Showing posts with label Siasa na Uraia. Show all posts
Showing posts with label Siasa na Uraia. Show all posts

Friday, 12 June 2009

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, WAKATI AKIWAHUTUBIA WANANCHI WA DODOMA, NA WABUNGE KWENYE UKUMBI WA KILIMANI, DODOMA TAREHE 10 JUNI, 2009



Waheshimiwa Wabunge;
Ndugu wananchi;
Nawashukuru kwa dhati wazee wangu, Waheshimiwa Wabunge na wananchi wenzangu wa Dodoma, kwa kuitikia wito wangu wa kuja kukutana na kuzungumza nanyi. Nakushukuru Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa na Katibu wa Baraza la Wazee kwa maandalizi mazuri.
Mara kadhaa katika hotuba zangu za siku za nyuma, nimekuwa nikielezea jinsi ambavyo uchumi wa dunia unavyopita katika misukosuko mikubwa na jinsi ambavyo mtikisiko huo unavyoweza kuathiri uchumi wetu pia. Tayari athari zake tumezipata na tunaendelea kuathirika nazo. Nilifanya uamuzi siku za nyuma wa kuunda kikundi kazi cha watalaam chini ya uongozi wa Gavana wa Benki Kuu, Profesa Benno Ndulu, kufanya uchambuzi wa hali ilivyo ili kubaini athari tulizopata na kushauri hatua za kunusuru uchumi wetu na kujenga uwezo wa kujihami na kukuza uchumi.

Ndugu Wananchi;
Wenzetu hao wamemaliza kazi yao na taarifa yao imeshajadiliwa na Baraza la Mawaziri na maamuzi kufanywa. Matokeo yake ni kuwepo kwa mkakati wa Kunusuru Uchumi wa Tanzania dhidi ya Msukosuko wa Uchumi wa Duniani. Katika mkakati huo mpango wa utekelezaji wa malengo na hatua mbalimbali za kuchukua zimeanishwa.

Mtikisiko Katika Mfumo wa Fedha Duniani
Ndugu Wananchi;
Uchumi wa dunia unakabiliwa na matatizo makubwa sana ambayo hayajawahi kutokea kwa zaidi ya miaka 60. Mara ya mwisho uchumi wa dunia ulikuwa na matatizo makubwa katika miaka 1930 lakini nayo hayakuwa makubwa kama ilivyo safari hii. Matatizo ya uchumi wa dunia yana sura mbili. Upande mmoja lipo tatizo la kuvurugika kwa masoko na mfumo wa fedha wa kimataifa. Na, upande wa pili kudorora kwa uchumi wa dunia kulikosababishwa na kuanguka kwa masoko ya fedha na mitaji.

Tatizo hili limeanzia Marekani kutokana na udhaifu katika usimamizi wa mfumo wa fedha na hasa mikopo. Baadae ukaenea Ulaya Magharibi na hatimaye dunia nzima na siye tukiwemo. Kiwango cha athari kinatofautiana kutoka nchi moja na nyingine. Mataifa makubwa kiuchumi ya Marekani, Ulaya na Asia yameathirika zaidi kuliko nchi maskini za Afrika. Hata hivyo, mataifa makubwa yana uwezo mkubwa zaidi wa kukabiliana na athari hizo pamoja na ukubwa wake. Mataifa maskini kama yetu hayana uwezo wa kukabiliana hata na hizi athari ndogo zinazotukabili. Kinachoonekana kidogo kwao, kwetu sisi ni kikubwa.
Mabenki mengi, makubwa kwa madogo, na asasi za fedha kubwa na ndogo katika mataifa tajiri zimeshashuhudiwa zikianguka kibiashara au kufilisika. Masoko ya hisa na mitaji nayo hivyo hivyo yameanguka kwa kiasi ambacho hakijawahi kufikiwa. Makampuni mengi madogo na makubwa yameanguka. Watu wengi wenye hisa wamejikuta wakiharibikiwa na hata kuwa maskini bila kutazamia.
Makampuni mengi yameanguka kibiashara na kufilisika. Watu wamepoteza ajira kwa mamilioni na wengi wamepoteza nyumba na mali walizozipata kwa mikopo kwa sababu ya kushindwa kulipa mikopo. Kwa ujumla hali ya kiuchumi na kimaisha katika nchi hizo ni ngumu kwa makampuni mengi na watu wengi.
Kutokana na hali hii, uwekezaji umepungua, biashara ya ndani na nje imeshuka, uzalishaji viwandani umepungua sana na kwingine umesimama, makampuni madogo na hata makubwa na yenye heshima yamefilisika, ununuzi wa bidhaa umepungua, watu kwa mamilioni wakakosa ajira katika nchi kubwa kiuchumi. Athari hizo bado zinaendelea na matokeo yake ni kuzorota kwa ukuaji wa uchumi wa mataifa hayo makubwa na uchumi wa dunia kwa ujumla. Mwaka 2008, uchumi wa nchi hizi ulikua kwa asilimia 0.9. na mwaka huu inatarajiwa utapungua kwa asilimia 3.8.
Hali hii imezilazimisha Serikali za nchi hizo kuingilia kati na kutumia fedha za Serikali kuokoa makampuni binafsi, kinyume kabisa na falsafa ya soko huria. Vilevile, Serikali za nchi hizo zikalazimika kukopa fedha nyingi kwa ajili ya miradi mingi mikubwa ili kuchochea shughuli za kiuchumi.

Athari kwa Tanzania
Ndugu Wananchi,
Kwa upande wetu hapa nchini mabenki yetu yako salama kwa vile hatujafungamanishwa na masoko ya fedha ya kimataifa. Lakini, kibiashara na baadhi ya shughuli za kiuchumi, tumeathirika hasa zile zinazotegemea masoko ya kimataifa hususan ya mataifa tajiri ya Marekani, Ulaya na Asia. Athari kubwa ya kwanza ni ile ya kupungua kwa bei na masoko ya bidhaa zetu tunazouza nje ya nchi hususan mazao ya kilimo, madini na bidhaa za viwandani. Kadhalika, sekta ya utalii nayo imeathirika na kupungua kwa watalii wanaokuja nchini. Vilevile uwekezaji wa kutoka nje umepungua.
Kwa upande wa mauzo ya mazao ya kilimo napenda nitoe mifano ya pamba, kahawa na hata maua na karafuu. Kwa pamba, kwa kipindi kifupi cha miezi minne kuanzia Septemba 2008 bei ya pamba ilianguka kutoka senti 82 za dola kwa paundi moja mpaka senti 40. Hivyo pamba iliyonunuliwa kwa bei ya juu toka kwa wakulima, ghafla ilibidi iuzwe kwa bei ya chini na nyingine kukosa soko kabisa. Hadi mwezi Aprili 2009 marobota 124,344 ya pamba yalikuwa bado hayajauzwa. Inakadiriwa kuwa hasara iliyopatikana kwa kuuza pamba nje kwa bei chini ya bei ya kununulia ni kadiri ya shilingi bilioni 15 na 18. Unapochanganya tatizo hili na lile la pamba kutokuuzwa, shilingi bilioni 93.6 zilizokopeshwa na CRDB peke yake (bila kujumuisha riba) hazijarejeshwa. Kati ya madeni hayo, shilingi bilioni 4.6 ni ya vyama vya ushirika na TSh bilioni 81.9 ni ya makampuni 24 makubwa yanayofanya biashara ya pamba.
Vilevile, kwa upande wa zao la kahawa, kutoka mwezi Oktoba, 2008 bei zilianza kushuka kutoka wastani wa US$ 140 kwa gunia la Arabica hadi wastani wa US$ 104.21. Robusta nayo ilishuka toka wastani wa US$ 91 kwa gunia hadi dola za Marekani 64 ilipofika mwezi Machi 2009, ikiwa ni anguko la bei la asilimia 26 kwa Arabica na asilimia 29 kwa Robusta. Kahawa iliyokumbwa na msukosuko huo ni kiasi cha kilo 26,645,439 za Arabica zenye thamani ya US$ 55,536,099 na kilo 11,981,710 za Robusta zenye thamani ya US$ 15,469,353.
Kutokana na bei za kununulia kahawa hizo kwa mkulima (farm gate price) kuwa za juu kuliko ile ya kuuzia kwenye soko la dunia, vyama vya ushirika vya kahawa na wafanyabiashara walionunua kahawa wamepata hasara inayokadiriwa kuwa TSh bilioni 4.85.

Ndugu Wananchi;
Hasara waipatayo wanunuzi na ugumu waupatao kuuza mazao yao kunasababisha washindwe kulipa madeni yao Benki na kuwaweka kwenye hatari ya kufilisiwa mali zao walizoweka dhamana. Aidha, kwa ukubwa wa mikopo ambayo haijalipwa na ambayo huenda isilipwe itayafanya mabenki yaliyokopesha kupata hasara. Pia mabenki hayo yanaweza kukataa kuwakopesha wanunuzi wa mazao na kusababisha mgogoro mwingine mkubwa wa mazao ya wakulima kutokununuliwa msimu ujao. Jambo hilo likitokea litafanya wakulima kula hasara na kuwa maskini zaidi.
Shabaha ya mkakati wetu ni kumpunguzia mnunuzi mzigo wa hasara na madeni, kuiepusha benki na hasara na kuwezesha mazao ya mkulima kuendelea kununuliwa.
Kwa upande wa kilimo cha maua na mboga mambo ni hayo hayo. Bei imeshuka kwa asilimia 25 na mauzo yamepungua kwa sababu mahitaji katika masoko ya nje yamepungua kutokana na hali mbaya ya uchumi katika nchi hizo. Kuna hatari kwamba wakulima wa maua watashindwa kulipa mikopo ya mabenki ya Tshs. bilioni 43.4, ajira za watu zitapotea (tayari Mount Meru Flowers imepunguza watumishi 36). Sekta hii inaajiri watu 3,000 na wengi wao ni wanawake. Ni dhamira yetu pia hapa kuwanusuru wakulima, mabenki na ajira.

Madini
Ndugu Wananchi;
Hali ni mbaya pia kwa upande wa bei na masoko ya vito hasa almasi na Tanzanite. Bei ya Tanzanite imeshuka kwa asilimia hamsini na kufikia US$200 kwa karati. Bei ya almasi imeshuka kwa asilimia 26 na kuwa US$8,870 mwezi Septemba. Wachimbaji na wanunuzi wa almasi, Tanzanite na vito vinginevyo wanakabiliwa na tatizo kubwa la madini ambayo wanapata taabu kuyauza.
Bahati nzuri dhahabu haina matatizo hayo. Soko lake ni zuri na bei ni nzuri sana. Mkakati wetu unalenga namna ya kuwasaidia wachimbaji wa vito ambao tusipowasaidia wao na serikali tutaendelea kukosa mapato na wakati huo watu wengine watakosa ajira kwa sababu ya shughuli za uchimbaji kupungua.

Viwanda na Utalii
Ndugu Wananchi;
Viwanda vyetu navyo hasa vya nguo, nyuzi, mavazi na vile vya ngozi vimeathirika na msukosuko wa uchumi wa dunia. Mauzo nje yamepungua sana na kusababisha hasara kubwa. Uzalishaji umepungua, ajira nazo hali kadhalika.
Sekta ya Utalii ambayo ndiyo sekta kiongozi kwa mapato ya fedha za kigeni nayo imebanwa pia. Idadi ya Watalii wanaokuja nchini inapungua. Takwimu zinaonyesha idadi hiyo kupungua kwa asilimia 10. Mapato yatokanayo na utalii ya mwezi Januari – Aprili, 2009 nayo yamepungua na kufikia US$302.1 kutoka US$388.2 milioni mwaka 2008. Hali hiyo inaathari kubwa kwa wawekezaji na kwa mapato ya Serikali na fedha za kigeni hivyo nayo tumeipa uzito stahiki katika mkakati wa kunusuru uchumi.

Mapato ya Ndani
Ndugu wananchi,
Kutokana na matatizo ya kupungua mauzo nje, utalii, uwekezaji n.k mapato ya ndani ya Serikali nayo yameathirika. Sasa hivi, tunakusanya mapato kutoka ushuru wa forodha, kodi za ndani n.k yako chini ya kiwango tulichotarajia. Kama mwenendo wa makusanyo ya kodi utaendelea kama ulivyo sasa, makusanyo ya kodi kwa mwaka 2008/09 yatakuwa chini ya makadirio ya bajeti kwa asilimia 10. Kwa maneno mengine, tutashindwa kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 472.9 ambazo matumizi yake tulishayapangia kwenye bajeti. Katika mkakati huo tumeweka mipango ya kuikabili hali hiyo katika mwaka huu wa fedha na mwaka ujao pia ambapo tunadhani athari zitakuwepo au hata kuzidi.

Mapato ya Fedha za Kigeni
Ndugu Wananchi;
Kwa sababu ya kupungua kwa mauzo ya mazao yetu nje, mapato yetu ya fedha za kigeni yatapungua pia. Inakadiriwa kuwa thamani ya mauzo nje itapungua kutoka US$ 2,891 milioni mwaka 2008/09 hadi US$2,860 milioni mwaka 2009/10. Wakati huo huo mapato ya fedha za kigeni kutokana na utalii yatapungua kwa US$ 186 milioni. Katika mkakati wetu tunayo mipango ya kuziba pengo hilo ili kuepuka matatizo ya upatikanaji wa fedha za kigeni kwa ajili ya manunuzi yetu ya nje.

Uwekezaji kutoka nje
Ndugu Wananchi;
Kwa sababu ya matatizo ya uchumi uwekezaji wa vitega uchumi kutoka nje umepungua. Wawekezaji wamekuwa wanakosa fedha kutoka mabenki na masoko ya mitaji. Matokeo yake ni kuchelewa au kukosa kabisa au kuahirishwa miradi mikubwa ambayo ingetoa mchango muhimu kwa ukuaji wa uchumi wetu na ajira. Kwa mfano: Mradi wa umeme wa MW 300 kule Mtwara kwa sababu ya Barrick Gold Ltd. kujitoa na Artumas peke yake haina uwezo wa kifedha; mradi wa nickel Kabanga, mradi wa aluminium smelter, Mtwara; mradi wa usambazaji umeme mkoani Mtwara, miradi ya viwanda vya saruji na mbolea Mtwara na uwekezaji katika utafutaji wa madini umepungua kutoka US$90 mpaka US$40 milioni.

Ajira
Ndugu Wananchi;
Hali ya ajira nchini nayo itakuwa mbaya kutokana na matatizo haya. Mwaka 2009 ni mwaka ambao athari za msukosuko zimeanza kujitokeza kwa nguvu katika masoko ya ajira na kusababisha watu wengi kupoteza kazi na hivyo kuongeza umaskini wa kipato.
Hadi kufikia Aprili 2009 jumla ya wafanyakazi 48,000 walikuwa wamepoteza ajira zao nchini. Kutokana na kutarajiwa kupungua kwa idadi ya watalii wanaokuja nchini, baadhi ya hoteli zilizotarajiwa kuwapokea watalii hao zimelazimika kupunguza wafanyakazi wao kutokana na kupungua kwa biashara. Kati ya asilimia 20-30 za ajira katika sekta ya utalii ZanzĂ­bar ziko hatarini kupotea kutokana na upungufu wa utalii.
Vivyo hivyo, katika sekta ya kilimo, viwanda na madini, watu wengine wanatarajiwa kupoteza kazi zao.

Kupungua kwa ukuaji wa uchumi
Waheshimiwa Wabunge, Ndugu Wananchi,
Matokeo ya athari zote hizi ni kupungua kwa kasi ya ukuaji wa uchumi nchini. Kama mjuavyo, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, uchumi wetu umekuwa ukikua kwa kiwango cha juu cha wastani wa asilimia 7.2. Tulitegemea mwaka huu uchumi wetu ungekuwa kwa zaidi ya asilimia 8 na kufikia asilimia 10 mwaka 2010 kama tulivyoahidi kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2005. Lakini kama wasemavyo Waswahili, ng’ombe wa maskini hazai. Msukosuko wa fedha na uchumi duniani umesababisha ukuaji wa uchumi wa Tanzania kupungua kutoka asilimia 7.4 mwaka jana hadi kati ya asilimia 5-6 mwaka huu. Kwa upande wa Zanzibar, uchumi wao unategemewa kukua kwa asilimia 4.5 mwaka huu ukilinganisha na asilimia 5.4 mwaka jana.

Mkakati wa Kuhami na Kuunusuru Uchumi
Ndugu Wananchi;
Baada ya kutafakari hali hii, na kuchambua athari hizi nilizobainisha kwa uchumi, ustawi na mipango ya muda mrefu ya maendeleo ya Taifa letu, na kwa kuzingatia azma yangu niliyoitangaza kwenye salamu ya mwaka mpya wa 2009, kwamba mwaka huu ni mwaka wa kuhami na kukuza uchumi, tumebuni na tutatekeleza Mkakati Maalum wa Kuhami na Kuunusuru Uchumi wa Tanzania.
Mkakati huu unazingatia ukweli kuwa msukosuko wa uchumi duniani ni wa kupita. Changamoto ya muda mfupi ni jinsi ya kujinusuru na hatimaye kudumisha juhudi za maendeleo baada ya msukosuko kupita.
Katika kukabili athari hizi nilizozitaja, tunalenga mambo mawili makuu. Kwanza ni kupunguza makali ya msukosuko, na pili, kulinda uwekezaji ambao ni muhimu katika kudumisha ukuaji endelevu wa uchumi katika kipindi cha muda wa kati.
Mkakati wetu wa kuhami na kuunusuru uchumi unalenga kukabili matatizo ya mpito na dharura – hasa ya ukwasi (liquidity) na siyo ufilisi (solvency). Mkakati huu sio mbadala wa mipango ya maendeleo na bajeti ya Serikali ya kila mwaka. Chini ya mkakati huu Serikali imepima matatizo kwa uzito wake na kushughulikia yale tu yaliyojitokeza hivi karibuni kutokana na msukosuko wa uchumi na siyo vinginevyo.

Ndugu Wananchi;
Tumetengeneza Mkakati huu kutimiza malengo makubwa manne:
1. Kulinda ajira na vipato vya wananchi;
2. Kuhakikisha upatikanaji wa chakula;
3. Kulinda uwekezaji muhimu katika miradi ya maendeleo, hususan miundombinu, na
4. Kulinda programu muhimu za kijamii

Ndugu Wananchi;
Kama nilivyosema, lengo kuu la kwanza la mkakati huu ni kupunguza makali au kuhimili shinikizo la msukosuko, hususan kuwalinda wananchi walio katika hatari kubwa zaidi ya kimaisha. Katika kutekeleza hili lengo yako mambo kadhaa ambayo tutayafanya:
(i) Kufidia hasara waliyopata wanunuzi wa mazao msimu wa 2008/09
Serikali imeamua kufidia vyama vya ushirika na makampuni yaliyonunua mazao ya wakulima na kuyauza kwa hasara. Hasara hiyo inayokisiwa kufikia shilingi 21.9 bilioni imepatikana kutokana na bei ya kuuzia mazao hayo kuwa chini sana ya gharama iliyotumika kuyanunua. Serikali italipa madeni yenye thamani ya hasara hiyo, moja kwa moja kwa mabenki yaliyokopesha vyama na makampuni hayo. Lakini tutafanya uhakiki kabla ya kulipa. Napenda kusisitiza kuwa hatutalipa madeni ya zamani ambayo hayahusiki na msukosuko wa uchumi wa dunia.

(ii) Kutoa udhamini wa kuahirisha mikopo ya waathirika
Yapo madeni ambayo wakopaji kwa sababu ya msukosuko wa uchumi wa dunia wanapata matatizo kulipa kwa wakati. Kundi hili linawajumuisha wengi wenye viwanda, wenye shughuli za utalii, kilimo n.k. Madeni hayo yanafikia Shs.270 bilioni.
Serikali itayadhamini madeni na kuyataka mabenki kuahirisha ulipaji wa mikopo hiyo na riba yake wa miaka miwili. Udhamini wa Serikali utatolewa kwa uwiano wa kila shilingi moja kwa shilingi tano na Serikali ikidhamini asilimia 70 ya mkopo. Kwa uwiano huu, fedha zitakazohitajika katika dhamana hiyo ni TSh 45 bilioni. Pamoja na kutoa nafuu kwa makampuni lakini hatua hii pia itayawezesha mabenki kuendelea kutoa mikopo na hivyo shughuli za kiuchumi na biashara hazitaisimama.

(iii) Kutoa mitaji ya uendeshaji (working capital) kwa riba nafuu
Tumeamua vilevile kuchukua hatua za kupunguza upungufu wa mitaji ya uendeshaji (working capital). Kwa ajili hiyo Serikali itayakopesha mabenki fedha kwa riba nafuu ya asilimia 2 ili na wao wawakopeshe wafanyabiashara fedha za mitaji ya uendeshaji kwa riba nafuu. Lengo ni kusaidia walioko kwenye sekta zinazokumbwa na msukosuko wa uchumi waweze kuhimili vishindo. Kwa kila shilingi moja tutakayotoa sisi Serikali, benki husika itatakiwa itoe shilingi moja na nusu (1:1½).
Kwa madhumuni haya, tutaanzisha mfuko maalumu wenye shilingi bilioni 80 ambao utasimamiwa na Benki Kuu na mabenki yatakayoshiriki yatatakiwa kutoa shilingi 120 bilioni. Viwango vya riba kwa wakopaji vitapangwa kwa maelewano ya pamoja baina ya BoT na mabenki na itategemea sekta na shughuli yenyewe.

(iv) Kuboresha Mifuko ya Dhamana:
Chini ya mkakati huu tutaiboresha na kuiongezea fedha mifuko ya kudhamini mikopo (credit guarantee schemes). Mifuko hiyo ni pamoja na Mfuko wa Udhamini wa Uuzaji wa Mazao Nje ya Nchi (Export Credit Guarantee Scheme -ECGS) na Mfuko wa Udhamini wa Mikopo kwa Wajasiliamali Wadogo na wa Kati (SME Credit Guarantee Scheme). Tutaongeza mtaji wa shilingi bilioni 10 kwa kila mfuko katika mwaka wa fedha wa 2009/10. Nyongeza hii itawezesha kuongeza dhamana ya mikopo ya shilingi bilioni 65 kwenye Mfuko wa Udhamini wa Uuzaji wa Mazao Nje ya Nchi na shilingi bilioni 60 kwenye Mfuko wa Udhamini wa Mikopo kwa Wajasiliamali Wadogo na wa Kati katika kuchochea mauzo ya bidhaa nje na uzalishaji. Hivi sasa mfuko wa ECGS una mtaji wa Shs.32.5 bilioni na umekopesha Shs.161.5 bilioni na ule wa SME una Shs.500 milioni na umeshakopesha Shs.6.5 bilioni.

(v) Kupunguza gharama za vito vya thamani:
Katika sekta ya vito vilivyoshuka bei kwa kiasi kikubwa, kama vile Tanzanite na almasi, tunaangalia uwezekano wa kuahirisha ulipaji wa mrahaba (royalty) kwa wachimbaji wa vito. Lengo ni kuwapa muda wa kupumua na kujijenga. Chini ya mpango huu Serikali itaahirisha mapato ya kiasi cha US$ milioni 0.5 kutoka almasi na US$ milioni 2.5 kutoka tanzanite.

(vi) Kuongeza uzalishaji wa Chakula
Ndugu Wananchi;
Lengo lingine muhimu la mkakati huu ni kuinusuru nchi kutokana na athari za upungufu wa chakula duniani zilizochochewa na msukosuko. Katika kutekeleza hili, mkakati huu utahakikisha kuwa miradi yote ya kilimo, hususan ile ya uzalishaji wa mazao ya chakula, inaendelea kugharimiwa bila kuathiriwa na msukosuko. Lengo la kwanza ni kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula ili kujitosheleza kwa chakula na kuuza ziada nje na hivyo kutumia ipasavyo fursa inayotokana na kuadimika kwa chakula duniani.
Chini ya mkakati huu, pamoja na kuendelea kuhimiza na kusimamia yale mambo yote ya kuongeza tija na uzalishaji kwenye kilimo, tumeamua katika kipindi hiki kufanya yafuatayo: (i) kutoa mikopo nafuu na ya muda mrefu ya shilingi 20 bilioni kupitia TIB kwa sekta binafsi kwa ajili ya kuendeleza kilimo (ii) kutoa shilingi bilioni 20 kwa ajili ya mkopo wa riba nafuu kwa zana za kilimo kama matrekta madogo kupitia mpango wa karadha (lease finance), ambapo, kwa kila shilingi ambayo serikali itatoa, mabenki yatakayoshiriki katika mkakati huu itabidi nayo yatoe shilingi moja: na (iii) Kuongeza kiasi na idadi ya wakulima watakaopata mbolea ya ruzuku kwa utaratibu wa vocha. Benki ya Dunia watatupa mkopo wa US$46 milioni na sisi tutatoa kiasi hicho hicho kwenye mfuko wa mbolea katika mwaka ujao wa fedha (2009/10).
Aidha tumeamua sasa tutumie Hifadhi ya Chakula ya Taifa kusaidia kutuliza bei za vyakula kwa walaji. Tunaiboresha sera ya sasa ambapo Hifadhi hungojea ilani ya njaa. Tumesema kupanda sana kwa bei za vyakula vikuu katika soko ni dalili ya upungufu hivyo kupunguza makali kila inapowezekana. Chini ya mkakati huu, tutatoa shilingi bilioni 20 kwa Hifadhi ya Chakula ya Taifa kwa ajili ya kuongeza akiba ya chakula na kudhibiti mfumuko wa bei.

Miundombinu
Ndugu Wananchi,
Kuhusu lengo la kulinda uwekezaji muhimu, hasa katika miundombinu, ya umeme na reli tumekubaliana kuwa tuendeleze juhudi za kutafuta mikopo kutoka Benki ya Dunia na mashirika mengine ya fedha. Kwa ajili hiyo tutatumia fedha za IMF kukwamua mradi wa usambazaji umeme Mtwara. Zinatakiwa US$ 7 milioni. Kuhusu Shirika la Reli, sisi tuchangie sehemu yetu, yaani US$43 milioni, kuongezea US$ 40milioni za Benki ya Dunia kuimarisha reli yetu. Wakati huo suala la uendeshaji tulitafutie jawabu muafaka.
Kadhalika tumekubaliana kuwa taendelee kuwekeza katika ujenzi wa barabara na miradi ya elimu, afya na maji. Suala la hati-fungani ambalo liliahirishwa kwa sababu ya matatizo ya soko la fedha tulitafutie vyanzo mbadala.

Ndugu Wananchi;
Tumekubaliana pia katika mkakati huu, kuwa lazima kuhakikisha kuwa utulivu wa uchumi unakuwepo ili kuhimiza ukuaji endelevu wa uchumi na kuvutia sekta binafsi kushiriki. Vilevile tuongeze kasi ya kuharakisha uimarishaji wa TIB na uanzishwaji wa Agricultural Development Bank.

Ndugu Wananchi;
Kuhusu lengo la Mkakati la kulinda programu muhimu za kijamii, Serikali itahakikisha kuwa mipango yote ya kijamii haitaathirika, hata ile ambayo itakosa fedha za kutosha kutoka kwa wafadhili. Hii inajumuisha mipango ya utoaji wa ruzuku kwa dawa za kurefusha maisha kwa wagonjwa wa UKIMWI, vyandarua vya kuzuia malaria, programu za kifua kikuu, na nyingine za kusaidia juhudi za vijana na kulinda makundi ya wanyonge.

Ndugu Wananchi;
Pia zipo hatua kadhaa nyingine za kisera ambazo Serikali inaziandaa katika kukabiliana na athari za msukosuko huu. Katika miezi inayokuja, Wizara mbalimbali zitatangaza hatua za kisera zenye nia ya kuzihami sekta hizo na athari hizi na kuchochea ukuaji wa sekta mbalimbali kama vile utalii na viwanda. Miongoni mwa hatua tunazoziandaa sasa ni kupunguza gharama za visa kwa watalii kutoka dola 100 na 200 na kuwa dola 50. hazina inaangalia uwezekano wa kufanya hivyo.

Namna Serikali Itakavyolipia Gharama za Programu Hii
Ndugu Wananchi;
Kutekeleza Mkakati huu ni gharama kubwa. Zitahitajika kiasi cha shilingi bilioni 1,692.5. Tumetenga pesa hizo katika Bajeti yetu ya mwaka wa fedha utakaoanza Julai, 1, 2009. Sehemu kubwa ni fedha zetu lakini pia tutapata misaada kutoka kwa marafiki zetu wa maendeleo hasa Benki ya Dunia, IMF, EU na India.

Hitimisho
Ndugu Wananchi,
Sasa nimefika mwisho wa hotuba yangu. Nawashukuru tena kwa kukubali wito wangu. Kwa nchi yetu ambayo bado ina safari ndefu katika maendeleo, hatua tuliyochukua hapa ni kubwa na ya kihistoria. Katika kuchukua hatua hii, tumezingatia mahitaji ya dhamana tuliyopewa na wananchi katika kuwaongoza na kusimamia maendeleo na ustawi wao na wa nchi yetu. Lakini vilevile, tumezingatia mafundisho ambayo historia ya nchi yetu imetupatia. Kwa mkakati huu, tumedhamiria kuepuka hali iliyojitokeza miaka ya 1980 ambapo kutokana na kushindwa kukabili kwa dhati na wakati muafaka, athari za kupanda kwa bei za mafuta na hali mbaya ya uchumi wa dunia iliyofuatia, zilisababisha nchi kupoteza miongo miwili ya ukuaji wa uchumi na mafanikio yaliyokuwa yamepatikana katika nyanja za jamii na miundombinu.
Mwisho kabisa, nawasihi viongozi wenzangu na wananchi kwa ujumla, tuwe wavumilivu na tuiunge mkono Serikali katika kutekeleza mkakati huu. Tangu mwaka 2006, mambo hayakuwa mepesi sana, tumepitia misukosuko mikubwa kwa uchumi wetu: mgao mkubwa wa umeme, njaa, bei kubwa ya mafuta na bei kubwa za vyakula na sasa msukosuko huu wa aina yake. Kwa kila tatizo tumepambana nalo kiume na kwa umakini mkubwa na kuvuka salama. Mshikamano wetu, umoja wetu ndiyo uliotufikisha hapo.
Napenda kuwahakikishia wananchi wa Tanzania kwamba Serikali yao inawajali na inafanya kila lililo ndani ya uwezo wake kutimiza wajibu wake katika kuwatumikia.
Sisi katika Serikali tupo kwa ajili yenu na tutaendelea kuwatumikia kwa nguvu zetu zote. Tutaendelea kutengeneza mipango na mikakati ya kukabiliana na matatizo na changamoto zinazowakabili wananchi wa Tanzania walioko katika kila kona ya nchi yetu. Tuliyaweza yale naamini na haya tutayamudu!!
Asanteni sana kwa kunisikiliza!
Mungu Ibariki Afrika!
Mungu Ibariki Tanzania!

Thursday, 11 June 2009

Hotuba ya Rais: Hatua za kuokoa uchumi

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425

PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mambo makuu katika Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Jakaya Mrisho Kikwete kwa Taifa kutoka Ukumbi wa Kilimani, Dodoma, – jumatano, Juni 10, 2009.

1. Rais ameelezea hali ya mtikisiko wa uchumi duniani, chimbuko la mtikisiko huo na athari za hali hiyo kwa uchumi wa Tanzania. Athari hizo ni kama ziafuatazo:

(a) Bei na mahitaji ya bidhaa za Tanzania kwenye masoko ya kimataifa yamepungua. Mifano ni mazao ya pamba, kahawa, karafuu,mwani na mazao mengine

(b) Mahitaji na bei za madini ya vito ya Tanzania pia vimepungua kwenye masoko ya kimataifa

(c) Mahitaji ya mazao ya kilimo ya Tanzania kama vile maua na mboga yamepungua pia na mauzo yake nchi za nje yameshuka kwa asilimia 25

(d) Viwanda vya ngozi, nguo, nyuzi na mavazi pia vimeathirika na hivyo kuathiri pia upatikanaji wa ajira nchini

(e) Sekta ya utalii ambayo ndiyo kubwa kwa uingizaji wa fedha za kigeni pia imeathirika kwa watalii wanaokuja nchini kupungua

(f) Mapato ya Serikali pia yamepungua na hivyo kuathiri mapato ya ndani na mapato ya fedha za kigeni

(g) Uwekezaji kutoka nje umepungua pia na baadhi ya makampuni yaliyokuwa yanataka kuja kuwekeza Tanzania, ama yameahirisha ama yamefuta mipango yao ya uwekezaji. Mifano ni mradi wa uwekezaji katika nickel pale Kabanga, Ngara, Kagera na miradi ya umeme, saruji, mbolea na aluminium smelter mkoani Mtwara

(h) Hali ya ajira nchini imekuwa mbaya zaidi kwa sababu ya matatizo hayo ya uchumi na hadi Aprili, mwaka huu, kiasi cha watu 48,000 walikuwa wamepoteza ajira

(i) Vile vile kasi ya kukua kwa uchumi wa Tanzania inakadiriwa kuwa itapungua kutoka kwenye asilimia 7.4 kama ilivyobashiriwa mwaka huu hadi kufikia asilimia 5 hadi 6



2. Kutokana na hali hiyo, Rais Kikwete ametangaza mkakati wa kuhami na kunusuru uchumi wa Tanzania kwa malengo makuu manne yafuatayo:



(a) Kulinda ajira na vipato vya wananchi

(b) Kuhakikisha upatikanaji wa chakula

(c) Kulinda uwekezaji muhimu katika miradi ya maendeleo, hususan miundombinu

(d) Kulinda programu muhimu za kijamii



3. Kutokana na hali hiyo, Rais ametangaza hatua zifuatazo katika kutekeleza mkakati huo wa kuunusuru uchumi (rescue package):

(a) Serikali imeamua kufidia hasara waliyopata wanunuzi wa mazao kwa msimu uliopita wa 2008/2009. Hasara hiyo ni kiasi cha bilioni 21.9 na Serikali italipia hasara hiyo ambayo imetokana na kushuka ghafla kwa bei ya mazao ya Tanzania kwenye soko la kimataifa

(b) Serikali itatoa udhamini kwa kuahirisha mikopo ya walioathirika ambao ni pamoja na viwanda, utalii, kilimo na sekta nyingi za uchumi kwa muda wa miaka miwili. Serikali imeyataka mabenki kutokutoza riba kwenye mikopo hiyo katika miaka hiyo miwili

(c) Serikali itatoa mitaji ya uendeshaji (working capital) kwa riba nafuu na itayakopesha mabenki kwa riba ndogo ya asilimia mbili na mabenki hayo yatatakiwa kuwakopesha wahitaji kwa riba ndogo zaidi kuliko ilivyo sasa.

(d) Serikali imedhamiria kuboresha mifuko ya dhamana ikiwa ni pamoja na mifuko ya kukopesha biashara ndogo ndogo kwa kuiongezea fedha zinazoweza kukopwa na wananchi

(e) Serikali imeamua kuongeza kasi ya uzalishaji chakula kwa kutoa mikopo ya thamani ya bilioni 20 kupitia Benki ya TIB, na pia kutoka kiasi kingine cha sh bilioni 20 kwa ajili ya mikopo yenye riba nafuu kwa ajili ya ununuzi wa zana za kilimo kupitia taasisi za karadha, na kuongeza idadi ya wakulima watakaopata mbolea ya ruzuku na kiasi cha bilioni 90 kwa ajili ya mboleo hiyo. Vile vile, Serikali imeamua kuanza kuutumia Mfuko wa Hifadhi ya Chakula (SGR) kupunguza bei ya vyakula kwa wananchi na hifadhi hiyo itaongezewa fedha za kununulia chakula zaidi

(f) Serikali imeamua kukwamua mradi wa kusambaza umeme mkoani Mtwara na pia kuboresha Reli ya Kati kwa kiasi cha dola za Marekani milioni 43.

(g) Serikali imeamua kuhakikisha kuwa programu zote za kijamii kama maji, elimu na afya kama vile ya kupambana na magonjwa ya ukimwi, kifua kikuu na malaria haziathiriki kwa sababu ya msukosuko wa sasa wa kiuchumi.

(h) MPANGO wote huu utaigharimu Serikali kiasi cha sh bilioni 1, 692.5 (karibu sh trilioni 1.7). Fedha hizo zimetengwa katika Bajeti ya Serikali ya mwaka 2009/2010 inayoanza Julai Mosi, 2009.

Sehemu kubwa ya fedha hizo ni za ndani ya nchi ingawa kutakuwapo na michango ya wabia wa maendeleo kama Benki ya Dunia, Shirika la Fedha Duniani (IMF), Serikali ya India na Umoja wa Ulaya (EU).


chanzo: www.tanzania.go.tz

Friday, 5 June 2009

Hotuba Bora (100%) kutoka kwa Rais Kikwete

HOTUBA YA MHE. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, KWENYE UZINDUZI WA KIVUKO CHA MV. MAGOGONI 4 JUNI 2009



Mheshimiwa Dk. Shukuru Kawambwa (Mb), Waziri wa Miundombinu,

Waheshimiwa Mawaziri,

Ndugu Viongozi na Watendaji wa Serikali,

Viongozi wa vyama vya siasa,

Ndugu Wananchi wenzangu,

Wageni waalikwa,

Mabibi na Mabwana,



Awali ya yote, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa kunialika kuja kujumuika nanyi hapa katika uzinduzi wa kivuko kipya cha Mv. Magogoni.

Nawapongeza sana wananchi wa Kigamboni na wa jiji la Dar es Salaam kwa jumla kwa kupata kivuko kipya kiitwacho MV. Magogoni. Kivuko hichi kipya, kikubwa na cha kisasa tumekinunua kutoka Ujerumani kwa gharama ya shilingi 8.5. bilioni. Kimetatua tatizo kubwa lililokuwa linawasumbua watu waliokuwa wanavuka kutoka au kwenda Kigamboni.

Kwa muda mrefu, wananchi wa Kigamboni wamekuwa wakipata adha ya usafiri, maisha yao kuwa hatarini na usalama wa mali zao kuwa mashakani. Vivuko vilivyokuwepo MV. Alina na MV. Kigamboni vilikuwa vimechakaa sana hivyo kushindwa kufanya kazi ipasavyo. Kwa kweli vilikuwa tishio kwa kila hali. Wakati wa kampeni za uchaguzi wa mwaka 2005, Chama cha Mapinduzi kiliahidi kupitia Ilani yake kutatua tatizo la vivuko kadhaa nchini, kimojawapo kikiwa hiki cha Kigamboni. Leo hii tunasherehekea kutimia kwa ahadi yetu kwa wananchi wa Dar es Salaa hasa wale waishio na waendao Kigamboni.

Kadhalika tumeshatimiza ahadi kwa wananchi wa Mwanza kwa kivuko cha Busisi (MV. Misungwi), kivuko cha Kisiwa cha Kome (MV. Kome) na kivuko cha kati ya Bugorora na Ukara (MV. Nyerere). Kwa wananchi wa Ruvuma kuna kivuko cha MV. Ruhuhu na wa Morogoro kivuko cha mto Kilombero.

Kivuko hiki tunachokizindua rasmi leo ndicho kikubwa kuliko vivuko vyote nchini. Kina uwezo mkubwa wa kubeba tani 500 yaani Magari 60 na abiria 2000 kwa wakati mmoja. Kwa kuwa na kivuko hiki tatizo la usafiri sasa siyo gumzo tena. Ifikapo mwezi Septemba, 2009 tatizo litakuwa limekwisha kabisa pale kivuko cha MV. Kigamboni kitakapoanza kazi. Hivi sasa kivuko hicho kinafanyiwa matengenezo makubwa kukirudisha katika kiwango cha juu cha ubora. Kadhalika kule Bususi, Mwanza nako matengenezo ya kivuko cha MV. Sengerema yatakapokamilika shughuli ya uvushaji watu kati ya Kigongo na Busisi katika Ziwa Victoria itakuwa imeimarika sana.



Ndugu Wananchi,

Nimefurahi kusikia kuwa ujenzi wa Kivuko Mv. Magogoni umefanyikia hapa Dar es salaam eneo la Bandari na kuweza kuwapatia ajira vijana 30 ambao wamejifunza na kupata maarifa na ufundi mpya wa ujenzi wa vivuko na hata maboti. Ninaamini kwa uzoefu walioupata wataweza kujiajiri wenyewe kwa kujenga vivuko na boti ndogondogo za uvuvi ili kujipatia riziki na kuboresha hali ya maisha yao.

Serikali itaendelea na utaratibu huu wa kujenga vivuko hapa nchini ili kutoa huduma nzuri ya usafiri wa majini na kuendeleza teknolojia ya ufundi wa kutengeneza vivuko hapa nchini, na kukuza ajira kwa vijana wetu.



Ndugu wananchi,

Ziko sehemu nyingi za nchi yetu ambako kufikika kwake ni kwa vivuko tu. Serikali imedhamiria kuhakikisha kuwa vivuko vyote nchini vinakuwa vya uhakika na salama kwa matumizi ya wananchi kwa kuvikarabati na kununua vipya pale vinapohitajika kadri uwezo wa bajeti ya serikali unavyoruhusu.

Katika kutekeleza hayo, Serikali kwa sasa inakarabati vivuko viwili vya Mv. Kigamboni hapa Dar es Salaam, na Mv. Sengerema huko Mwanza. Aidha, tumenunua vivuko vipya sita vya Kilombero huko Morogoro, Kivuko cha Mv. Nyerere kinachohudumia kati ya Bugorora na Ukara Mkoani Mwanza, Mv. Ruhuhu Mkoani Ruvuma, Mv. Misungwi kinachohudumia kati ya Kigongo hadi Busisi huko Mwanza na Mv. Kome II kinachofanya kazi kati ya Kisiwa cha Kome kwenda Nyakalilo. Vilevile, tutanunua vivuko vipya vya Musoma kwenda Kinesi Mkoani Mara ambapo wananchi wa Kinesi watakwenda Musoma mjini kwa kutumia kivuko kwa muda wa dakika 30 badala ya kuzunguka Kilometa 54, pia tunanunua vivuko vingine vipya vya Rugezi hadi Kisorya Wilayani Ukerewe, Utete mkoani Pwani na Pangani mkoani Tanga.

Vilevile, katika mipango ya miaka mitatu ijayo, Serikali inatarajia kununua vivuko vifuatavyo kuanzia 2009/10:

1. Kivuko cha tani 50 katika maeneo ya Kilambo - Mtwara. Kivuko hiki kitarahisisha usafiri eneo la mwambao wa kati ya Mtwara Tanzania na Msumbiji



2. Kivuko cha tani 50 kitakachotumika kati ya Msanga Mkuu na Mtwara Mjini ambapo kitapunguza usumbufu wa wananchi kuzunguka Km 20 kufika Mtwara.



3. Kivuko cha Mto Rusumo – Ngara Kagera ambapo kitapunguza Km 60 za kuzunguka kuja Bukoba Mjini.



4. Kivuko cha Kyela – Itungi Port wananchi watatumia nusu saa kusafiri kwa kivuko badala ya kuzunguka kwa Km 70 kufika Kyela.



Ndugu wananchi,

Kuna sehemu ambazo tunatumia vivuko kwa sababu ya kujenga madaraja haiwezekani kwa jinsi maumbile yake yalivyo. Lakini zipo sehemu ambazo tunatumia vivuko lakini madaraja yanawezekana kujengwa. Tunachelewa kujenga madaraja kwa sababu ya gharama kubwa na uwezo wetu mdogo wa fedha. Tunayo dhamira ya kujenga madaraja kidogo kidogo katika sehemu hizi.

Moja ya madaraja ambayo tumeshafanya uamuzi wa dhati kabisa kujenga ni Daraja la Kigamboni. Mipango ya ujenzi wa daraja hili imekuwapo tangu uhuru. Lakini sasa tumedhamiria kufanya. Tumeahidi katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM Ibara ya 44 (f) kwamba, katika kipindi cha miaka mitano tuwe tumeanza maandalizi ya ujenzi wa daraja hili. Nafurahi kwamba tutatimiza ahadi hiyo. Na tutafanya hivyo kwa kushirikiana na wenzetu wa sekta binafsi.

Tuko kwenye hatua nzuri za maandalizi. Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) lipo kwenye mchakato kumpata Mtaalam Mshauri ili atayarishe nyaraka za zabuni. Matumaini yetu ni kwamba, ifikapo mwezi Septemba mwaka huu, nyaraka hizo zitakuwa tayari. Mambo yote yakienda kama yalivyopangwa, basi ujenzi wa daraja unaweza kuanza katika mwaka wa fedha wa 2010/2011. Daraja hili litafungua kwa kiasi kikubwa fursa za uchumi na uwekezaji huko Kigamboni.

Vilevile, kwa sasa, tunafanya usanifu wa ujenzi wa daraja tuliloliahidi kwenye ibara ya 44 (i) ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM wa 2005, yaani Daraja la Mto Kilombero ili kuunganisha Wilaya za Kilombero na Ulanga.



Ndugu wananchi,

Hata hivyo, kujenga daraja kuvuka ng’ambo pekee hakutoshi kama barabara za Kigamboni haziko katika hali nzuri. Kwa kutambua hilo tunajenga barabara kwa kiwango cha lami kutoka Kivukoni hadi Mjimwema mpaka Kongowe. Barabara nyingine tutakayojenga kwa lami ni ya kutoka Kivukoni hadi Tungi na nyingine ni ile ya kutoka Mjimwema hadi Pembamnazi. Wakati tunajenga barabara hizi kwa lami, tutaendelea kuimarisha barabara nyingine za Kigamboni, kama ile ya Tungi hadi Kibada.



Ndugu wananchi,

Ukiacha hili la Kivuko ambalo tumelitimiza na barabara za Kigamboni, Serikali inaendelea na jitihada za kupunguza matatizo ya ya usafiri na usafirishaji katika Jiji la Dar es Salaam. Hivi sasa tunaelekeza nguvu zetu katika kujaribu kupunguza msongamano wa magari katika barabara za Dar es Salaam.

Kwa ajili hiyo, zipo barabara ambazo tunazifanyia ukarabati mkubwa ili zirudi katika hali yake ya zamani, kama tufanyavyo kwa barabara ya Mandela. Baadhi tunazijenga upya na kuzipanua kama ilivyo kwa barabara ya Sam Nujoma na barabara ya Kilwa. Nyote ni mashahidi wa kazi inayoendelea kufanyika katika barabara hizo.

Vilevile ziko barabara kadhaa za Dar es Salaam ambazo hivi sasa ni za udongo ambazo tumeamua tutazijenga kwa kiwango cha lami. Nia yetu kuu ni kupunguza msongamano katika baadhi ya mabarabara kwa kutoa fursa kwa magari kuchepukia barabara hizo. Tumekwishatoa kiasi cha shilingi bilioni 20 kwa ajili ya ujenzi na upanuzi wa barabara hizi. Baadhi ya barabara hizo ni pamoja na zifuatazo:

1. Barabara ya kutoka Ubungo Bus Terminal hadi Kigogo Roundabout, na kutoka Kigogo Roundabout hadi Mtaa wa Twiga Jangwani. Maombi yangu ni kwamba wasiue viwanja vya michezo vya Jangwani.



Nimeambiwa kuwa mikataba ya ujenzi wa barabara hizi itasainiwa wakati wowote wiki ijayo na ujenzi kuanza mara moja.



2. Barabara nyingine ni ile ya kutoka Tabata Dampo hadi Kigogo;



3. Vilevile iko barabara ya kutoka Ubungo Maziwa hadi Mabibo External;



4. Barabara ya kutoka Jet Club hadi Vituka hadi Davis Corner ya umbali wa kilomita 12;



5. Barabara ya kuanzia Mbezi Mwisho hadi Barabara ya Nyerere Ukonga Banana kupitia Malamba Mawili na Kinyerezi. Barabara hii itawezesha magari yanayotoka viwandani maeneo ya Nyerere Road kuweza kuanza safari za mikoani au nchi jirani bila kupitia Ubungo.



6. Barabara ya kutoka Tegeta Kibaoni hadi Mbezi Mwisho (Morogoro Road) kupitia Goba. Barabara hii itawawezesha wachukuzi wa saruji kutoka kiwandani Wazo Hill kwenda mikoani au nchi jirani bila kupitia mjini. Vilevile itawezesha wakazi wengi wa maeneo ya Bagamoyo Road, Tegeta na Mbweni kuweza kusafiri mikoani bila kupitia mjini.



7. Tunao mpango wa kutengeneza kwa lami barabara kutoka Tangi Bovu hadi Goba



8. Vilevile tunao mpango wa kupanua njia mbili kipande cha barabara kutoka njia panda ya Morocco hadi Kawe kuungana na barabara ya Bagamoyo kupitia Shoppers Plaza, kupitia Mikocheni na Mlalakua ili kupunguza msongamano mkubwa wa kipande kile cha barabara. Pia kuunganisha kipande cha kutoka Tume ya Sayansi hadi Msasani kwa Mwalimu Nyerere kwa barabara ya njia mbili.



9. Pia barabara ya Kimara Kinguruwe hadi Mabibo External nayo tutaijenga kwa lami. Barabara hii ya kilomita 9 itawezesha watu kupita kuja na kutoka mjini bila kupitia Ubungo;



10. Vilevile, ipo mipango ya kutengeneza kwa lami barabara ya Kimara Baruti hadi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kupitia Msewe na Changanyikeni.



11. Tumefanya mazungumzo mazuri na Serikali ya Japan wakati wowote tutapata majibu kuhusu utoaji fedha kwa ajili wa upanuzi wa barabara ya kutoka njia panda ya Morocco Road hadi Tegeta Kibaoni ambayo itapunguza sana msongamano wa magari Jijini.



Ndugu wananchi,

Nimeona niwape taarifa ya barabara hizi ili mjue hatua tunazochukua kupunguza tatizo la usafiri Dar es Salaam.



Usalama wa Vyombo vya Majini

Ndugu wananchi,

Hali ya usalama wa vyombo vya majini imekuwa siyo ya kuridhisha hata kidogo. Matukio ya ajali za vyombo vya majini hapa nchini yamekuwa mengi mno. Katika kipindi cha kuanzia Januari, 2006 hadi Desemba 2008 yamekuwepo matukio 28 ya ajali zilizo sababisha vifo vya watu 149 na 240 kuokolewa. Majuzi tena kumetokea ajali ya Meli ya Mv. Faith iliyopinduka katika Bandari ya Malindi kule Zanzibar.

Tathmini zinaonyesha kuwa ajali hizo zimekuwa zinasababishwa na ubovu wa vyombo unaochangiwa na umri mkubwa na matengenezo yasiyoridhisha, makosa ya kibinadamu na hali mbaya ya hewa. Wakati mwingine pia uelewa mdogo wa umuhimu na matumizi ya vifaa vya kuokolea umechangia vifo vya watu.

Serikali iliunda SUMATRA kwa nia ya kuboresha usimamizi wa uendeshaji wa vyombo vya majini ili kuongeza usalama wa usafiri majini. Tunaipongeza SUMATRA kwa kazi kubwa na nzuri ambayo imekuwa inafanywa tangu kuundwa kwake mpaka sasa. SUMATRA imeweka maafisa wasimamizi katika maeneo mbalimbali nchini ikiwa ni pamoja na Mwanza, Bukoba, Sumbawanga, Kigoma na Dar es Salaam. Hata hivyo, lazima SUMATRA waongeze udhibiti wa vyombo vinavyosafiri majini. Wawe makini zaidi katika kusimamia ubora wa vyombo hivyo, ujuzi wa manahodha na wafanyakazi wake, ubora wa huduma stahiki kwa abiria ikiwamo zile za kuokolea abiria panapotokea ajali.

Aidha SUMATRA iendelee kutoa mafunzo kwa wamiliki na waendesha vyombo vya usafiri majini ili kuwaongezea ufahamu juu ya umuhimu wa kuzingatia taratibu na kanuni zinazosimamia uendeshaji wa vyombo hivyo.



Ndugu wananchi,

Katika kuimarisha uwezo wetu wa kuzuia na kukabiliana na majanga kwenye maji, Serikali imejenga mnara wa kuongozea meli katika eneo la Magogoni ambao una kituo cha kuratibu shughuli za utafutaji na uokoaji pamoja na kuratibu matukio ya uharamia baharini. Kituo hiki kimezinduliwa mwezi Machi, 2009 na kwa muda mfupi wa uwepo wake, kimeweza kuratibu zoezi la utafutaji na uokoaji wa meli ya Comoro iliyopata ajali ikiwa safarini kutoka Dar es salaam kwenda Comoro tarehe 16 Aprili, 2009. Katika zoezi hilo watu 77 waliokolewa.



Ndugu wananchi,

Kabla sijamaliza, naomba niongelee uvumi ambao umeenea sana ndani ya jamii yetu, hasa kwa wakazi wa Kigamboni. Kumekuwa na upotoshaji mkubwa kwamba eneo zima la Kigamboni limeuzwa kwa wawekezaji. Wapo wanaodai kuwa Kigamboni imeuzwa kwa watu maarufu wa Marekani na wapo wanaodai kwamba imeuzwa kwa watu maarufu kutoka Uarabuni. Mwanzoni niliposikia maneno hayo niliyapuuza. Lakini nikagundua kuwa yameenea sana na yanaaminiwa na watu wengi hata wale ambao ungedhani wana uelewa wa juu wa mambo. Nikamuagiza Waziri wa Ardhi atoe ufafanuzi.

Ningependa nami kurudia kwamba hakuna ukweli kabisa katika uvumi huo. Ninachokijua mimi ni kuwa Jiji Dar es Salaam likishirikiana na Serikali Kuu (Wizara ya Adhi, Nyumba na Makazi) inao mpango kabambe wa kuufanya Kigamboni kuwa Mji Mpya. Hii ni kwa maana ya kwamba uwe umepangwa na kujengwa kisasa. Nia ni nzuri ya kuendeleza Kigamboni na jiji la Dar es Salaam kwa jumla hasa sasa ambapo kutajengwa daraja hivyo kushawishi watu wengi zaidi kupenda kuhamia na kuishi huko.

Tatizo kubwa la Dar es Salaam ni kuwa na nyumba nyingi kujengwa maeneo yasiyopimwa na kupangwa vizuri. Hali hii haikubaliki, tusiiache iendelee hivi. Na tusiiache Kigamboni nayo ikawa hivyo. Mwelekeo huo tayari upo. Ndiyo sababu ya uamuzi huo wa Jiji na Wizara ya Ardhi ambao nia yake ni njema, naomba tuwape ushirikiano na msaada unaostahili.



Ndugu Wananchi,

Naomba sasa nimalize kwa kuwakumbusha wenzetu wa Wizara na hasa TEMESA kuhakikisha kuwa kivuko hiki kunatunzwa ipasavyo. Kinafanyiwa matengenezo ya mara kwa mara kwa mujibu wa ratiba yake. Hamzidishi magari, abiria na mizigo kupita uwezo unaostahili. Tukifanya hayo kitadumu na kutuhudumia kwa miaka mingi kama ilivyokusudiwa. Tuukumbuke daima msemo wa Waswahili usemao “Kitunze Kidumu” na Kitunze Kikutunze” Tusifanye kinyume chake.

Baada ya kusema hayo, sasa niko tayari kwa uzinduzi wa kivuko hiki kipya cha Mv. Magogoni.



ASANTENI SANA KWA KUNISIKILIZA

Saturday, 30 May 2009

CCM still powerful - Research

Friday, May 29, 2009
CCM bado ina nguvu Tanzania-Tafiti

The Revolutionary State Party (CCM) is clearly the dominant political party in Tanzania, according to a poll by REPOA, Michigan State University, and Afrobarometer.
79 per cent of respondents would vote for the nominee of the CCM in the next presidential election.
The candidates representing the Civic United Front (CCW) and the Party for Democracy and Progress (CHADEMA) are far behind, with four per cent each.
Only one per cent of respondents would support the candidate of the National Convention for Construction and Reform (NCCR).
Tanzania held presidential and legislative elections in December 2005.
The CCM’s Jakaya Kikwete won the ballot with 80.2 per cent of the vote. His party also won most of multilateral level.
If a presidential election were held tomorrow, which party’s candidate would you vote for?Revolutionary State Party (CCM) 79%
Civic United Front (CUF) 4%
Party for Democracy and Progress (CHADEMA) 4%
National Convention for Construction and Reform (NCCR) 1%
Source: REPOA / Michigan State University / Afrobarometer Methodology:
Face-to-face interviews with 1,208 Tanzanian adults, conducted in June and July 2008. Margin of error is 2 per cent.

(Angus Reid Global Monitor) - kama nilivyochukua kutoka http://charaz.blogspot.com/


source: lukwangule.blogspot.com

Friday, 15 May 2009

Ikulu yampongeza Mhe. Anne Kilango MB

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425

PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mheshimiwa Anne Kilango (MB), Jimbo la Same Mashariki

YAH: KUTUNUKIWA TUZO YA KIMATAIFA YA WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA MAREKANI KWA WANAWAKE JASIRI (SECRETARY OF STATE’S GLOBAL AWARD FOR WOMEN OF COURAGE)

Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amepokea kwa furaha kubwa habari za kutunukiwa kwako Tuzo ya Mwanamke Jasiri kwa Mwaka 2009 inayotolewa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani. Aidha anakupongeza kwa mafanikio hayo makubwa na ya kujivunia.

Kutunukiwa kwako Tuzo hiyo ni ishara ya kutambuliwa na kuthaminiwa kwa mchango wako katika mapambano dhidi ya rushwa. Aidha, ukiwa Mbunge wa Chama Cha Mapinduzi, Tuzo hii ni tunda la wazi la utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya 2005 kuhusu vita dhidi ya rushwa ambayo Chama Cha Mapinduzi na Serikali yake vimetoa fursa pana zaidi kwa wananchi, wanahabari na viongozi wakiwemo Waheshimiwa Wabunge kushiriki kwa ukamilifu zaidi.
Hongera sana.

Ikulu
Dar es Salaam
27 March, 2009


chanzo: www.tanzania.go.tz

Friday, 24 April 2009

Reginald: call a spade a spade!!

IPP Limited Executive Chairman Reginald Mengi yesterday named five people he described as ``notoriously corrupt sharks``.

``I would like to conclude by saying that all corrupt people and especially those who are being accused of notorious corruption must be dealt with conclusively, otherwise they will rock the stability of our nation. We must realise that we have now reached the stage when we must say enough is enough.``


SOURCE: Guardian, 2009-04-24 12:52:23
By Patrick Kisembo

Thursday, 16 April 2009

Waziri Mkuu azungumzia kero za wananchi

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amesema shughuli za Kampuni ya DECI (Development Enterprenueurship Community Initiative) za wanachama kuweka fedha kupata faida marudufu ni sawa na upatu na ni kinyume cha sheria za nchi.

Akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo (Jumanne Apr. 14, 2009) alisema ndiyo maana Serikali imeunda timu ya kuingalia DECI na kuchukua hatua bila kuwaathiri wanachama wa DECI.

“Hakuna cha maono wala ufunuo, DECI ni upatu tu. DECI siyo mkombozi ni ujanja ujanja ambao ambao lazima utaleta matatizo hatimaye,” alisema.

Shughuli za upatu ni kinyume cha sheria Na. 8 ya mwaka 2006, iliyoidhinishwa na Rais Januari 5, mwaka 2007, kuwa ni kosa kuendesha shughuli za upatu ambao hauna usalama wa fedha watu wazochanga, aliongeza.

Alisema kuwa timu iliyoundwa na serikali kuangalia shughuli za DECI ina wataalamu kutoka Benki Kuu, Wakala wa Soko la Mitaji na Dhamana (Capital Markets Authority) na Idara ya Polisi.

DECI ilianza shughuli zake nchini mwaka 2007 na iliandikishwa kwa Wakala wa Usajili wa Makampuni (BRELA).

Waziri Mkuu alisema DECI ilianzishwa kama chama cha kuweka na kukopa, lakini baadaye ikawa inaendesha upatu na kwamba ina wanachama zaidi ya 430,000 na ina ofisi 46 katika mikoa 18 kati ya 26 nchini, kwa mujibu wa taarifa alizopata.

Benki ina akiba ya Sh. bilioni 1, lakini fedha ambazo zimezungushwa kupitia DECI ni Sh. bilioni 13 ambazo zilitolewa na kuchukuliwa na wanachama kama faida.

Kuhusu suala la ardhi katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, Waziri Mkuu alisema kuwa suala la ardhi linatawaliwa na sheria za kila nchi na siyo la ushirikiano katika jumuiya.

Alisema suala ardhi, kama vile la hoja ya mtu akiikaa katika nchi moja kwa mfululizo kwa miaka mitano apate uraia wa nchi hiyo, ni masuala ambayo hayawezi yakachukuliwa kwa pupa na Tanzania lazima iyaangalie kwa makini.

Kuhusu udahili wa wanafunzi wa vyuo vikuu vya umma ambavyo baadhi yao vilifungwa kwa muda kutokana na suala la uchangiaji, Waziri Mkuu alisema udahili umekwenda vizuri na kunavigezo vipya vya kujua uwezo wa mwanafunzo kucjangia kiasi gani.

Waziri Mkuu pia alisema Tanzania isisite kuhusu kuwaruhusu wakulima wakubwa binafsi kuwekeza katika kilimo cha kisasa cha kibiashara kwani bado kuna ardhi kubwa yenye rutuba lakini haijaguswa.

Alisema kinachotakiwa ni kuwa na Benki ya Ardhi ili muwekezaji akitaka kuwekeza katika kilimo anapewa ardhi ambayo kwa mfumo wa Tanzania ni ya Serikali na inatolewa kwa kukodishwa kwa masharti maalum
.

Kuhusu uvunjifu wa amani huko Tarime na maeneo mengine katika mkoa wa Mara, Waziri Mkuu alisema Serikali imepanga kuwa na mkoa wa kipolisi wilayani Tarime ili kuimarisha ulinzi.

Vilevile, inafaa kutenga eneo la amani la watu kuweza kukimbilia kama vile kuwa na kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) katika maeneo yenye magomvi.

Kuhusu maagizo ya Waziri Mkuu kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuangalia hesabu za Kituo cha Mabasi cha Ubungo na Soko la Kariakoo, Waziri Mkuu alisema kazi hiyo imekwishaanza na kwamba amepewa muda wa kutosha kuikamilisha.
(mwisho)

Imetolewa na:
Ofisi ya Waziri Mkuu
S.L.P. 3021
DAR ES SALAAM


source: lukwangule blog (Beda Msimbe)

Thursday, 2 April 2009

Hotuba ya Rais (March)

Alhamis, April 02, 2009

HOTUBA YA MHE. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, KWA WANANCHI, 31 MACHI, 2009

Ndugu wananchi,
Kwa mara nyingine tumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kupata nafasi ya kuzungumza na taifa katika utaratibu wetu wa kila mwezi.
Naomba radhi kuzungumza nanyi leo badala ya jana kwa sababu ya shughuli za ugeni wa Gavana-Jenerali wa Nchi rafiki ya Australia, Mama Quentin Bryce aliyetutembelea kuanzia tarehe 30 Machi na kuondoka leo asubuhi.
Leo napenda kuzungumzia mambo matatu. Jambo la kwanza ni mwenendo wa mvua na hali ya chakula nchini. Jambo la pili ni hali ya upatikanaji na uzalishaji umeme nchini. Na, la tatu ni mkutano wa Kundi la Nchi Ishirini Tajiri Duniani au maarufu kwa jina la G-20 kwa lugha ya Kiingereza. Mkutano unaoanza kesho mjini London, Uingereza.

Mwenendo wa Mvua
Ndugu Wananchi, Kwa kawaida hii ingekuwa wiki ya pili katika msimu wa mvua za masika kwa maeneo yanayopata mvua hizo. Mvua ambazo hunyesha kwa wingi na kwa saa nyingi mfululizo. Wakati mwingine hunyesha kwa siku mbili au hata tatu mfululizo. Lakini, ninyi na mimi ni mashahidi kuwa mpaka sasa mvua bado hazijaenea maeneo yote na unyeshaji wake siyo kama ule tuliouzoea.
Ingawaje ni mapema mno kuoneakana tuna mashaka, lakini hali ilivyo inatupa kila sababu ya kuwa na wasiwasi kuwa huenda mvua za masika zitanyesha chini ya wastani. Hata wenzetu wa Idara ya Utabiri wa hali ya Hewa wanaonyesha hofu kuwa huenda mvua za masika zisiwe nzuri kama tunavyotarajia.
Ndugu Wananchi;
Bahati mbaya sana Mikoa inayopata mvua za masika hivi sasa hazikupata mvua nzuri wakati wa msimu wa mvua za vuli mwaka wa jana. Kwa sababu hiyo kilimo katika mikoa hiyo kimeathirika, mavuno yamekuwa chini ya wastani na wako baadhi ya wakulima ambao hawakujaaliwa kupata chochote kabisa. Katika hali hiyo basi, kama katika msimu wa masika hali itakuwa chini ya wastani, ni dhahiri kwamba kutajitokeza tatizo kubwa kwa upande wa upatikanaji wa chakula na mapato ya wakulima kwa jumla.
Napenda kuwahakikishia kuwa Serikali inafuatilia kwa karibu hali hii na tumekuwa tunajiandaa kuchukua hatua zipasazo. Tathmini tuliyoifanya baada ya kumalizika kwa msimu wa mvua za vuli katika mikoa 9 ya Pwani, Dar es Salaam, Tanga, Kilimanjaro, Arusha, Manyara, Mara, Shinyanga na Kagera zinaonesha kuwa watu wapatao 279,607 katika wilaya 20 watakabiliwa na upungufu wa chakula katika kipindi cha miezi ya Aprili na Mei 2009. Mipango ya usambazaji wa chakula katika wilaya hizo zenye upungufu inaendelea vizuri.
Serikali inaendelea na itaendelea, kukusanya taarifa za hali ya chakula kutoka wilaya zote nchini na kuzifanyia uchambuzi na kutazama namna ya kuboresha hali ya upatikanaji wa chakula. Tutaendelea kutumia akiba yetu ya chakula kuwahudumia wananchi wenzetu watakaokabiliwa na upungufu wa chakula. Napenda kuwahakikishia Watanzania wote kwamba tutafanya kila tuwezalo kuhakikisha hakuna mtu atakayekufa kwa njaa. Aidha, napenda kuzihimiza Halmashauri za wilaya zote nchini kuendelea kutuma Wizara ya Kilimo na Chakula taarifa za hali ya mazao na chakula za wilaya zao kila wiki ili kuwezesha Serikali kujua hali ya chakula nchini. Nawataka Wakuu wa Wilaya kulisimamia ipasavyo zoezi hilo. Na, Wakuu wa Mikoa wahakikishe linafanyika.Wizara ya Kilimo na Chakula itafanya tathmini ya awali ya hali ya mavuno na chakula kuanzia mwezi ujao. Wanategemea kukamilisha ripoti hiyo mwezi Juni, 2009. Hii pia itaiwezesha Serikali kujipanga kukabiliana na hali ya chakula na mavuno itakayojitokeza.

Wito kwa Wananchi
Ndugu Wananchi;
Napenda kuchukua fursa hii kurudia kusisitiza mambo matano yafuatayo:-
Kwanza, kwamba kwa wenzetu wa mikoa ya Rukwa, Ruvuma, Iringa, Mtwara, Kigoma na Kagera ambako mvua imekuwa nzuri, tuitumie vizuri fursa hii kuhakikisha kuwa mavuno yamekuwa mazuri.
Pili, kwamba katika mikoa yenye matatizo ya upungufu wa mvua naomba wananchi watumie mvua zinazonyesha hivi sasa kupanda mbegu zinazokomaa kwa muda mfupi hasa wapande mazao yanayohimili ukame. Kwa ajili hii, tutilie maanani mazao ya viazi, muhogo, mtama na uwele. Hii itatusaidia kupunguza tatizo la uhaba wa chakula nchini iwapo litatokea.
Tatu, tutumie kwa tahadhari kubwa chakula tulichonacho nchini. Uhaba wa mvua ukiendelea, hali ya upatikanaji wa chakula nchini haitakuwa nzuri mwaka huu. Na ukizingatia kwamba hali ya chakula duniani kwa ujumla pia siyo nzuri ni muhimu wananchi wenzangu tukawa waangalifu katika kutumia chakula tulichonacho. Ni muhimu kufanya hivyo kwani inawezekana kabisa mtu ukawa na fedha za kununulia chakula nje ya nchi, lakini ukakosa chakula cha kununua.
Nne, kwa kuwa mazao ya nafaka ndiyo yatakayoathirika zaidi na mwenendo wa mvua, napenda kuchukua fursa hii kuwahimiza na kuwahamasisha watanzania wenzangu kwamba sasa tuongeze matumizi ya vyakula visivyo vya nafaka, kama vile, ndizi, muhogo na viazi.
Na, Tano, tuongeze bidii na tija kwenye uzalishaji wa mazao ya chakula ili tujitosheleze kwa chakula na kuuza akiba nje ya nchi. Tuzingatie kanuni za kilimo bora na tutumie pembejeo za kisasa.
Aidha, nawaomba tuendelee kuomba dua Mwenyezi Mungu atujalie mvua itakayonusuru mazao mashambani na kutuepusha na tatizo la upungufu wa chakula mwaka huu.
Hali ya Upatikanaji wa Umeme Nchini
Ndugu Wananchi,Kwa takriban miezi mwili sasa umeme umekuwa gumzo kubwa hapa nchini. Mjadala umekuwa wa namna mbili. Kwanza umehusu nia ya Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) kununua mitambo ya Kampuni ya Dowans pale Ubungo. Na, pili, umehusu mgao wa umeme unaoendelea tangu tarehe 26 Machi, 2009 mpaka sasa hasa hapa Dar es Salaam na wilaya jirani.
Mgao wa Umeme
Ndugu Wananchi,Kiini cha kuwepo kwa mgao wa umeme ni kuharibika kwa mitambo miwili ya kuzalisha MW 53 za umeme katika kituo cha kuzalisha umeme cha SONGAS. Jumamosi tarehe 28 Machi, 2009 mtambo mmoja wenye uwezo wa kuzalisha MW 20 ulitengemaa hivyo upungufu umebaki MW 33 kutoka kwenye mashine ya pili.
Taarifa niliyopewa leo ni kuwa hitilafu yake ni kubwa hivyo huenda ikachukua mpaka wiki mbili au tatu au zaidi kutengemaa. Maana yake ni kwamba mgao utaendelea kuwepo kwa kipindi hicho. Hivyo, Ndugu zangu, mgao huu hauna uhusiano na ile hadhari aliyoitoa Dkt. Idris Rashid, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO alipokuwa akizungumzia suala la Dowans kuwa nchi inaweza kuingia kwenye giza siku za usoni.
Ndugu Wananchi;
Kwa mujibu wa wataalamu wa TANESCO, mfumo wetu wa umeme nchini, kwa sasa, hauna ziada ya umeme unaosubiri kutumika kama akiba. Kutokana na hali hiyo, kunapotokea upungufu wowote wa uzalishaji wa umeme kwa sababu yoyote ile, kama huu uliotokea tarehe 26 Machi, 2009, husababisha kuwepo kwa mgao wa umeme kwa watumiaji.
Umeme wote unaozalishwa hapa nchini hutumika na wala mahitaji halisi hayajatoshelezwa. Kimsingi umeme unaopatikana na kutumika ni chini ya mahitaji (supressed demand). Ni asilimia 14 tu ya Watanzania ndiyo wanaopata na kutumia umeme wakati watu wengi sana wanaohitaji umeme bado hawajapata.
Ndugu Wananchi;
Wakati wote Serikali kwa kushirikiana na TANESCO imekuwa na mipango ya kuongeza uzalishaji na usambazaji wa umeme nchini. Kwa upande wa uzalishaji kumekuwepo hata na ratiba ya lini, kituo kipi na cha ukubwa gani kinaratajiwa kuwepo. Utekelezaji wa mipango hiyo ndiyo iliyotufikisha hapa tulipo sasa. Mwaka 2007, kufuatia matatizo makubwa ya umeme unaozalishwa kwa nguvu ya maji, mpango huo ukaboreshwa na kuongezwa ujenzi wa vituo vya kutumia gesi asilia na makaa ya mawe. Utekelezaji wa mpango wa uzalishaji wa umeme kwa mujibu wa uboreshaji uliofanywa mwaka 2007 uko nyuma ya wakati. Mradi wa kuzalisha umeme wa megawati 200 kwa kutumia makaa ya mawe Kiwira umechelewa kwa sababu ya ugumu wa kupata mikopo kutoka kwenye vyombo vya fedha. Kiini cha tatizo ni hofu inayotokana na taarifa hasi kuhusu mradi huo. Mradi wa kuzalisha megawati 300 kutokana na gesi asilimia ya Mnazi Bay unacheleweshwa na matatizo ya sasa ya kudorora kwa uchumi wa dunia ambapo nimeambiwa kwamba wabia muhimu wamejitoa kwa sasa.
Ndugu Wananchi,
Kuchelewa kutekelezwa kwa miradi hiyo ni dalili kuwa baada ya muda si mrefu hali ya upatikanaji wa umeme itakuwa mbaya hata kama mitambo yote ya sasa itakuwa inafanya kazi kwa ukamilifu. Kwa sasa mahitaji yanaongezeka kwa asilimia 10 – 15 kwa mwaka. Hili ni ongezeko kubwa sana ambalo linahitaji kusiwepo kukwama kokote. Kwa nia ya kutaka kupunguza makali ya tatizo hilo, ndipo uongozi wa TANESCO ukaona waombe kununua mitambo ya Dowans ambayo wakati huo ilikuwa inatangazwa kuuzwa. Uamuzi huo ukazua mtafaruku mkubwa ambao sina haja ya kuelezea kwa kirefu kwani wengi wetu tunaufahamu vizuri. Baada ya kuona ugumu wa kuendelea na nia hiyo, uongozi wa TANESCO umechukua uamuzi wa kuachana na nia yao hiyo.
Ndugu Wananchi;
Katika taarifa yake ya kutamka uamuzi wa kuachana na nia ya kununua mitambo ya Dowans, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO alielezea hofu yake kwamba uamuzi huo unaweza kusababisha nchi kuwa gizani hapo baadaye. Taarifa hiyo imeleta hofu kubwa katika jamii. Nataka kuwatoa hofu na kuwahakikishia Watanzania wenzangu wote kuwa Serikali itafanya kila iwezalo kuhakikisha kuwa nchi yetu haifikii hatua hiyo. Tutahakikisha kuwa nchi haiwi gizani na kwamba umeme wa ziada unaotakiwa utapatikana na shughuli za uzalishaji mali na utoaji huduma zitaendelea kama kawaida.
Ndugu Wananchi;
Tayari Wizara ya Nishati na Madini imeshaanza kuchukua hatua ambazo zinaonesha kuwa na mwelekeo wa kutia matumaini. Naamini tutafanikiwa. Tukiwa tayari, taarifa itatolewa. Penye nia pana njia.
Napenda kutumia nafasi hii kusema mambo mawili. Kwanza, kwamba, nawapongeza viongozi wa TANESCO kwa uamuzi wao wa busara wa kuachana na nia yao ya kununua mitambo ya Dowans. Wameyasoma vizuri mazingira na nyakati na kufanya uamuzi muafaka. Pili, niwaombe wanasiasa wenzangu kuwa, maadam waliokuwa na nia ya kununua mitambo hiyo hawanayo tena, suala hili limemalizika.
Sioni sababu ya kuendelea kulumbana, kutiana vidole machoni na kutoleana maneno makali na mengine hata hayastahili kusemwa. Tumekuwa tunawatia hofu wananchi kwa jambo lisilokuwepo tena. Nawaomba muzihifadhi nguvu zenu na bongo zenu ili muwafanyie wananchi mambo yenye tija kwao. Wanalo jukumu kubwa la kujiletea maendeleo kwa lengo la kujiondoa kwenye umaskini na kuwa na hali bora ya maisha yao.
Uongozi wetu wanasiasa unahitajika sana katika juhudi zao hizo. Tuelekeze nguvu zetu na maarifa yetu huko. Wapeni pumzi wananchi kutokana na malumbano haya.
Mkutano wa G-20
Ndugu Wananchi;
Jambo la mwisho ambalo ningependa kuliongelea leo hii ni kuhusu msukusuko wa uchumi wa dunia na hasa mkutano wa Kundi la Nchi Ishirini Tajiri Duniani (G-20) ambao unategemewa kufanyika kesho tarehe 2 Aprili na kumazika tarehe 3 Aprili, 2009 mjini London, Uingereza. Mkutano huu umeitishwa kutafuta njia za pamoja za kukabili kudorora kwa uchumi duniani.
Mataifa haya tajiri ishirini, ambayo yanamiliki asilimia 85 ya uchumi wa dunia ni pamoja na Marekani, Uingereza, China, Japan, Ujerumani, Ufaransa, Afrika ya Kusini, Australia, Uturuki, Brazil, Canada, Argentina, Mexico, Indonesia, India, Italy, Urusi, Korea Kusini, Umoja wa Nchi za Ulaya na Saudi Arabia.
Ndugu Wananchi;
Uchumi wa dunia sasa hivi unapita kwenye kipindi kigumu kuliko wakati wowote katika historia ya dunia. Hali hii isipodhibitiwa kwa haraka na kwa umakini itakuwa na athari kubwa ya kushusha viwango vya hali ya maisha ya watu katika nchi zote duniani tajiri na maskini. Matajiri watakuwa maskini na maskini watakuwa fukara zaidi.
Kama nilivyosema katika hotuba zangu zilizopita, kiini cha kudorora huku kwa uchumi wa dunia ni machafuko na kuanguka kwa mfumo wa fedha wa kimataifa. Tatizo lilianzia nchini Marekani na kuenea katika mataifa tajiri ya Ulaya na Asia. Mabenki makubwa na madogo yameanguka na kufilisika.
Viwanda vikubwa na vidogo pamoja makampuni makubwa na madogo yamefilisika na kufungwa. Mamilioni ya watu wamepoteza ajira na wanaendelea kupoteza ajira. Maelfu kwa maelfu ya watu wamepoteza nyumba zao za kuishi. Kwa ujumla, mamilioni ya watu katika mataifa tajiri wanaishi maisha ya mashaka. Wengi maisha yao yameanza kuporomoka.
Nchi zetu hazihusiki na kuzuka mwa matatizo haya lakini, athari za kudorora kwa uchumi wa dunia zinatukumba sote. Tayari tunashuhudia kupungua kwa bei na mahitaji ya bidhaa za nchi zetu kwenye soko la dunia, kupungua kwa idadi ya watalii na kupungua kwa uwekezaji na vitega uchumi kutoka nje.
Aidha, mapato ya fedha za kigeni na mapato ya Serikali nayo yanapungua. Mambo haya hatimaye yatasababisha kushuka kwa uchumi wa nchi zetu, watu kupoteza ajira na kipato na hali za maisha za watu katika nchi zetu kuporomoka. Kunahitajika hatua thabiti zichukuliwe na hatua hizo ziwahusishe na kunufaisha wadau wote. Nchi tajiri duniani zinao wajibu mkubwa zaidi. Kwanza, zina wajibu wa kuhakikisha kuwa wanadhibiti hali ili uchumi wa nchi zao usiendelee kudorora. Pia zinao wajibu wa kuzisaidia nchi kama zetu ziweze kukabiliana na athari za kudorora kwa uchumi wa dunia.
Nchi tajiri zimekuwa zinachukua hatua za kunusuru uchumi wa nchi zao na bado wanaendelea. Bahati mbaya nchi zetu maskini ambazo hazina uwezo wa kuwa na mipango kama hiyo, pamoja na ukweli kwamba nazo pia zinaihitaji sana, bado hazijasaidiwa.
Ndugu Wananchi;
Mkutano wa kesho wa Mataifa 20 Tajiri Duniani umeitishwa kujadili hatua zaidi za kuchukua kuzuia mambo yasiwe mabaya zaidi na kufanya uchumi ukue. Pia wanakusudia kuzungumzia njia za kuepuka maatizo kama haya yasitokee tena duniani. Katika mkutano wa kesho pia watazungumzia namna ya kuzisaidia nchi maskini za Afrika na zile zinazoendelea ziweze kujihami na kukabiliana na athari za matatizo ya uchumi wa dunia.
Katika mkutano wao wa kwanza, uliofanyika Washington, Marekani, jambo hili halikufanyika. Wakati ule nikiwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), nilimwandikia Rais George Bush wa Marekani, ambaye alikuwa Mwenyekiti wa mkutano ule, kumuomba wayaangalie maslahi ya Afrika, lakini hatukufanikiwa. Tulipata ahadi kuwa katika mkutano utakaofuata jambo hilo litazingatiwa. Tunamshukuru Waziri Mkuu wa Uingereza, Bw. Gordon Brown kwa kutimiza ahadi yake aliyonipatia kuhusu kujali maslahi ya Afrika pamoja na kutoa fursa ya ushiriki na sauti ya Afrika kuwepo katika mkutano huu wa pili. Kwa nia ya kupata maoni ya Waafrika hasa kuhusu matakwa na matarajio ya Afrika katika mkutano wa G-20, Waziri Mkuu wa Uingereza, tarehe 16 Machi, 2009 aliitisha mkutano maalum baina yake na viongozi kadhaa wa Afrika mjini London, Uingereza. Mkutano huo uliohusisha viongozi wa nchi za Tanzania, Liberia, Afrika Kusini, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Botswana, Misri, na Cape Verde ulikuwa na manufaa makubwa.
Ndugu Wananchi,
Nilitumia nafasi hiyo kuwasilisha maoni na mapendekezo ya mkutano wa pamoja wa Mawaziri wa Fedha, Magavana wa Benki Kuu za Afrika na Shirika la Fedha Duniani (IMF) uliofanyika hapa Dar es Salaam kuanzia tarehe 10 hadi 11 Machi, 2009. Mapendekezo hayo yalikuwa msingi wa mazungumzo yetu katika mkutano wetu na Bw. Gordon Brown.
Kwa muhtasari, matarajio ya Afrika katika mkutano wa G-20 ni kwa Afrika kusaidiwa kujikinga na kukabili madhara ya kudorora kwa uchumi wa dunia. Miongoni mwa mambo ambayo tuliyasisitiza ni haja ya kuanzishwa mfuko maalum ambapo fedha zake zitatumika kuzisaidia nchi za Afrika kuchukua hatua za kunusuru uchumi wao kama wafanyavyo mataifa tajiri.Kwa maneno mengine tuliunga mkono pendekezo la Benki ya Dunia na kutaka Mkutano wa G-20 ukubali kwamba asilimia 0.7 ya fedha walizotumia kugharamia mipango yao ya kuchochea uchumi wao (stimulus packages) zitengwe kwa ajili ya kusaidia kuchochea kukua kwa uchumi kwa nchi za Afrika.
Pili, tulisitiza kuwa nchi tajiri zisipunguze misaada ya maendeleo kwa nchi maskini. Badala yake misaada hiyo iongezwe kama walivyoahidi kwenye mikutano ya Monterrey, Gleneagles na kwingineko.
Tatu, tulisema kwamba tunatarajia pia misaada kwa Afrika, na uwekezaji kutoka nje vitaelekezwa katika kujenga na kuboresha miundombinu, kuleta mapinduzi katika kilimo, kukuza biashara miongoni mwa nchi za Kiafrika na baina yake na nchi nyingine za dunia na kusaidia zaidi makundi katika jamii ambayo yanahitaji msaada zaidi (vulnerable groups). Nne, kwamba nchi tajiri duniani pamoja na Taasisi za Kimataifa za Fedha Duniani zilegeze masharti na kupunguza urasimu wa kupata fedha za misaada na mikopo kwa kutambua kwamba hiki ni kipindi kugumu na cha dharura.
Aidha, masharti ya kukopa kutoka vyombo vingine vya fedha yalegezwe pia. Tano, kwamba nchi tajiri zisaidie nchi za Afrika kujenga mitaji ya vyombo vya fedha vya kikanda kama vile Benki ya Maendeleo ya Afrika.
Na, la sita, kwamba, nchi tajiri zitakubaliana kuruhusu uwazi katika mabenki yao na taasisi zao za fedha ili kuwezesha nchi za Kiafrika kufuatilia na kurudishiwa fedha, majumba na rasilimali zilizoporwa kutoka katika bara letu na kuhifadhiwa kisirisiri katika mabenki ya nchi tajiri.Ndugu Wananchi, Tunamshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu Gordon Brown kwa kuyapokea mapendekezo haya ya Afrika kwa moyo mkunjufu na kuahidi kuyafikisha na kusaidia kuyatetea katika kikao hicho. Pia tunamshukuru amepokea rai ya Afrika ya kuwakilishwa kwenye mkutano huo kwa kumwalika Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Meles Zenawi, ambaye atatuwakilisha kwa kofia yake ya Uenyekiti wa NEPAD.
Ndugu Wananchi;
Mkutano huu wa G-20 ni muhimu sana kwani unalo jukumu la kihistoria la kuuokoa uchumi wa dunia. Kwa msemo wa Kiswahili tungeweza kusema kuwa kazi ya mkutano huu ni ya kufa na kupona. Mkutano ukifanikiwa, sote tumenusurika. Ukishindwa sote tutakuwa mashakani na tunaweza kuangamia. Tuwatakie viongozi wa G-20 heri na fanaka tele katika mazungumzo yao. Hatima ya maisha na ustawi wa dunia na watu wake uko mikononi mwao.
Mwisho
Ndugu Wananchi;
Mwisho kabisa napenda kuelezea masikitiko yangu kwa ajali tatu zilizotokea hivi majuzi. Ya kwanza, ni ile ajali ya magari iliyotokea mkoani Mbeya. Ya pili, ni ile ya treni mbili zilizogongana mkoani Dodoma. Na ya tatu ni ajali ya mgodi kufukia wachimbaji, wilayani Geita. Kwa ajali zote hizo tatu, moyo wangu uko pamoja na familia za wafiwa na waliojeruhiwa. Majonzi yao ndio majonzi yangu. Na machungu yao ndio machungu yangu. Tuzidi kumuomba Mwenyezi Mungu aziweke roho za marehemu wetu hao mahali pema peponi. Amin!
Aidha, tunawaombea majeruhi waweze kupona haraka na kuendelea na juhudi zao za ujenzi wa Taifa.
Kuhusu ajali ya treni, tutachukua hatua za kisheria kwa wote waliosababisha ajali hiyo. Tayari wahusika, wakiwemo dereva wa treni ya mizigo, Mastesheni Masta na askari wawili waliokuwa kwenye treni ya mizigo wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma za uzembe na kusababisha mauaji.
Aidha, Serikali imeunda Tume ya kuchunguza chanzo cha ajali hiyo. Kwa upande wa ajali ya mgodi, napenda kuwahakikishia kuwa Serikali itafanya kila tuwezalo kusaidia juhudi za uokoaji. Ni kwa nia hiyo, nimeagiza Jeshi la Wananchi wa Tanzania kusaidia juhudi hizo, na Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. William Ngeleja, yupo Geita kwa ajili hiyo.
Naomba nimalize kwa kuwashukuru na kuwapongeza wananchi na viongozi wote walioshiriki, na wanaoendelea kushiriki, kwa hali na mali katika juhudi za uokoaji.
Mungu Ibariki Afrika
Mungu Ibariki Tanzania
Asanteni sana kwa kunisikiliza!



kutoka: lukwangule.blogspot.com

Tuesday, 17 March 2009

Commonwealth

The English noun commonwealth dates from the fifteenth century. The original phrase "common-wealth" or "the common weal" comes from the old meaning of "wealth," which is "well-being." The term literally meant "common well-being." Thus commonwealth originally meant a state or nation-state governed for the common good as opposed to an authoritarian state governed for the benefit of a given class of owners. Commonwealth derives from the Latin term res publica, a broad concept which is also sometimes translated as "public affairs" or "the state" in certain contexts. Res publica is also the term from which the English word republic arises.

Today the term is more general and means a political community.

The type of community indicated by the term commonwealth varies. For instance, in different contexts it might indicate:

a political unit founded in law by agreement of the people for the common good;
a federated union of constituent states;
a community of sovereign states;
a republic;
a democratic constitutional monarchy;
When capitalized, "Commonwealth" normally refers to the 53 member Commonwealth of Nations


(From Wikipedia, the free encyclopedia)

Monday, 9 February 2009

Mapinduzi ya kijeshi sio mazuri -Jakaya Kikwete

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

RAIS Jakaya Mrisho Kikwete jana, Jumanne, Februari 3, 2009, alizima jaribio la kubadilisha msimamo wa Umoja wa Afrika kuhusu mapinduzi ya kijeshi katika Afrika, akisisitiza kuwa kamwe hakuna mapinduzi yoyote ya kijeshi mazuri duniani.



Katika mchango wake uliokatishwa zaidi ya mara nne kwa makofi na mamia ya wajumbe waliofurika katika Ukumbi wa UNCC-ECA mjini Addis Ababa, Ethiopia, kuhudhuria Mkutano wa 12 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika (AU), Rais aliwaomba viongozi wenzake wa nchi za Afrika kuwa wakweli katika kujadili masuala muhimu ya maendeleo na ustawi wa Afrika.



Rais Kikwete aliungwa mkono katika hoja yake na baadhi ya viongozi waandamizi wa Afrika akiwamo Rais Idriss Deby wa Chad, Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda, na Waziri Mkuu wa Ethopia, Zenawi Meles na hivyo kukatisha mjadala huo.



Rais Kikwete aliingia kati kuzima jaribio hilo baada ya Mwenyekiti mpya wa AU, Kanali Muammar Gaddafi wa Libya, akiungwa mkono na Rais wa Senegal, Abdoulaye Wade kuwasilisha pendekezo kwenye mkutano huo wa kuzirejeshea tena uanachama nchi za Mauritania na Guinea, ambazo zimesimamishwa kwa sababu ya mapinduzi ya kijeshi.



Katika mchango wake, Rais Wade alisema kuwa mapinduzi hasa ya Guinea ni tofauti na mapinduzi mengine ya kijeshi, na kuwa utawala wa kijeshi wa nchi hiyo unaungwa mkono na wananchi.



Rais Wade alitoa uzoefu wake kuhusu utawala huo wa Guinea baada ya kuwa ametembelea nchi hiyo na kudai kuwa aliona jinsi wananchi wa nchi hiyo walivyozitokeza kwa wingi mitaani kumpokea na kuonyesha kuunga mkono utawala huo mpya.



Majeshi katika nchi hizo mbili yalitwaa madaraka katika Guinea na Mauritania mwaka uliopita wakati wa uenyekiti wa Rais Kikwete, ambaye mara moja aliamuru nchi hizo mbili kusimamisha uanachama wa AU kwa mujibu wa maamuzi ya viongozi wa nchi wanachama wa AU.



“Nawaombeni wenzangu tuwe wakweli katika kujadili mambo haya. Ni rahisi sana kwa jeshi kuwapanga watu mitaani na wakashangilia. Na hilo haliweza kuwa msingi wa kubadilisha uamuzi wa msingi kabisa wa Umoja huu,” alisema Rais Kikwete na kuongeza:



“Unaweza kufanya lolote ukiwa na bunduki, na niamini mimi kwa sababu nilipata kuwa jeshini. Chini ya utawala wa kijeshi, unaweza hata kuitisha kura ya maoni na kupata asilimia 99,9. Ndugu zangu hebu tuheshimu misingi mikuu ya Umoja wetu kama tulivyokubaliana.”



“Hakuna mapinduzi mazuri ya kijeshi, na lazima tukomeshe utamaduni wa mapinduzi ya kijeshi. Tusirudi nyuma katika miaka ile ya 1960 na 1970. Mtu anayetaka kuwa rais anatakiwa aingie katika siasa na kuomba ridhaa ya wananchi,” alisema, akisisitiza:



“Kama unataka kuwa Rais, unajiuzulu kutoka jeshini.. kama mimi nilivyofanya tena nikiwa na umri mdogo na sasa nimekuwa Rais. Isitoshe, hawa ni watu wanaosema kuwa watakuwa madaraka kwa muda mfupi…lakini angalia yule Lassana Conte wa Guinea aliahidi miaka miwili, akaishia akishikilia madaraka kwa miaka 24.”



Rais Kikwete, kwa hisia na ufasaha mkubwa alielezea historia ya mapinduzi katika Afrika, akitoa mifano ya karibuni zaidi ya mapinduzi katika nchi za Ivory Coast, Guinea, Madagascar na Mauritania. Mwishoni mwa mjadala hata Rais Gaddafi alibadilisha msimamo na kuunga mkono msimamo wa Rais Kikwete na wenzake.



Rais Kikwete aliungwa mkono mara moja na Rais Deby wa Chad ambaye aliwaambia viongozi wenzake: “Kama alivyosema Rais Kikwete, hakuna mapinduzi ya kijeshi mazuri. Tunapoteza muda tu kujadili jambo hilo ambalo tulikwishakulichukua uamuzi….tuache kuzungumzia suala hili, tunapoteza muda tu…”



Naye Rais Museveni alisema kuwa kazi ya jeshi ni kulinda amani ya nchi. “Sasa hawa badala ya kulinda amani ambao ndio wajibu wao wanajaribu kutawala nchi. Hakuna mapinduzi ya kijeshi mazuri na hayajawahi kutokea katika historia. Mapinduzi ya kijeshi ni jam bo lisilokuwa na maana. Ni jambo lisilokuwa na thamani.”



Alisisitiza: “Tokea mwaka 1963, tumekuwa na watu hawa wa kustajabisha…akina Idi Amin. Tutauua Umoja huu kwa mawazo na mijadala ya ovyo na ajabu kama hii. Tuyakatae mapinduzi katika Afrika…na kwenye hili tuko tayari kutofautiana. Hatuwezi kamwe kuzikubali Guinea na Mauritania kurudisha wanachama mpaka zitimize masharti.”



Museveni alisema kuwa yeye ana uzoefu wa kutosha wa kuendesha Serikali zote mbili, ya kijeshi na iliyoingia madarakani kwa kuchaguliwa na wananchi.



“Niamini mimi. Nimekuwa hata mpiganaji wa misituni (rebel). Lakini mchakato wa uchaguzi ni mzuri, unawalazimisha viongozi kufanya kazi. Lakini watu kama Gaddafi wanaukejeli…Ni muhimu kuwapo uchaguzi. Mimi nimeongoza serikali zote mbili, ya kijeshi na isiyokuwa ya kijeshi, najua ninachokisema,” alisisitiza Rais Museveni.



Naye Waziri Mkuu Meles alisema: “Pengine masuala haya ni muhimu lakini siyo ya lazima. Sisi ni viongozi tuache kushinda tunazunguka tu kuhusu hoja zisizokuwa na msingi na kuhusu suala ambalo tayari limeamuliwa. Tuwe na ajenda, vinginevyo tutakuwa sawa na wasusi wa nywele wa jadi katika Ethiopia, ambao kwa sababu wana muda tokea asubuhi hadi jioni, na kwa sababu hawana ajenda, huzungumzia jambo lolote linaloingia kichwani.”



“Hii ni mikutano ya kuzungumzia mambo muhimu na ya maana. Siyo nafasi ya kuja na kupiga picha kwa baadhi ya viongozi,” alisema Meles.

(source: www.tanzania.go.tz/pressrelease/Rais1.htm)