Watakaouza ardhi kwa wageni kushitakiwa
Serikali itawashitaki wananchi watakaouza ardhi kwa wageni sanjari na wataonunua, na itaichukua ardhi hiyo.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, John Chiligati amesema leo bungeni mjini Dodoma kuwa, kuuza ardhi kwa raia wa kigeni ni kuvunja sheria hivyo anayeuza na anayenunua wanatenda kosa.
Waziri Chiligati amewaeleza wabunge katika kikao cha nane, mkutano wa 16 wa Bunge kuwa, ardhi ni mali ya umma chini ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
“Sheria imesema, raia wa nje hawezi kumiliki ardhi hapa Tanzania isipokuwa mwekezaji” amesema Chiligati.
Amesema, kila Mtanzania ana haki ya kumiliki ardhi bila kubaguliwa, lakini wageni wanaoruhusiwa kufanya hivyo ni wawekezaji tu wenye vibali kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) na kwa kuzingatia Sheria ya Uwekezaji namba 26 ya mwaka 1997.
Chiligati amesema, Mtanzania anayeishi mjini ana haki ya kumilikishwa ardhi aitumie kwa miaka 33, 66 hadi 99, na kwamba vijijini haki ya kuitumi ardhi haina ukomo.
Wakati akijibu swali la Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai, Chiligati alisema, katika bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2009/2010 Serikali imetenga fedha za kupima mipaka ya vijiji vyote nchini ikiwa ni sehemu ya mchakato wa kuwamilisha wananchi ardhi.
Amesema, baada ya mashamba ya wananchi kupimwa, wao wataamua namna ya kuyatumia.
Wakati akijibu swali la Mbunge wa Bariadi Magharibi, John Cheyo, Chiligati alisema, maeneo yanayomilikiwa kimila mkoani Kilimanjaro maarufu kwa jina la vihamba pia yatapimwa ili yapate hati miliki.
Amesema, zitatolewa hati kwa kihamba kimoja kimoja, na kama kuna vihamba vingi vinavyomilikiwa na ukoo, itatolewa hati moja kwa vihamba hivyo na atakabidhiwa mkuu wa ukoo husika.
“Sheria zetu za ardhi haziruhusu wageni kumilikishwa ardhi”amesema Chiligati wakati akijibu swali la Mbunge wa Gando, Khalifa Suleiman Khalifa.
Kwa mujibu wa Waziri Chiligati, hadi sasa jumla ya wageni 20 wamemilikishwa jumla ya hekta 69,128 kwa ajili ya uwekezaji kwenye kilimo, Viwanda na hoteli.
Amesema, wageni 15 kati ya hao wamemilikishwa ardhi kati ya mwaka 2005 na mwaka jana, na kwamba Serikali imepata sh milioni 711.2 kupitia vyanzo mbalimbali vya taratibu za kuwamilikisha ikiwamokodi ya pango la ardhi na hati.
“Baada ya mwaka 2001 kama kuna mgeni ameuziwa ardhi chini ya utaratibu huu ni kinyume cha sheria” amesema Chiligati.
chanzo: habari-leo, Imeandikwa na Basil Msongo, Dodoma; Tarehe: 18th June 2009 @ 14:02
Showing posts with label Ardhi Makazi Nyumba. Show all posts
Showing posts with label Ardhi Makazi Nyumba. Show all posts
Thursday, 18 June 2009
Monday, 16 March 2009
Lawama: utoaji wa hatimiliki za viwanja TZ
Ufisadi watikisa Ardhi
Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi imetupiwa tuhuma nzito za ufisadi katika suala zima la utoaji wa hatimiliki za viwanja.
Tuhuma hizo zimetolewa na wananchi mbalimbali ambao wanadai kwa muda mrefu sasa wamekuwa wakihangaikia bila ya mafanikio kupata hati za miliki za viwanja vyao ambazo hutolewa na wizara hiyo.
Wizara hiyo inalaumiwa kuwa na urasimu mkubwa katika utoaji wa hati hizo kiasi cha kusababisha waombaji wakae muda mrefu bila ya kuzipata na wakati mwingine kulazimika kutoa rushwa kwa baadhi ya maafisa wake wasio waaminifu ili waweze kuzipata kirahisi.
Wakizungumza na Nipashe Jumapili kwa nyakati tofauti kuhusiana na suala hilo, baadhi ya wananchi wameilalamikia Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi, kuwa imekuwa ikiwazungusha kwa muda mrefu katika kuwapatia hati za viwanja vyao pamoja na kwamba wamekamilisha taratibu zote zinazotakiwa.
Wananchi hao wamelalamika kuwa kutokana na kucheleshwa kupata hati hizo kwa sababu zisizojulikana, wamekwama kufanya shughuli zao mbalimbali za maendeleo zinazohusiana na viwanja hivyo kama vile kuviendeleza au kutumia hati hizo kuomba mikopo benki kwa ajili ya kupambana na umasikini.
Mmoja wa wananchi hao kutoka mkoani Arusha ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alidai amekuwa akizungushwa kwa muda wa miezi mitano sasa kupata hati ya shamba lake, hali ambayo alidai imekwamisha mipango yake mingi ya kukiendeleza kiwanja hicho pamoja na kuitumia hati hiyo kuomba mkopo benki.
Alisema yeye ni mmoja wa watu waliohamasika na mpango wa serikali wa kuwapatia wananchi hati miliki za maeneo yao baada ya kuyapima ili waweze kuomba mikopo benki kwa ajili ya kupambana na umasikini, lakini Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi inamkatisha tamaa kutokana na utaratibu wake usioeleweka wa kutoa hati hizo.
``Serikali inatuhamasisha wananchi kupima maeneo yetu ili tupewe hati za umiliki zitakazotuwezesha kukopa benki, sasa tunashangazwa na wizara hii ambayo ndiyo yenye jukumu la kutoa hati hizo kutuzungusha kwa muda mrefu na wala hatujui tatizo ni nini maana hatujibiwi chochote,`` alisema.
Alifafanua kuwa yeye pamoja na wenzake wengine ambao nao wanakabiliwa na tatizo kama hilo, wametimiza taratibu zote za kupatiwa hati hizo kuanzia ngazi ya kijiji hadi kanda ambako ndiko hati hizo inakotolewa, lakini wameelezwa kuwa kanda haina mamlaka ya kuzitoa na kwamba zimetumwa wizarani Dar es Salaam ambako zimekwama huko wao wakisubiri kwa muda mrefu bila ya wao kujua kinachoendelea.
``Kwa utaratibu mtu anatakiwa kuanzia ngazi ya kijiji kwa kuitisha mkutano wa wanakijijiji wakikubali unaenda wilayani ambako unapewa kibali cha kupima ardhi kabla ya kwenda ngazi ya mkoa na kisha kanda ambako hati husajiliwa na kutiwa saini, mimi nimetimiza yote hayo lakini nilipoenda ofisi ya kanda nikaambiwa zimepelekwa wizarani ambako zimekwama,`` alieleza.
Nipashe Jumapili lilipowasilliana kwa njia ya simu na Kamishna wa Ardhi Kanda ya Kaskazini ili kujua ni tatizo gani linalosababisha kuchelewa kutolewa kwa hati hizo kufuatia malalamiko ya baadhi ya wananchi alikataa kutoa ushirikiano na badala yake ilitaka wizara ndiyo iulizwe kuhusiana na suala hilo.
Malalamiko kama hayo pia yametolewa na baadhi ya wananchi jijini Dar es Salaam na kutoka mikoa mingine, kuwa inawachukuwa muda mrefu sana kupata hati za umiliki wa maeneo yao huku wakiwa hawajui tatizo ni nini pamoja na kufuata taratibu zote zinazotakiwa.
Wananchi hao wamemuomba Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, John Chiligati, kulifuatilia kwa karibu tatizo hilo ili kulipatia ufumbuzi wa haraka, kwa kile walichodai kuwa baadhi ya maafisa wa wizara hiyo siyo waaminifu kwani wamekuwa wakifanya makusudi kuchelewesha kutoa hati ili waweze kupewa rushwa.
Walisema wizara hiyo inatakiwa kwenda sambamba na kauli mbiu ya Rais Jakaya Kikwete ya Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi mpya katika utendaji wake ikiwa ni pamoja na kuwaondoa watumishi wote wanaokwenda kinyume na maadili ya kazi zao ili kuleta ufanisi.
Nipashe Jumapili lilipowasiliana na Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, John Chiligati, kuhusiana na malalamiko hayo ya wananchi alionekana kushangazwa na maelezo hayo, akieleza kuwa kwa sasa hakuna tatizo kama hilo la ucheleweshaji wa utoaji wa hati za umiliki wa ardhi.
Alieleza kuwa tatizo hilo lilikuwapo zamani lakini wizara yake imeshalifanyia kazi na kwamba kwa sasa halipo tena, tofauti na madai ya wananchi hao.
Chiligati, alifafanua kuwa kutokana na tatizo hilo kuwa sugu siku za nyuma, wizara yake ilianzisha utaratibu wa maombi ya hati za umiliki wa ardhi kushughulikiwa katika kanda badala ya wizarani, ili kuwawezesha wananchi kuzipata bila ya usumbufu na kwa haraka.
``Tatizo hilo limekuwa historia, tangu tupate uhuru maombi yote yalikuwa yanashughulikiwa wizarani tu na Kamishana wa Ardhi, lakini sasa tumeunda kanda tano kwa ajili ya kurahisisha mambo, mimi ndiyo muasisi wa utaratibu huu, wananchi wanatakiwa kupeleka maombi yao huko kwa ajili ya kupatiwa hati za umiliki wa ardhi badala ya kuja moja kwa moja wizarani kama zamani,`` alifafanua.
Alizitaka kanda hizo kuwa ni Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Ziwa, Kanda ya Kusini, Kanda ya Kati na Kanda ya Mashariki.
Alitoa wito kwa mwananchi yoyote anayezungushwa kupata hati hizo baada ya kukamilisha taratibu zote aende wizarani akaonane naye ili aweze kushughulikia tatizo hilo.
Kwa muda mrefu sasa kumekuwa na malalamiko mengi kutoka wananchi wakiilalamikia baadhi ya maofisa wa Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi kuwa wamekuwa kikwazo katika utoaji wa hati za umiliki wa ardhi kwa lengo la kupewa rushwa, hali ambayo inakwamisha mipango yao ya kuboresha hali zao za maisha.
SOURCE: Nipashe, 2009-03-15 14:08:05
Na Abdallah Bawazir
Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi imetupiwa tuhuma nzito za ufisadi katika suala zima la utoaji wa hatimiliki za viwanja.
Tuhuma hizo zimetolewa na wananchi mbalimbali ambao wanadai kwa muda mrefu sasa wamekuwa wakihangaikia bila ya mafanikio kupata hati za miliki za viwanja vyao ambazo hutolewa na wizara hiyo.
Wizara hiyo inalaumiwa kuwa na urasimu mkubwa katika utoaji wa hati hizo kiasi cha kusababisha waombaji wakae muda mrefu bila ya kuzipata na wakati mwingine kulazimika kutoa rushwa kwa baadhi ya maafisa wake wasio waaminifu ili waweze kuzipata kirahisi.
Wakizungumza na Nipashe Jumapili kwa nyakati tofauti kuhusiana na suala hilo, baadhi ya wananchi wameilalamikia Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi, kuwa imekuwa ikiwazungusha kwa muda mrefu katika kuwapatia hati za viwanja vyao pamoja na kwamba wamekamilisha taratibu zote zinazotakiwa.
Wananchi hao wamelalamika kuwa kutokana na kucheleshwa kupata hati hizo kwa sababu zisizojulikana, wamekwama kufanya shughuli zao mbalimbali za maendeleo zinazohusiana na viwanja hivyo kama vile kuviendeleza au kutumia hati hizo kuomba mikopo benki kwa ajili ya kupambana na umasikini.
Mmoja wa wananchi hao kutoka mkoani Arusha ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alidai amekuwa akizungushwa kwa muda wa miezi mitano sasa kupata hati ya shamba lake, hali ambayo alidai imekwamisha mipango yake mingi ya kukiendeleza kiwanja hicho pamoja na kuitumia hati hiyo kuomba mkopo benki.
Alisema yeye ni mmoja wa watu waliohamasika na mpango wa serikali wa kuwapatia wananchi hati miliki za maeneo yao baada ya kuyapima ili waweze kuomba mikopo benki kwa ajili ya kupambana na umasikini, lakini Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi inamkatisha tamaa kutokana na utaratibu wake usioeleweka wa kutoa hati hizo.
``Serikali inatuhamasisha wananchi kupima maeneo yetu ili tupewe hati za umiliki zitakazotuwezesha kukopa benki, sasa tunashangazwa na wizara hii ambayo ndiyo yenye jukumu la kutoa hati hizo kutuzungusha kwa muda mrefu na wala hatujui tatizo ni nini maana hatujibiwi chochote,`` alisema.
Alifafanua kuwa yeye pamoja na wenzake wengine ambao nao wanakabiliwa na tatizo kama hilo, wametimiza taratibu zote za kupatiwa hati hizo kuanzia ngazi ya kijiji hadi kanda ambako ndiko hati hizo inakotolewa, lakini wameelezwa kuwa kanda haina mamlaka ya kuzitoa na kwamba zimetumwa wizarani Dar es Salaam ambako zimekwama huko wao wakisubiri kwa muda mrefu bila ya wao kujua kinachoendelea.
``Kwa utaratibu mtu anatakiwa kuanzia ngazi ya kijiji kwa kuitisha mkutano wa wanakijijiji wakikubali unaenda wilayani ambako unapewa kibali cha kupima ardhi kabla ya kwenda ngazi ya mkoa na kisha kanda ambako hati husajiliwa na kutiwa saini, mimi nimetimiza yote hayo lakini nilipoenda ofisi ya kanda nikaambiwa zimepelekwa wizarani ambako zimekwama,`` alieleza.
Nipashe Jumapili lilipowasilliana kwa njia ya simu na Kamishna wa Ardhi Kanda ya Kaskazini ili kujua ni tatizo gani linalosababisha kuchelewa kutolewa kwa hati hizo kufuatia malalamiko ya baadhi ya wananchi alikataa kutoa ushirikiano na badala yake ilitaka wizara ndiyo iulizwe kuhusiana na suala hilo.
Malalamiko kama hayo pia yametolewa na baadhi ya wananchi jijini Dar es Salaam na kutoka mikoa mingine, kuwa inawachukuwa muda mrefu sana kupata hati za umiliki wa maeneo yao huku wakiwa hawajui tatizo ni nini pamoja na kufuata taratibu zote zinazotakiwa.
Wananchi hao wamemuomba Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, John Chiligati, kulifuatilia kwa karibu tatizo hilo ili kulipatia ufumbuzi wa haraka, kwa kile walichodai kuwa baadhi ya maafisa wa wizara hiyo siyo waaminifu kwani wamekuwa wakifanya makusudi kuchelewesha kutoa hati ili waweze kupewa rushwa.
Walisema wizara hiyo inatakiwa kwenda sambamba na kauli mbiu ya Rais Jakaya Kikwete ya Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi mpya katika utendaji wake ikiwa ni pamoja na kuwaondoa watumishi wote wanaokwenda kinyume na maadili ya kazi zao ili kuleta ufanisi.
Nipashe Jumapili lilipowasiliana na Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, John Chiligati, kuhusiana na malalamiko hayo ya wananchi alionekana kushangazwa na maelezo hayo, akieleza kuwa kwa sasa hakuna tatizo kama hilo la ucheleweshaji wa utoaji wa hati za umiliki wa ardhi.
Alieleza kuwa tatizo hilo lilikuwapo zamani lakini wizara yake imeshalifanyia kazi na kwamba kwa sasa halipo tena, tofauti na madai ya wananchi hao.
Chiligati, alifafanua kuwa kutokana na tatizo hilo kuwa sugu siku za nyuma, wizara yake ilianzisha utaratibu wa maombi ya hati za umiliki wa ardhi kushughulikiwa katika kanda badala ya wizarani, ili kuwawezesha wananchi kuzipata bila ya usumbufu na kwa haraka.
``Tatizo hilo limekuwa historia, tangu tupate uhuru maombi yote yalikuwa yanashughulikiwa wizarani tu na Kamishana wa Ardhi, lakini sasa tumeunda kanda tano kwa ajili ya kurahisisha mambo, mimi ndiyo muasisi wa utaratibu huu, wananchi wanatakiwa kupeleka maombi yao huko kwa ajili ya kupatiwa hati za umiliki wa ardhi badala ya kuja moja kwa moja wizarani kama zamani,`` alifafanua.
Alizitaka kanda hizo kuwa ni Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Ziwa, Kanda ya Kusini, Kanda ya Kati na Kanda ya Mashariki.
Alitoa wito kwa mwananchi yoyote anayezungushwa kupata hati hizo baada ya kukamilisha taratibu zote aende wizarani akaonane naye ili aweze kushughulikia tatizo hilo.
Kwa muda mrefu sasa kumekuwa na malalamiko mengi kutoka wananchi wakiilalamikia baadhi ya maofisa wa Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi kuwa wamekuwa kikwazo katika utoaji wa hati za umiliki wa ardhi kwa lengo la kupewa rushwa, hali ambayo inakwamisha mipango yao ya kuboresha hali zao za maisha.
SOURCE: Nipashe, 2009-03-15 14:08:05
Na Abdallah Bawazir
Tuesday, 3 March 2009
Upimaji Ardhi TZ
Wananchi waanza kupimiwa ardhi
Serikali imeanza kuchukua hatua ya kurasimisha ardhi na nyumba za wakulima na wafugaji ili kuwawezesha kupata mikopo benki, mifuko na taasisi za fedha nchini ili kuwaondoa katika umaskini uliokithiri.
Kauli hiyo ilitolewa juzi na Waziri wa ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, John Chiligati wakati akizindua upimaji na utoaji wa hati miliki za ardhi kimila uliofanyika Wilaya ya Bariadi mkoani Shinyanga.
Wilaya hiyo ni moja ya maeneo ya majaribio kitaifa. Nyingine ni ya Babati mkoani Arusha pia.
Uzinduzi huo wa mpango umefanyika baada ya viongozi wa serikali na vyama vya kisiasa na wataalamu kupewa mafunzo elekezi wilayani humo ya kuchambua chimbuko la mradi huo katika utekelezaji wa sera ya Taifa ya Ardhi ya mwaka 1995 na Sheria ya Ardhi ya Vijiji namba 5 ya mwaka 2004.
Chiligati alisema hatua hiyo ni ya utekelezaji wa Mkakati wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara Tanzania (Mkurabita) kwa lengo la kuwawezesha Watanzania kurasimisha ardhi na nyumba zao ili waweze kuzitumia kupata mikopo kwa urahisi.
Alisema mpango huo ambao ni wa kwanza kutekelezwa nchini utawawezesha wakulima na wafugaji kumiliki ardhi zao za kimila kwa kuhusisha serikali za vijiji na kupanga matumizi bora ya ardhi.
Alisema maeneo muhimu ambayo yatazingatiwa wakati wa upimaji huo ni ya makazi, huduma za kijamii, makaburi na maeneo ya hifadhi ya ardhi ya kijiji kama vile maeneo ya malisho.
Alisema baada ya kutambua kila kipande cha ardhi ndani ya kijiji chini ya mpango huo, ndipo utekelezaji utafanyika kwa kutambua mipaka ya kila mwenye shamba au eneo la malisho ya mifugo na kuweka mipaka bayana.
Pamoja na kuweka kumbukumbu za miliki ya ardhi bayana, alisema mpango huo pia utammilikisha na kumpatia kila mhusika hatimiliki ya eneo lake, wakati kipande cha ardhi kwa mtu mmoja mmoja au familia ya mume na mke au eneo linalomilikiwa kiukoo itamilikishwa kwa kupitia kiongozi wa familia au ukoo.
Chiligati aliagiza kuwapo kwa ushirikishwaji wa kila mwanakijiji na kuutaja mradi huo kuwa ni shirikishi.
SOURCE: Nipashe, 2009-03-03 10:55:06
Na Stephen Wang`anyi, Shinyanga
Serikali imeanza kuchukua hatua ya kurasimisha ardhi na nyumba za wakulima na wafugaji ili kuwawezesha kupata mikopo benki, mifuko na taasisi za fedha nchini ili kuwaondoa katika umaskini uliokithiri.
Kauli hiyo ilitolewa juzi na Waziri wa ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, John Chiligati wakati akizindua upimaji na utoaji wa hati miliki za ardhi kimila uliofanyika Wilaya ya Bariadi mkoani Shinyanga.
Wilaya hiyo ni moja ya maeneo ya majaribio kitaifa. Nyingine ni ya Babati mkoani Arusha pia.
Uzinduzi huo wa mpango umefanyika baada ya viongozi wa serikali na vyama vya kisiasa na wataalamu kupewa mafunzo elekezi wilayani humo ya kuchambua chimbuko la mradi huo katika utekelezaji wa sera ya Taifa ya Ardhi ya mwaka 1995 na Sheria ya Ardhi ya Vijiji namba 5 ya mwaka 2004.
Chiligati alisema hatua hiyo ni ya utekelezaji wa Mkakati wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara Tanzania (Mkurabita) kwa lengo la kuwawezesha Watanzania kurasimisha ardhi na nyumba zao ili waweze kuzitumia kupata mikopo kwa urahisi.
Alisema mpango huo ambao ni wa kwanza kutekelezwa nchini utawawezesha wakulima na wafugaji kumiliki ardhi zao za kimila kwa kuhusisha serikali za vijiji na kupanga matumizi bora ya ardhi.
Alisema maeneo muhimu ambayo yatazingatiwa wakati wa upimaji huo ni ya makazi, huduma za kijamii, makaburi na maeneo ya hifadhi ya ardhi ya kijiji kama vile maeneo ya malisho.
Alisema baada ya kutambua kila kipande cha ardhi ndani ya kijiji chini ya mpango huo, ndipo utekelezaji utafanyika kwa kutambua mipaka ya kila mwenye shamba au eneo la malisho ya mifugo na kuweka mipaka bayana.
Pamoja na kuweka kumbukumbu za miliki ya ardhi bayana, alisema mpango huo pia utammilikisha na kumpatia kila mhusika hatimiliki ya eneo lake, wakati kipande cha ardhi kwa mtu mmoja mmoja au familia ya mume na mke au eneo linalomilikiwa kiukoo itamilikishwa kwa kupitia kiongozi wa familia au ukoo.
Chiligati aliagiza kuwapo kwa ushirikishwaji wa kila mwanakijiji na kuutaja mradi huo kuwa ni shirikishi.
SOURCE: Nipashe, 2009-03-03 10:55:06
Na Stephen Wang`anyi, Shinyanga
Subscribe to:
Posts (Atom)