walijeruhiwa baada ya milipuko hiyo.
Kamati hiyo iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi, ilitakiwa kutoa ripoti ya awali jana, lakini kutokana na kutokamilika, imeongezewa muda hadi mwishoni mwa mwezi huu.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Cleophace Rweye, alisema kuwa zoezi la kuandikisha nyumba na mali limesitishwa rasmi na jambo wanalofanya sasa ni kumalizia kazi ya kuthaminisha mali hizo.
Rweye alisema zoezi hilo linaendelea vema na wanatarajia kumaliza katika muda waliopewa.
Alisema wanachofanya kwa sasa ni kuandikisha na kuthaminisha nyumba mpya ambazo ziliharibiwa na milipuko ya mabomu iliyotokea Jumatano iliyopita wakati askari wa jeshi hilo walipokuwa wakiteketeza mabomu ambayo hayakuwa yamelipuka katika ajali ya kwanza.
Wakizungumza na Nipashe jana, baadhi ya wenye nyumba na wapangaji walilalamikia zoezi zima la uandikishaji wakidai kuwa mali zao nyingi zilikuwa zimeachwa bila kuandikishwa.
Mchungaji wa Kanisa la African Inland (AIC), Ezekiel Mahalu, alisema wathamini hao wameandikisha kanisa tu na kuacha vifaa vya muziki vilivyoharibika vyenye thamani ya Sh. milioni 10.
Alisema wathamini hao hawakuandikisha mali zozote licha ya kutakiwa kufanya hivyo.
Mpangaji Joshua Kishiwa, alisema wakati Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alipotembelea Mbagala baada ya milipuko hiyo, aliwaahidi kwamba nyumba na mali zote zilizoharibiwa zitaorodheshwa na kuthaminiwa kwa ajili ya kuwalipa fidia wahusika.
Kishiwa ambaye alidai kuwa mali zake zimeharibiwa kabisa, alisema hakuna hata moja ambayo imeorodheshwa kwa ajili ya kufanyiwa tathmini.
“Wamechukua picha ya mwenye nyumba wangu na kuandikisha nyumba yake, lakini sikuulizwa kuandikisha mali zangu. Nilifikiri kwamba walikuwa wanaanza kwanza kuandikisha nyumba na baadaye kuandikisha mali. Nimeshitushwa sana kusikia kwamba zoezi hilo limefungwa rasmi,” alisema.
Mustapha Muhidin, alisema haikuwa sahihi kwa wathamini kuzingatia tu suala la nyumba kwa sababu katika nyumba waliyokuwa wakiishi kulikuwa na wapangaji watano na hakuna hata mmoja aliyetakiwa kuandikisha mali zake.
Muhidin alihoji kitendo cha wathamini kwenda kinyume cha agizo la Waziri Mkuu kwa sababu mali zao zote zilikuwa zimeharibiwa na sasa hakuna hata mmoja aliyekwenda kuandikisha mali zao.
Aliiomba serikali kufuatilia zoezi zima kwa sababu mwisho wa siku kutakuwa na malalamiko mengi kutoka kwa wapangaji.
Said Mohamed aliwalalamikia wathamini hao kwa kukataa kuandikisha televisheni yake moja, seti ya DVD pamoja na samani. Alisema kwa sasa hana kazi, hali ambayo itamuwia vigumu kupata vitu hivyo katika siku za hivi karibuni.
“Kama zoezi la uandikishaji limefikia mwisho na mali zangu hazijaandikishwa, ina maana kwamba sitaweza kuwa na televisheni tena,” alisema.
Wakati huo huo, Diwani wa Mbagala Kuu, Anderson Chale, alisema walimkamata mtu mmoja akijaribu kuandikisha nyumba yake ambayo ilikuwa katika hatua ya ujenzi.
Alisema mara baada ya kubaini ukweli kwamba mkazi huyo alikuwa na lengo la kuwadanganya wathamini, jina lake liliondolewa katika orodha ya watu wanaotakiwa kulipwa fidia. Alisema serikali itaendelea kutoa chakula kwa waathirika hadi hapo watakapolipwa fidia.
CHANZO: NIPASHE 18th May 2009
Showing posts with label Ulinzi na Usalama. Show all posts
Showing posts with label Ulinzi na Usalama. Show all posts
Monday, 18 May 2009
Tuesday, 5 May 2009
Ajali ya mlipuko wa mabomu: Wanajeshi waliopoteza maisha
Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa imewataja wanajeshi watano na ofisa wa jeshi hilo mmoja waliopoteza maisha wakati wakiwa ndani ya ghala la kuhifadhia silaha lililolipuka wiki iliyopita. Wanajeshi hao waliopoteza maisha wakiwa ndani ya ghala hilo wakifanya kazi zao za kawaida na kupoteza maisha ni pamoja na Meja A. M Muhidin, Sajini Amelye Mbeyale, Koplo Phinias Mwambashi, Koplo Mohamed Seif na Koplo Bernard Mbilo. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi alimtaja mwingine aliyepoteza maisha kuwa ni Ofisa Mteule Daraja la Kwanza, Timothy Mtweve ambaye alikwenda eneo la tukio kwa ajili ya kuzima moto na kuwaokoa walioumia katika mlipuko huo.
Alifariki dunia alipofikishwa hospitalini kwa matibabu. Dk. Mwinyi alisema katika tukio hilo, wanajeshi wawili waliokuwa nje ya ghala hilo la kuhifadhia silaha walijeruhiwa. “Wengine mwanajeshi na mpishi walikuwa nje ya ghala walifanikiwa kukimbia baada ya kusikia mlipuko na hao tunawategemea kutusaidia kutoa maelezo ya chanzo cha mlipuko huo,” alisema Dk. Mwinyi.
Dk. Mwinyi alisema kuwa Baraza la Uchunguzi limeshaundwa kuchunguza tukio hilo ambalo lina wajumbe tisa na linaongozwa na Meja Jenerali Sylvester Chacha Rioba. Wajumbe wa baraza hilo ni pamoja na wataalamu wa milipuko, wakemia, maboharia, Ofisa wa Polisi, Ofisa wa Idara ya Zimamoto na Ofisa Mhakiki Mali. Hadidu rejea kwa baraza hilo ni pamoja na kuchunguza na kubaini chanzo, madhara, hasara na kupendekeza hatua za kuchukuliwa ili kuzuia tukio kama hilo lisitokee tena. Sambamba na baraza, hatua za ziada zinachukuliwa kuepusha tukio kama hilo lisitokee katika maghala mengine.
“Tahadhari ya usalama inatolewa kwa wananchi wote wasiokote au kuficha chuma chochote kilichotokana na mlipuko, silaha, risasi zilizosambaa eneo la mlipuko na kwenye makazi. Vitu vya aina hiyo vitolewe taarifa kwa timu ya wanajeshi wanaovikusanya au kituo cha Polisi, ni kosa la jinai kama mtu atapatikana anahifadhi silaha, risasi au mlipuko wa aina yoyote”, alisisitiza Waziri huyo.
Waziri huyo alisema kazi ya kusafisha eneo la makazi ya wananchi kwa kuondoa vipande vya mabomu na mabaki ya makombora inaendelea na kuwataka wananchi watoe ushirikiano kwa wanajeshi kuwaonyesha yalipo mabaki. Aprili 29, mwaka huu, ghala lililokuwa limehifadhi silaha ndogondogo, mabomu, makombora na risasi katika kambi ya Jeshi Mbagala lililipuka na kusababisha vifo vya wanajeshi hao na raia 18 sambamba na nyumba kadhaa kuharibika.
Wakati huohuo, serikali imesema kwa mujibu wa tathmini kaya 3,750 za wakazi wa eneo la Mbagala Kuu hazina mahala pa kuishi baada ya nyumba zao kuharibiwa vibaya na milipuko hiyo ya mabomu. Aidha, Sh milioni 660.2 zimechangwa na watu mbalimbali ikiwamo serikali kwa ajili ya kusaidia ununuzi wa chakula, maji, mahema, nguo na mahitaji mengine muhimu.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kupokea msaada wa Sh milioni 5.2 kutoka kwa Jumuiya ya Mabohora Dar es Salaam, iliyoongozwa na Makamu Mwenyekiti wake, Zainuddin Adamjee, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi alisema kwa mujibu wa tathmini hiyo mpaka sasa nyumba 4,636 zimeharibika vibaya. “Tunajaribu kufanya kila tunaloweza kuwasaidia waathirika wa tukio hili na tayari serikali imetoa mifuko 3,750 ya mchele ambapo kila kaya itapewa mfuko mmoja wa kilo 30 na maharage kilo 10,” alisema Lukuvi.
Alisema pamoja na hayo wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwamo ya ukosefu wa mahema ambayo mpaka sasa yamepatikana 87 wakati mahitaji halisi ni mahema 550. “Hapa Tanzania hakuna mahala pa kununua mahema hivyo tunategemea kuazima, tumeaongea na Shirika la Umoja wa Mataifa la Wakimbizi (UNHCR) bado tunasubiri,” alisema. Alisema kwa sasa kinachoendelea ni tathmini ambapo timu za wathamini zimeanza kazi lakini zimeongezewa nguvu na wathamini kutoka Morogoro, Pwani na Tanga na wamezungumza na Mkuu wa Chuo cha Ardhi ambaye ameahidi kuongeza wahitimu 20 wa tathmini katika timu hiyo ili kuweza kufanya tathmini ya nyumba lakini pia pamoja na mali.
Akizungumzia wagonjwa, alisema hadi sasa katika Hospitali ya Temeke wapo 12 na wengine 15 wameongezeka jana ambao kati yao tisa wamelazwa, waliokufa ni raia 18 na maiti zote zimetambuliwa ikiwapo iliyoopolewa jana katika mto Mzinga na kati ya maiti hizo 15 zimezikwa Dar es Salaam moja Singida. Kwa upande wa misaada, Lukuvi alisema serikali imetoa Sh milioni 200, Ofisi ya Waziri Mkuu Sh milioni 200, Bakhresa Sh milioni 100, Quality Group milioni 30, Mwenyekiti wa IPP Reginald Mengi Sh milioni 25, Vodacom Sh milioni 20, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Sh milioni 20, manispaa zote tatu Ilala, Temeke na Kinondoni Sh milioni 60 na Mabohora Sh milioni 5.2.
Alisema fedha hizo zimetumika kulipia gharama za mazishi, kununulia vyakula, maji, nguo kama vile mablanketi na vyandarua, posho za wathamini, mafuta ya magari na posho za askari Polisi 100 wanaolinda eneo la kambi. Naye Meya wa Manispaa ya Temeke, Jerome Bwanausi, alisema kutokana na malalamiko ya baadhi ya waathirika kwamba misaada haiwafikii mengi ni ya uongo na kwamba timu iliyopangwa kugawa misaada hiyo inagawa kulingana na tathmini inayofanywa na idadi ya kaya. Wakati gazeti hili likiwa eneo la maafa, lilishuhudia kikosi cha askari wa JWTZ kikifukua kifusi cha nyumba zilizobomoka huku kikitoa tahadhari kwa watu kukaa mbali kutokana na kuwapo uwezekano wa mabomu ambayo hayajalipuka
(chanzo: www.habarileo.co.tz,
Imeandikwa na Maulid Ahmed na Halima Mlacha; Tarehe: 5th May 2009 @ 08:48)
Alifariki dunia alipofikishwa hospitalini kwa matibabu. Dk. Mwinyi alisema katika tukio hilo, wanajeshi wawili waliokuwa nje ya ghala hilo la kuhifadhia silaha walijeruhiwa. “Wengine mwanajeshi na mpishi walikuwa nje ya ghala walifanikiwa kukimbia baada ya kusikia mlipuko na hao tunawategemea kutusaidia kutoa maelezo ya chanzo cha mlipuko huo,” alisema Dk. Mwinyi.
Dk. Mwinyi alisema kuwa Baraza la Uchunguzi limeshaundwa kuchunguza tukio hilo ambalo lina wajumbe tisa na linaongozwa na Meja Jenerali Sylvester Chacha Rioba. Wajumbe wa baraza hilo ni pamoja na wataalamu wa milipuko, wakemia, maboharia, Ofisa wa Polisi, Ofisa wa Idara ya Zimamoto na Ofisa Mhakiki Mali. Hadidu rejea kwa baraza hilo ni pamoja na kuchunguza na kubaini chanzo, madhara, hasara na kupendekeza hatua za kuchukuliwa ili kuzuia tukio kama hilo lisitokee tena. Sambamba na baraza, hatua za ziada zinachukuliwa kuepusha tukio kama hilo lisitokee katika maghala mengine.
“Tahadhari ya usalama inatolewa kwa wananchi wote wasiokote au kuficha chuma chochote kilichotokana na mlipuko, silaha, risasi zilizosambaa eneo la mlipuko na kwenye makazi. Vitu vya aina hiyo vitolewe taarifa kwa timu ya wanajeshi wanaovikusanya au kituo cha Polisi, ni kosa la jinai kama mtu atapatikana anahifadhi silaha, risasi au mlipuko wa aina yoyote”, alisisitiza Waziri huyo.
Waziri huyo alisema kazi ya kusafisha eneo la makazi ya wananchi kwa kuondoa vipande vya mabomu na mabaki ya makombora inaendelea na kuwataka wananchi watoe ushirikiano kwa wanajeshi kuwaonyesha yalipo mabaki. Aprili 29, mwaka huu, ghala lililokuwa limehifadhi silaha ndogondogo, mabomu, makombora na risasi katika kambi ya Jeshi Mbagala lililipuka na kusababisha vifo vya wanajeshi hao na raia 18 sambamba na nyumba kadhaa kuharibika.
Wakati huohuo, serikali imesema kwa mujibu wa tathmini kaya 3,750 za wakazi wa eneo la Mbagala Kuu hazina mahala pa kuishi baada ya nyumba zao kuharibiwa vibaya na milipuko hiyo ya mabomu. Aidha, Sh milioni 660.2 zimechangwa na watu mbalimbali ikiwamo serikali kwa ajili ya kusaidia ununuzi wa chakula, maji, mahema, nguo na mahitaji mengine muhimu.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kupokea msaada wa Sh milioni 5.2 kutoka kwa Jumuiya ya Mabohora Dar es Salaam, iliyoongozwa na Makamu Mwenyekiti wake, Zainuddin Adamjee, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi alisema kwa mujibu wa tathmini hiyo mpaka sasa nyumba 4,636 zimeharibika vibaya. “Tunajaribu kufanya kila tunaloweza kuwasaidia waathirika wa tukio hili na tayari serikali imetoa mifuko 3,750 ya mchele ambapo kila kaya itapewa mfuko mmoja wa kilo 30 na maharage kilo 10,” alisema Lukuvi.
Alisema pamoja na hayo wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwamo ya ukosefu wa mahema ambayo mpaka sasa yamepatikana 87 wakati mahitaji halisi ni mahema 550. “Hapa Tanzania hakuna mahala pa kununua mahema hivyo tunategemea kuazima, tumeaongea na Shirika la Umoja wa Mataifa la Wakimbizi (UNHCR) bado tunasubiri,” alisema. Alisema kwa sasa kinachoendelea ni tathmini ambapo timu za wathamini zimeanza kazi lakini zimeongezewa nguvu na wathamini kutoka Morogoro, Pwani na Tanga na wamezungumza na Mkuu wa Chuo cha Ardhi ambaye ameahidi kuongeza wahitimu 20 wa tathmini katika timu hiyo ili kuweza kufanya tathmini ya nyumba lakini pia pamoja na mali.
Akizungumzia wagonjwa, alisema hadi sasa katika Hospitali ya Temeke wapo 12 na wengine 15 wameongezeka jana ambao kati yao tisa wamelazwa, waliokufa ni raia 18 na maiti zote zimetambuliwa ikiwapo iliyoopolewa jana katika mto Mzinga na kati ya maiti hizo 15 zimezikwa Dar es Salaam moja Singida. Kwa upande wa misaada, Lukuvi alisema serikali imetoa Sh milioni 200, Ofisi ya Waziri Mkuu Sh milioni 200, Bakhresa Sh milioni 100, Quality Group milioni 30, Mwenyekiti wa IPP Reginald Mengi Sh milioni 25, Vodacom Sh milioni 20, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Sh milioni 20, manispaa zote tatu Ilala, Temeke na Kinondoni Sh milioni 60 na Mabohora Sh milioni 5.2.
Alisema fedha hizo zimetumika kulipia gharama za mazishi, kununulia vyakula, maji, nguo kama vile mablanketi na vyandarua, posho za wathamini, mafuta ya magari na posho za askari Polisi 100 wanaolinda eneo la kambi. Naye Meya wa Manispaa ya Temeke, Jerome Bwanausi, alisema kutokana na malalamiko ya baadhi ya waathirika kwamba misaada haiwafikii mengi ni ya uongo na kwamba timu iliyopangwa kugawa misaada hiyo inagawa kulingana na tathmini inayofanywa na idadi ya kaya. Wakati gazeti hili likiwa eneo la maafa, lilishuhudia kikosi cha askari wa JWTZ kikifukua kifusi cha nyumba zilizobomoka huku kikitoa tahadhari kwa watu kukaa mbali kutokana na kuwapo uwezekano wa mabomu ambayo hayajalipuka
(chanzo: www.habarileo.co.tz,
Imeandikwa na Maulid Ahmed na Halima Mlacha; Tarehe: 5th May 2009 @ 08:48)
Labels:
habari na matukio,
Tanzania,
Ulinzi na Usalama
Friday, 1 May 2009
Ajali na Mlipuko wa mabomu Mbagala, Dar
11 wafa kwa mabomu
Watu 11 wakiwamo wanajeshi sita, wamethibitika kufa katika milipuko ya makombora na mabomu iliyotokea juzi katika kambi ya maghala ya silaha ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Mbagala Kizuiani, Dar es Salaam. Idadi hiyo ya vifo imeongezeka ikilinganishwa na ya juzi, ambapo ilithibitika kuwa watu watatu walikufa katika milipuko hiyo wote wakiwa raia, akiwamo mwanamke mkazi wa Mbagala Kuu eneo la Mwanamtoti aliyekatwa kiuno na chuma cha makombora.
Pamoja na watu hao pia askari sita wengine haijulikani walipo huku wagonjwa zaidi ya 117 wakiwa bado wamelazwa katika hospitali za Temeke na Muhimbili wakiendelea na matibabu na wengine wawili wamelazwa katika Chumba cha Wagonjwa Wanaohitaji Uangalizi Maalumu (ICU).
Rais Jakaya Kikwete jana alitembelea kambi hiyo akifuatana na mawaziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Lawrence Masha, Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe, Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Emmanuel Nchimbi, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange na wakuu wa usalama akiwamo Mkuu wa Polisi (IGP) Said Mwema.
Akitoa taarifa ya athari ya tukio hilo ambalo bado chanzo chake hakijabainika mbele ya Rais Kikwete, Mkuu wa Tiba wa JWTZ, Profesa Brigedia Jenerali Yadon Kohi, alisema mpaka sasa majeruhi waliohusika katika tukio hilo ni 163 na kati yao 35 wamelazwa wakiwa na majeraha makubwa. “Wagonjwa 24 wamelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kati yao, saba wamejeruhiwa vibaya na watatu wamelazimika kufanyiwa operesheni ya dharura jana (juzi) usiku,” alisema Kohi.
Alisema wagonjwa 11 wamelazwa katika Hospitali ya Temeke huku wengine 117 wakifanyiwa uchunguzi na 11 ndio waliopoteza maisha wakiwamo watano raia na sita askari Jeshi ambao watano wamebainika kufa baada ya kupatikana kwa viungo vyao kama vile vipande vya miguu na nyama vikiwa vimezagaa eneo la tukio na mmoja kufia hospitalini. Alisema kati ya raia watano, wanne kati yao walikufa papo hapo kutokana na athari za milipuko ya mabomu hayo, mmoja ni mtoto aliyekufa kwenye Mto Mzinga alikotumbukia wakati akikimbia kuokoa maisha yake.
Naye Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Luteni Jenerali Abdulrahaman Shimbo, akitoa taarifa ya athari za tukio hilo kwa upande wa Jeshi, alisema milipuko ya mabomu hayo imesababisha hasara kubwa katika maghala hayo ya silaha ambazo hata hivyo idadi na kiasi cha hasara kimetakiwa kisitajwe. Alisema kambi hiyo ambayo ni kiungo cha masuala ya kitaalamu cha Jeshi ilianzishwa mahsusi kwa madhumuni ya kuandaa silaha na zana za kupelekwa Msumbiji na nyingine za dharura.
“Hata askari waliopangiwa kwenda Darfur kama silaha zao zikipatikana na hitilafu huletwa katika kambi hii kuchunguzwa na hupewa nyingine,” alisema Shimbo wakati akitoa mfano wa matumizi halisi ya kambi hiyo. Naye Mkuu wa Kikosi cha Anga, Brigedia Jenerali, F. Olomi, akitoa taarifa ya kambi kwa Rais alisema tukio hilo limesababisha hasara kwa kuharibu kabisa baadhi ya ofisi za kambi hiyo ikiwa ni pamoja na kuteketeza nyumba 50 za raia.
“Hali ilikuwa mbaya, mabomu yalikuwa yanaruka yametekeza ofisi, mashubaka ya kuhifadhia makombora na vifaa vya Jeshi baadhi vimeungua na nyumba 50 za raia zimeteketea kwa moto na nyingine mabati yametoka na kuta kudondoka,” alisema Olomi.
Alisema kazi kubwa kwa Jeshi hilo kwa kushirikiana na vyombo vingine vya Dola, ilikuwa ni kuhakikisha usalama wa raia kutokana na milipuko hiyo ya makombora kusababisha mengine kuruka hadi umbali wa kilometa 21. “Bomu moja aina ya roketi limeokotwa leo (jana) eneo la Banana karibu na Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere,” alisema.
Pamoja na hayo Olomi alisema bado askari hao hadi jana walikuwa wakiendelea kukagua na kukusanya mabaki ya makombora ambayo hayakulipuka, lakini yaliruka hadi maeneo ya raia na maroketi ambayo yamezagaa katika maeneo mbalimbali ya Mbagala.
Katika ziara hiyo, Rais Kikwete ambaye hakuzungumza chochote zaidi ya kutoa pole kwa wahusika, alitembelea kambi hiyo, baadhi ya maeneo ya wananchi ambayo yameathirika, Hospitali ya Temeke na Muhimbili ambako alizungumza na kuwafariji wagonjwa.
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Temeke, Dk. Aisha Mahita, akitoa taarifa yake kwa Rais, alisema wagonjwa 210 walifikishwa hospitalini hapo jana miongoni mwao wakiwamo walioumia vibaya na hadi jana walibaki wagonjwa 39 huku wengine wakiruhusiwa na wengine wakihamishiwa katika hospitali nyingine kutokana na hali zao kuwa mbaya.
Wakati katika Taasisi ya Mifupa (MOI) pekee kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Taasisi hiyo, Jumaa Almasi walikuwapo wagonjwa 25, kati yao wanane waliruhusiwa, 13 wamelazwa ambao kati yao wawili wamelazwa ICU.
Katika wodi nyingine ambazo Rais Kikwete alitembelea ikiwamo ya Mwaisela kulikuwa na wagonjwa sita wakiwamo waliovunjika miguu, kiuno na wengine kuishiwa nguvu huku kukiwa na taarifa za kuwapo wagonjwa wengine katika wodi ya Kibasila, lakini idadi yake haikuweza kupatikana mara moja.
Aidha gazeti hili lilitembelea kambi ya Jeshi Kituo cha Mgulani (JKT) ambako kulihifadhiwa watoto na watu wazima 255 waliokimbia milipuko hiyo ya mabomu na hadi jana bado kulikuwa na watu 83 ambao hawajaonana na familia zao kati yao wakiwamo watoto 61 na watu wazima 22.
Aidha kwa uchunguzi uliofanywa na 'HabariLeo' imebainika kuwa baadhi ya wazazi wakazi wa Mbagala jana bado walikuwa wakitafuta watoto na ndugu zao ambapo wengine walifanikiwa kuwaona na wengine bado wanaendelea kuwatafuta.
Hata hivyo kwa tathmini ya haraka iliyofanywa na gazeti hili, hali ya kambi hiyo imeonekana kutulia huku kukiwa hakuna hatari ya kutokea tena kwa milipuko hiyo, ingawa bado kuna hofu kwa baadhi ya wakazi wa eneo hilo ambao walijikusanya wengi barabarani wakati Rais Kikwete alipotembelea eneo hilo.
Kwa upande wake, Kamanda wa Kanda Maalumu Mkoa wa Dar es Salaam, Suleiman Kova, wakati akihojiwa asubuhi na Taasisi ya Taifa ya Utangazaji (TBC) alisema vurugu kubwa na kuumia kwa watu wengi juzi kulitokana udanganyifu na vitisho vilivyokuwa vikisambazwa kwa njia ya simu na baadhi ya watu.
“Watu walizidisha uongo kuliko hali halisi ya tukio, mtu anatuma ujumbe mfupi eti kuna bomu kubwa linasubiriwa likilipuka Dar es Salaam nzima itateketea, jamani kukitokea hali kama hii tulieni msubiri maelekezo kutoka vyombo vya Dola,” alisema. Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), umetoa salamu za rambirambi na pole kwa wafiwa waliopoteza ndugu zao na kujeruhiwa katika tukio hilo. “Tunaamini tukio hili ni bahati mbaya na kamwe si hujuma.”
source: www.habarileo.co.tz (Imeandikwa na Halima Mlacha; Tarehe: 1st May 2009)
Watu 11 wakiwamo wanajeshi sita, wamethibitika kufa katika milipuko ya makombora na mabomu iliyotokea juzi katika kambi ya maghala ya silaha ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Mbagala Kizuiani, Dar es Salaam. Idadi hiyo ya vifo imeongezeka ikilinganishwa na ya juzi, ambapo ilithibitika kuwa watu watatu walikufa katika milipuko hiyo wote wakiwa raia, akiwamo mwanamke mkazi wa Mbagala Kuu eneo la Mwanamtoti aliyekatwa kiuno na chuma cha makombora.
Pamoja na watu hao pia askari sita wengine haijulikani walipo huku wagonjwa zaidi ya 117 wakiwa bado wamelazwa katika hospitali za Temeke na Muhimbili wakiendelea na matibabu na wengine wawili wamelazwa katika Chumba cha Wagonjwa Wanaohitaji Uangalizi Maalumu (ICU).
Rais Jakaya Kikwete jana alitembelea kambi hiyo akifuatana na mawaziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Lawrence Masha, Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe, Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Emmanuel Nchimbi, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange na wakuu wa usalama akiwamo Mkuu wa Polisi (IGP) Said Mwema.
Akitoa taarifa ya athari ya tukio hilo ambalo bado chanzo chake hakijabainika mbele ya Rais Kikwete, Mkuu wa Tiba wa JWTZ, Profesa Brigedia Jenerali Yadon Kohi, alisema mpaka sasa majeruhi waliohusika katika tukio hilo ni 163 na kati yao 35 wamelazwa wakiwa na majeraha makubwa. “Wagonjwa 24 wamelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kati yao, saba wamejeruhiwa vibaya na watatu wamelazimika kufanyiwa operesheni ya dharura jana (juzi) usiku,” alisema Kohi.
Alisema wagonjwa 11 wamelazwa katika Hospitali ya Temeke huku wengine 117 wakifanyiwa uchunguzi na 11 ndio waliopoteza maisha wakiwamo watano raia na sita askari Jeshi ambao watano wamebainika kufa baada ya kupatikana kwa viungo vyao kama vile vipande vya miguu na nyama vikiwa vimezagaa eneo la tukio na mmoja kufia hospitalini. Alisema kati ya raia watano, wanne kati yao walikufa papo hapo kutokana na athari za milipuko ya mabomu hayo, mmoja ni mtoto aliyekufa kwenye Mto Mzinga alikotumbukia wakati akikimbia kuokoa maisha yake.
Naye Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Luteni Jenerali Abdulrahaman Shimbo, akitoa taarifa ya athari za tukio hilo kwa upande wa Jeshi, alisema milipuko ya mabomu hayo imesababisha hasara kubwa katika maghala hayo ya silaha ambazo hata hivyo idadi na kiasi cha hasara kimetakiwa kisitajwe. Alisema kambi hiyo ambayo ni kiungo cha masuala ya kitaalamu cha Jeshi ilianzishwa mahsusi kwa madhumuni ya kuandaa silaha na zana za kupelekwa Msumbiji na nyingine za dharura.
“Hata askari waliopangiwa kwenda Darfur kama silaha zao zikipatikana na hitilafu huletwa katika kambi hii kuchunguzwa na hupewa nyingine,” alisema Shimbo wakati akitoa mfano wa matumizi halisi ya kambi hiyo. Naye Mkuu wa Kikosi cha Anga, Brigedia Jenerali, F. Olomi, akitoa taarifa ya kambi kwa Rais alisema tukio hilo limesababisha hasara kwa kuharibu kabisa baadhi ya ofisi za kambi hiyo ikiwa ni pamoja na kuteketeza nyumba 50 za raia.
“Hali ilikuwa mbaya, mabomu yalikuwa yanaruka yametekeza ofisi, mashubaka ya kuhifadhia makombora na vifaa vya Jeshi baadhi vimeungua na nyumba 50 za raia zimeteketea kwa moto na nyingine mabati yametoka na kuta kudondoka,” alisema Olomi.
Alisema kazi kubwa kwa Jeshi hilo kwa kushirikiana na vyombo vingine vya Dola, ilikuwa ni kuhakikisha usalama wa raia kutokana na milipuko hiyo ya makombora kusababisha mengine kuruka hadi umbali wa kilometa 21. “Bomu moja aina ya roketi limeokotwa leo (jana) eneo la Banana karibu na Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere,” alisema.
Pamoja na hayo Olomi alisema bado askari hao hadi jana walikuwa wakiendelea kukagua na kukusanya mabaki ya makombora ambayo hayakulipuka, lakini yaliruka hadi maeneo ya raia na maroketi ambayo yamezagaa katika maeneo mbalimbali ya Mbagala.
Katika ziara hiyo, Rais Kikwete ambaye hakuzungumza chochote zaidi ya kutoa pole kwa wahusika, alitembelea kambi hiyo, baadhi ya maeneo ya wananchi ambayo yameathirika, Hospitali ya Temeke na Muhimbili ambako alizungumza na kuwafariji wagonjwa.
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Temeke, Dk. Aisha Mahita, akitoa taarifa yake kwa Rais, alisema wagonjwa 210 walifikishwa hospitalini hapo jana miongoni mwao wakiwamo walioumia vibaya na hadi jana walibaki wagonjwa 39 huku wengine wakiruhusiwa na wengine wakihamishiwa katika hospitali nyingine kutokana na hali zao kuwa mbaya.
Wakati katika Taasisi ya Mifupa (MOI) pekee kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Taasisi hiyo, Jumaa Almasi walikuwapo wagonjwa 25, kati yao wanane waliruhusiwa, 13 wamelazwa ambao kati yao wawili wamelazwa ICU.
Katika wodi nyingine ambazo Rais Kikwete alitembelea ikiwamo ya Mwaisela kulikuwa na wagonjwa sita wakiwamo waliovunjika miguu, kiuno na wengine kuishiwa nguvu huku kukiwa na taarifa za kuwapo wagonjwa wengine katika wodi ya Kibasila, lakini idadi yake haikuweza kupatikana mara moja.
Aidha gazeti hili lilitembelea kambi ya Jeshi Kituo cha Mgulani (JKT) ambako kulihifadhiwa watoto na watu wazima 255 waliokimbia milipuko hiyo ya mabomu na hadi jana bado kulikuwa na watu 83 ambao hawajaonana na familia zao kati yao wakiwamo watoto 61 na watu wazima 22.
Aidha kwa uchunguzi uliofanywa na 'HabariLeo' imebainika kuwa baadhi ya wazazi wakazi wa Mbagala jana bado walikuwa wakitafuta watoto na ndugu zao ambapo wengine walifanikiwa kuwaona na wengine bado wanaendelea kuwatafuta.
Hata hivyo kwa tathmini ya haraka iliyofanywa na gazeti hili, hali ya kambi hiyo imeonekana kutulia huku kukiwa hakuna hatari ya kutokea tena kwa milipuko hiyo, ingawa bado kuna hofu kwa baadhi ya wakazi wa eneo hilo ambao walijikusanya wengi barabarani wakati Rais Kikwete alipotembelea eneo hilo.
Kwa upande wake, Kamanda wa Kanda Maalumu Mkoa wa Dar es Salaam, Suleiman Kova, wakati akihojiwa asubuhi na Taasisi ya Taifa ya Utangazaji (TBC) alisema vurugu kubwa na kuumia kwa watu wengi juzi kulitokana udanganyifu na vitisho vilivyokuwa vikisambazwa kwa njia ya simu na baadhi ya watu.
“Watu walizidisha uongo kuliko hali halisi ya tukio, mtu anatuma ujumbe mfupi eti kuna bomu kubwa linasubiriwa likilipuka Dar es Salaam nzima itateketea, jamani kukitokea hali kama hii tulieni msubiri maelekezo kutoka vyombo vya Dola,” alisema. Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), umetoa salamu za rambirambi na pole kwa wafiwa waliopoteza ndugu zao na kujeruhiwa katika tukio hilo. “Tunaamini tukio hili ni bahati mbaya na kamwe si hujuma.”
source: www.habarileo.co.tz (Imeandikwa na Halima Mlacha; Tarehe: 1st May 2009)
Friday, 6 March 2009
Hotuba ya Mhe Rais Kikwete (Jeshini)
HOTUBA YA MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NA AMIRI JESHI MKUU WA JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA, KWENYE UZINDUZI WA KAMANDI YA JESHI LA NCHI KAVU YA JESHI LA ULINZI WA
WANANCHI WA TANZANIA, MSANGANI, PWANI,
TAREHE 04 FEBRUARI, 2009
Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la
Kujenga Taifa;
Mheshimiwa Naibu Waziri wa Elimu na
Mafunzo ya Ufundi;
Mheshimiwa Mkuu wa Majeshi;
Mnadhimu Mkuu wa Jeshi;
Mheshimiwa Katibu Mkuu;
Waheshimiwa Viongozi wa Serikali;
Wakuu wa Majeshi Wastaafu; Wanadhimu Wakuu
Wastaafu na Majenerali Wastaafu
Kamanda Kamandi ya Nchi Kavu;
Ndugu Makamanda na Wapiganaji;
Wageni Waalikwa;
Mabibi na Mabwana.
Napenda kuanza kwa kutoa shukrani zangu za dhati kwa heshima mliyonipa ya kunishirikisha kwenye sherehe hii adhimu ya uzinduzi wa Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania. Kunishirikisha kwenu kwenye tukio hili muhimu kunanipa faraja kubwa kwani nami ninakuwa sehemu muhimu ya historia ya maendeleo ya Jeshi letu.
Waheshimiwa Mawaziri, Makamanda na Wapiganaji;
Siku ya leo ni siku muhimu sana katika historia ya jeshi letu. Ni siku ambayo tunashuhudia mabadiliko ya muundo wa kiutawala na kiutendaji wa Jeshi letu ukizinduliwa rasmi kwa uzinduzi wa Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu. Sasa majukumu na mamlaka ya kiutendaji ya Jeshi letu lote yamepangwa kwa Kamandi. Pamoja na Kamandi hii tunayo Kamandi ya Jeshi la Anga na Kamandi ya Jeshi la Majini.
Kama mtakavyokumbuka, mapema miaka ya 80 tulikuwa na Kamandi mbili tu, yaani ya Ulinzi wa Anga na ya Wanamaji. Shughuli nyingine zote za Jeshi ambazo sasa tumezindua Kamandi yake ya Nchi Kavu, yaani Vikosi, Brigedi na wakati ule Divisheni za askari wa miguu zilikuwa zinafanywa Makao Makuu ya Jeshi. Kamandi mpya ya Jeshi la Nchi Kavu sasa ndiyo yenye jukumu la uongozi na usimamizi wa shughuli za kiutawala na kiutendaji za siku kwa siku za vikosi na brigedi. Makao Makuu ya Jeshi sasa yanabakia na majukumu ya msingi yanayohusu Jeshi zima ya sera, mikakati, na uratibu. Makao Makuu ya Jeshi yanahusika pia na masuala ya uwezeshaji wa Kamandi zake tatu na maslahi ya Wanajeshi kwa ujumla ili waweze kutimiza ipasavyo wajibu wao.
Nakupongeza sana CDF kwa uamuzi wako wa busara wa kufanya mabadiliko katika muundo wa Jeshi letu. Ni mabadiliko yanayoenda na wakati. Ndiyo maana sikusita kiyaunga mkono na kuyakubali. Nafarijika sana ninapoona Jeshi letu likijitahidi kuendeleza msukumo wa historia yake ya kubadilika kuendana na mabadiliko ya nyakati. Hiyo ndiyo siri kubwa ya uimara na mafanikio ya Jeshi letu.
Tangu Jeshi letu lianziswe mwaka 1964, limeshafanya mabadiliko mengi, ya kimuundo na kiutendaji kama matakwa ya kimazingira, kiutendaji na kiteknolojia yalivyojitokeza. Uzinduzi wa Kamandi hii unadhihirisha dhamira ya Jeshi letu ya kwenda na wakati. Mimi naamini ni mabadiliko yenye maslahi kwa Jeshi letu. Yatakaleta ufanisi na kuliimarisha Jeshi letu kwa utendaji kivita na kiutawala. Nawashukuru sana viongozi wa Jeshi na Wizara. Naomba muendelee kuwa wabunifu ili muendelee kufanya mabadiliko stahiki zaidi kwa nia ya kupata ufanisi mkubwa zaidi. Nasema tena hongereni sana.
Mheshimiwa Waziri, CDF, Makamanda na Askari;
Kuundwa kwa Kamandi hii, kunaleta uwiano wa kiutendaji kati ya Kamandi hii na Kamandi nyingine za Jeshi la Anga na Jeshi la Majini, hivyo kuongeza ufanisi katika utendaji wa Jeshi letu. Muundo huu pia, utasaidia kuleta ulinganifu wa mifumo ya Jeshi letu na majeshi ya nchi nyingine jirani katika jumuiya ya Afrika Mashariki na SADC na hata mataifa mengine rafiki duniani ambayo tunashirikiana nayo kwa mambo mbalimbali kama vile mazoezi na operesheni za pamoja. Hii itawasaidia wanajeshi wetu kushiriki kwa ufanisi zaidi kwenye mashirikiano hayo.
Ndugu Makamanda na Askari;
Wakati tunazindua Kamandi hii na kupongezana napenda kuwaomba muendelee kuwa wabunifu, mfikirie na kufanya mabadiliko zaidi yanayostahili ili muendelee kujiimarisha na kwenda na wakati. Ni muhimu kwa ajili hiyo mkaangalia miundo ya utumishi wa Jeshi, ikama, mitaala ya ufundishaji, zana na vifaa mbalimbali vya kijeshi ili navyo viendane na wakati. Napenda kuwahakikisheni kuwa Serikali itaendelea kuwaunga mkono katika jitihada zenu kadiri uwezo wa bajeti yetu utakavyoruhusu. Kwa moyo huo huo wa kuendelea kuwaunga mkono ndiyo maana nimekubali kuongeza umri wa kustaafu wa wanajeshi nchini kuwa miaka 60 badala ya 57 ya sasa. Mabadiliko hayo yatakayoanza Julai Mosi mwaka huu tunayafanya ili yaendane na wakati. Siku hizi watu wanachelewa kuzeeka tofauti na ilivyokuwa zamani,
Mheshimiwa Waziri; Naibu Waziri;
CDF, Makanda na Askari;
Nitakuwa mwizi wa fadhila kama sitaitumia nafasi hii, kwa mara nyingine kuwapongeza Wanajeshi wetu wote kwa kazi nzuri mnayoifanya ya kulinda uhuru na mipaka ya nchi yetu. Septemba Mosi, mwaka huu JWTZ litatimiza miaka 45 tangu kuasisiwa kwake. Imekuwa ni miaka 45 ya utumishi uliotukuka na mafanikio makubwa. Jeshi letu limetekeleza majukumu yake kwa ushujaa, umahiri, utii na uaminifu wa hali ya juu. Jeshi letu limezingatia kwa dhati misingi ya uweledi na uzalendo. Matokeo yake ni usalama na utulivu endelevu wa nchi yetu na watu wake. Tumefanikiwa kulinda mipaka ya nchi yetu wakati wote hata pale palipotokea tishio la wazi la nchi kuvamiwa na sehemu kutekwa na majeshi ya fashisti Idd Amin wa Uganda mwaka 1978. Nakumbuka Operesheni CHAKAZA mwaka 1978 – 1979. Nawapongeza sana.
Ndugu Makamanda na Askari;
Leo tunapozindua Kamandi hii, ninayo imani kubwa kwamba Jeshi letu litaendelea kujengeka na kwamba tutegemee mafanikio makubwa zaidi siku za usoni. Jeshi letu linaimarika zaidi na hivyo litaweza kutimiza vizuri zaidi jukumu lake la msingi la kulinda mipaka ya nchi yetu. Uimara utokao ogopesha wajinga wa nje na ndani kutothubutu kuchezea uhuru na mipaka ya nchi yetu. Jeshi letu pia litaendelea kutimiza ipasavyo wajibu wake wa kimataifa. JWTZ nao uzoefu wa kutosha na uweledi mkubwa katika nyanja za kimataifa. Limeshashiriki kwa ufanisi mkubwa katika operesheni nyingi, ndani na nje ya nchi. JWTZ limefundisha wapigania uhuru wa nchi za Kusini mwa Afrika wakati wa vita vya ukombozi. Sasa linaendekea kutoa mafunzo kwa wanajeshi wa nchi rafiki. JWTZ limeshiriki katika harakati na vita vya ukombozi na kuhami nchi marafiki.
Nazikumbuka operesheni KUMEKUCHA dhidi ya Wareno 1960, TEGAMA – Msumbiji, dhidi ya majeshi ya Rhodesia na Afrika Kusini, (1975 – 1980); SAFISHA – Msumbiji, dhidi ya RENAMO (1986 – 1988); Operesheni dhidi ya Mamluki waliovamia kisiwa cha Shelisheli mwaka (1981 – 1982) na hivi karibuni operesehni DEMOKRASIA huko Comoro mwezi Machi hadi Aprili, 2008 ya kumuondoa Kanali muasi Mohamed Bakar kutoka kisiwa cha Anjuan. Jeshi letu pia limekuwa linashiriki katika operesheni za kulinda amani chini ya Majeshi ya Umoja wa Mataifa. Hivi sasa tunajiandaa kwenda Darfur kwa ajili hiyo. JWTZ lina hazina kubwa ya uzoefu kutokana na operesheni hizo.
Ndugu Makamamanda na Wapiganaji;
Naomba nimalize kwa kuwashukuru tena, kwa kazi nzuri mnayoendelea kuifanya ya kulinda nchi yetu. Napenda kuwahakikishia kwamba Serikali inawajali na inathamini kazi yenu. Nawaomba msisahau kuwa siri kubwa ya mafaniko yetu Jeshini ni: Umoja, Ujasiri, Nidhamu na Uweledi. Yazingatieni. Nawatakia kila kheri katika majukumu yenu.
Asanteni sana.
WANANCHI WA TANZANIA, MSANGANI, PWANI,
TAREHE 04 FEBRUARI, 2009
Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la
Kujenga Taifa;
Mheshimiwa Naibu Waziri wa Elimu na
Mafunzo ya Ufundi;
Mheshimiwa Mkuu wa Majeshi;
Mnadhimu Mkuu wa Jeshi;
Mheshimiwa Katibu Mkuu;
Waheshimiwa Viongozi wa Serikali;
Wakuu wa Majeshi Wastaafu; Wanadhimu Wakuu
Wastaafu na Majenerali Wastaafu
Kamanda Kamandi ya Nchi Kavu;
Ndugu Makamanda na Wapiganaji;
Wageni Waalikwa;
Mabibi na Mabwana.
Napenda kuanza kwa kutoa shukrani zangu za dhati kwa heshima mliyonipa ya kunishirikisha kwenye sherehe hii adhimu ya uzinduzi wa Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania. Kunishirikisha kwenu kwenye tukio hili muhimu kunanipa faraja kubwa kwani nami ninakuwa sehemu muhimu ya historia ya maendeleo ya Jeshi letu.
Waheshimiwa Mawaziri, Makamanda na Wapiganaji;
Siku ya leo ni siku muhimu sana katika historia ya jeshi letu. Ni siku ambayo tunashuhudia mabadiliko ya muundo wa kiutawala na kiutendaji wa Jeshi letu ukizinduliwa rasmi kwa uzinduzi wa Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu. Sasa majukumu na mamlaka ya kiutendaji ya Jeshi letu lote yamepangwa kwa Kamandi. Pamoja na Kamandi hii tunayo Kamandi ya Jeshi la Anga na Kamandi ya Jeshi la Majini.
Kama mtakavyokumbuka, mapema miaka ya 80 tulikuwa na Kamandi mbili tu, yaani ya Ulinzi wa Anga na ya Wanamaji. Shughuli nyingine zote za Jeshi ambazo sasa tumezindua Kamandi yake ya Nchi Kavu, yaani Vikosi, Brigedi na wakati ule Divisheni za askari wa miguu zilikuwa zinafanywa Makao Makuu ya Jeshi. Kamandi mpya ya Jeshi la Nchi Kavu sasa ndiyo yenye jukumu la uongozi na usimamizi wa shughuli za kiutawala na kiutendaji za siku kwa siku za vikosi na brigedi. Makao Makuu ya Jeshi sasa yanabakia na majukumu ya msingi yanayohusu Jeshi zima ya sera, mikakati, na uratibu. Makao Makuu ya Jeshi yanahusika pia na masuala ya uwezeshaji wa Kamandi zake tatu na maslahi ya Wanajeshi kwa ujumla ili waweze kutimiza ipasavyo wajibu wao.
Nakupongeza sana CDF kwa uamuzi wako wa busara wa kufanya mabadiliko katika muundo wa Jeshi letu. Ni mabadiliko yanayoenda na wakati. Ndiyo maana sikusita kiyaunga mkono na kuyakubali. Nafarijika sana ninapoona Jeshi letu likijitahidi kuendeleza msukumo wa historia yake ya kubadilika kuendana na mabadiliko ya nyakati. Hiyo ndiyo siri kubwa ya uimara na mafanikio ya Jeshi letu.
Tangu Jeshi letu lianziswe mwaka 1964, limeshafanya mabadiliko mengi, ya kimuundo na kiutendaji kama matakwa ya kimazingira, kiutendaji na kiteknolojia yalivyojitokeza. Uzinduzi wa Kamandi hii unadhihirisha dhamira ya Jeshi letu ya kwenda na wakati. Mimi naamini ni mabadiliko yenye maslahi kwa Jeshi letu. Yatakaleta ufanisi na kuliimarisha Jeshi letu kwa utendaji kivita na kiutawala. Nawashukuru sana viongozi wa Jeshi na Wizara. Naomba muendelee kuwa wabunifu ili muendelee kufanya mabadiliko stahiki zaidi kwa nia ya kupata ufanisi mkubwa zaidi. Nasema tena hongereni sana.
Mheshimiwa Waziri, CDF, Makamanda na Askari;
Kuundwa kwa Kamandi hii, kunaleta uwiano wa kiutendaji kati ya Kamandi hii na Kamandi nyingine za Jeshi la Anga na Jeshi la Majini, hivyo kuongeza ufanisi katika utendaji wa Jeshi letu. Muundo huu pia, utasaidia kuleta ulinganifu wa mifumo ya Jeshi letu na majeshi ya nchi nyingine jirani katika jumuiya ya Afrika Mashariki na SADC na hata mataifa mengine rafiki duniani ambayo tunashirikiana nayo kwa mambo mbalimbali kama vile mazoezi na operesheni za pamoja. Hii itawasaidia wanajeshi wetu kushiriki kwa ufanisi zaidi kwenye mashirikiano hayo.
Ndugu Makamanda na Askari;
Wakati tunazindua Kamandi hii na kupongezana napenda kuwaomba muendelee kuwa wabunifu, mfikirie na kufanya mabadiliko zaidi yanayostahili ili muendelee kujiimarisha na kwenda na wakati. Ni muhimu kwa ajili hiyo mkaangalia miundo ya utumishi wa Jeshi, ikama, mitaala ya ufundishaji, zana na vifaa mbalimbali vya kijeshi ili navyo viendane na wakati. Napenda kuwahakikisheni kuwa Serikali itaendelea kuwaunga mkono katika jitihada zenu kadiri uwezo wa bajeti yetu utakavyoruhusu. Kwa moyo huo huo wa kuendelea kuwaunga mkono ndiyo maana nimekubali kuongeza umri wa kustaafu wa wanajeshi nchini kuwa miaka 60 badala ya 57 ya sasa. Mabadiliko hayo yatakayoanza Julai Mosi mwaka huu tunayafanya ili yaendane na wakati. Siku hizi watu wanachelewa kuzeeka tofauti na ilivyokuwa zamani,
Mheshimiwa Waziri; Naibu Waziri;
CDF, Makanda na Askari;
Nitakuwa mwizi wa fadhila kama sitaitumia nafasi hii, kwa mara nyingine kuwapongeza Wanajeshi wetu wote kwa kazi nzuri mnayoifanya ya kulinda uhuru na mipaka ya nchi yetu. Septemba Mosi, mwaka huu JWTZ litatimiza miaka 45 tangu kuasisiwa kwake. Imekuwa ni miaka 45 ya utumishi uliotukuka na mafanikio makubwa. Jeshi letu limetekeleza majukumu yake kwa ushujaa, umahiri, utii na uaminifu wa hali ya juu. Jeshi letu limezingatia kwa dhati misingi ya uweledi na uzalendo. Matokeo yake ni usalama na utulivu endelevu wa nchi yetu na watu wake. Tumefanikiwa kulinda mipaka ya nchi yetu wakati wote hata pale palipotokea tishio la wazi la nchi kuvamiwa na sehemu kutekwa na majeshi ya fashisti Idd Amin wa Uganda mwaka 1978. Nakumbuka Operesheni CHAKAZA mwaka 1978 – 1979. Nawapongeza sana.
Ndugu Makamanda na Askari;
Leo tunapozindua Kamandi hii, ninayo imani kubwa kwamba Jeshi letu litaendelea kujengeka na kwamba tutegemee mafanikio makubwa zaidi siku za usoni. Jeshi letu linaimarika zaidi na hivyo litaweza kutimiza vizuri zaidi jukumu lake la msingi la kulinda mipaka ya nchi yetu. Uimara utokao ogopesha wajinga wa nje na ndani kutothubutu kuchezea uhuru na mipaka ya nchi yetu. Jeshi letu pia litaendelea kutimiza ipasavyo wajibu wake wa kimataifa. JWTZ nao uzoefu wa kutosha na uweledi mkubwa katika nyanja za kimataifa. Limeshashiriki kwa ufanisi mkubwa katika operesheni nyingi, ndani na nje ya nchi. JWTZ limefundisha wapigania uhuru wa nchi za Kusini mwa Afrika wakati wa vita vya ukombozi. Sasa linaendekea kutoa mafunzo kwa wanajeshi wa nchi rafiki. JWTZ limeshiriki katika harakati na vita vya ukombozi na kuhami nchi marafiki.
Nazikumbuka operesheni KUMEKUCHA dhidi ya Wareno 1960, TEGAMA – Msumbiji, dhidi ya majeshi ya Rhodesia na Afrika Kusini, (1975 – 1980); SAFISHA – Msumbiji, dhidi ya RENAMO (1986 – 1988); Operesheni dhidi ya Mamluki waliovamia kisiwa cha Shelisheli mwaka (1981 – 1982) na hivi karibuni operesehni DEMOKRASIA huko Comoro mwezi Machi hadi Aprili, 2008 ya kumuondoa Kanali muasi Mohamed Bakar kutoka kisiwa cha Anjuan. Jeshi letu pia limekuwa linashiriki katika operesheni za kulinda amani chini ya Majeshi ya Umoja wa Mataifa. Hivi sasa tunajiandaa kwenda Darfur kwa ajili hiyo. JWTZ lina hazina kubwa ya uzoefu kutokana na operesheni hizo.
Ndugu Makamamanda na Wapiganaji;
Naomba nimalize kwa kuwashukuru tena, kwa kazi nzuri mnayoendelea kuifanya ya kulinda nchi yetu. Napenda kuwahakikishia kwamba Serikali inawajali na inathamini kazi yenu. Nawaomba msisahau kuwa siri kubwa ya mafaniko yetu Jeshini ni: Umoja, Ujasiri, Nidhamu na Uweledi. Yazingatieni. Nawatakia kila kheri katika majukumu yenu.
Asanteni sana.
Tuesday, 20 January 2009
Simu ya Polisi Arusha
Polisi Arusha watoa namba mpya kudhibiti uhalifu
Wakazi wa Arusha wametakiwa kutumia simu namba
0767 750173,
kutoa taarifa za dharura kwa jeshi la Polisi Mkoani humo iwapo kutatokeaa tatizo lolote la uhalifu katika eneo husika.
Akiongea na vyombo vya habari ofisini kwake, Kaimu Kamanda wa Polisi,Mkoa wa Arusha, Roberti Boaz, alisema kuwa, simu hiyo ni maalum kwakutumia ujumbe wa maneno kwa gharama nafuu.
"lengo la kutoa namba hii, kurahisisha utoaji wa taarifa kwa wananchi,wengine wanapata tukio ila wanashindwa kuja polisi kwa umbali, lakinikwa kutumia simu itasaidia kushirikiana" alisema Boaz
(chanzo: Faustine's Baraza)
Wakazi wa Arusha wametakiwa kutumia simu namba
0767 750173,
kutoa taarifa za dharura kwa jeshi la Polisi Mkoani humo iwapo kutatokeaa tatizo lolote la uhalifu katika eneo husika.
Akiongea na vyombo vya habari ofisini kwake, Kaimu Kamanda wa Polisi,Mkoa wa Arusha, Roberti Boaz, alisema kuwa, simu hiyo ni maalum kwakutumia ujumbe wa maneno kwa gharama nafuu.
"lengo la kutoa namba hii, kurahisisha utoaji wa taarifa kwa wananchi,wengine wanapata tukio ila wanashindwa kuja polisi kwa umbali, lakinikwa kutumia simu itasaidia kushirikiana" alisema Boaz
(chanzo: Faustine's Baraza)
Labels:
Arusha,
Mambo ya Ndani,
Tanzania,
Ulinzi na Usalama
Subscribe to:
Posts (Atom)