Thursday 18 June 2009

'Kila Mtanzania ana haki ya kumiliki ardhi'

Watakaouza ardhi kwa wageni kushitakiwa

Serikali itawashitaki wananchi watakaouza ardhi kwa wageni sanjari na wataonunua, na itaichukua ardhi hiyo.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, John Chiligati amesema leo bungeni mjini Dodoma kuwa, kuuza ardhi kwa raia wa kigeni ni kuvunja sheria hivyo anayeuza na anayenunua wanatenda kosa.

Waziri Chiligati amewaeleza wabunge katika kikao cha nane, mkutano wa 16 wa Bunge kuwa, ardhi ni mali ya umma chini ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Sheria imesema, raia wa nje hawezi kumiliki ardhi hapa Tanzania isipokuwa mwekezaji” amesema Chiligati.

Amesema, kila Mtanzania ana haki ya kumiliki ardhi bila kubaguliwa, lakini wageni wanaoruhusiwa kufanya hivyo ni wawekezaji tu wenye vibali kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) na kwa kuzingatia Sheria ya Uwekezaji namba 26 ya mwaka 1997.

Chiligati amesema, Mtanzania anayeishi mjini ana haki ya kumilikishwa ardhi aitumie kwa miaka 33, 66 hadi 99, na kwamba vijijini haki ya kuitumi ardhi haina ukomo.

Wakati akijibu swali la Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai, Chiligati alisema, katika bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2009/2010 Serikali imetenga fedha za kupima mipaka ya vijiji vyote nchini ikiwa ni sehemu ya mchakato wa kuwamilisha wananchi ardhi.

Amesema, baada ya mashamba ya wananchi kupimwa, wao wataamua namna ya kuyatumia.

Wakati akijibu swali la Mbunge wa Bariadi Magharibi, John Cheyo, Chiligati alisema, maeneo yanayomilikiwa kimila mkoani Kilimanjaro maarufu kwa jina la vihamba pia yatapimwa ili yapate hati miliki.

Amesema, zitatolewa hati kwa kihamba kimoja kimoja, na kama kuna vihamba vingi vinavyomilikiwa na ukoo, itatolewa hati moja kwa vihamba hivyo na atakabidhiwa mkuu wa ukoo husika.

“Sheria zetu za ardhi haziruhusu wageni kumilikishwa ardhi”amesema Chiligati wakati akijibu swali la Mbunge wa Gando, Khalifa Suleiman Khalifa.

Kwa mujibu wa Waziri Chiligati, hadi sasa jumla ya wageni 20 wamemilikishwa jumla ya hekta 69,128 kwa ajili ya uwekezaji kwenye kilimo, Viwanda na hoteli.

Amesema, wageni 15 kati ya hao wamemilikishwa ardhi kati ya mwaka 2005 na mwaka jana, na kwamba Serikali imepata sh milioni 711.2 kupitia vyanzo mbalimbali vya taratibu za kuwamilikisha ikiwamokodi ya pango la ardhi na hati.

“Baada ya mwaka 2001 kama kuna mgeni ameuziwa ardhi chini ya utaratibu huu ni kinyume cha sheria” amesema Chiligati.



chanzo: habari-leo, Imeandikwa na Basil Msongo, Dodoma; Tarehe: 18th June 2009 @ 14:02

Wembley Stadium

Wembley Stadium (usually shortened to just Wembley) is located in the Borough of Brent in North West London, England. Primarily a football venue, Wembley is owned by The Football Association (The FA) via its subsidiary Wembley National Stadium Limited, and hosts England's home international football matches and the main English domestic cup finals. The Stadium is also used for music concerts and other sporting events. Wembley will host the 2011 UEFA Champions League Final.

The most expensive stadium ever built, Wembley's 90,000 capacity makes it the second largest stadium in Europe, and is the largest in the world with every seat under cover. Immediately following its opening, it was often referred to as the "new Wembley Stadium" to distinguish it from the original stadium.

The previous Wembley Stadium (originally known as the British Empire Exhibition Stadium or Empire Stadium) was one of the world's most famous football stadiums, being England's national stadium for football, and because of the geographical origins of the game was often referred to as "The Home of Football". It hosted the European Cup (now the UEFA Champions League) final a record five times, and is one of seventeen stadiums to have held a FIFA World Cup final. Though the original structure was closed in 1999, it was not demolished until 2003, after which construction began on the new stadium, originally intended to open in 2006. This was later delayed until early 2007. The final completion date of the stadium was 9 March 2007, when the keys to the stadium were handed over to the FA.

Building
Wembley was designed by architects Populous (formerly HOK Sport) and Foster and Partners with engineers Mott MacDonald, built by Australian company Brookfield Multiplex and funded by Sport England, WNSL (Wembley National Stadium Limited), the Football Association, the Department for Culture Media and Sport and the London Development Agency. It is the most expensive stadium ever built at a cost of £798 million (roughly US$1.57 billion) and has the largest roof-covered seating capacity in the world.


Construction of the new Wembley, looking east, taken January 2006The all-seater stadium is based around a bowl design with a capacity of 90,000, protected from the elements by a sliding roof that does not completely enclose it. It can also be adapted as an athletic stadium by erecting a temporary platform over the lowest tier of seating[citation needed]. The stadium's signature feature is a circular section lattice arch of 7 m (23 ft) internal diameter with a 315 m (1,033 ft) span, erected some 22° off true, and rising to 140 m (459 ft) tall. It supports all the weight of the north roof and 60% of the weight of the retractable roof on the southern side. The archway is the world's longest unsupported roof structure. Instead of the 39 steps climbed, in the original stadium, to enter the Royal Box and collect a trophy, there are now 107.

A "platform system" has been designed to convert the stadium for athletics use, but its use would decrease the stadium's capacity to approximately 60,000. No athletics events have taken place at the stadium, and none are scheduled.

The stadium is linked to Wembley Park Station on the London Underground via Olympic Way, and Wembley Central via the White Horse Bridge. It also has a rail link—provided by the Wembley Stadium railway station—to London Marylebone and Birmingham.

The initial plan for the reconstruction of Wembley was for demolition to begin before Christmas 2000, and for the new stadium to be completed some time during 2003, but this work was delayed by a succession of financial and legal difficulties. It was scheduled to open on 13 May 2006, with the first game being that year's FA Cup Final. However, worries were expressed as to whether the stadium would actually be completed on time.[8] The new stadium was completed and handed over to the FA on 9 March 2007, with the total cost of the project (including local transport infrastructure redevelopment and the cost of financing) estimated to be £1 billion (roughly US$1.97 billion).


The stadium in its very early stages of construction, circa August 2003
New Wembley Stadium looking south, down the new Wembley Way, January 2007In October 2005, Sports Minister Richard Caborn announced: "They say the Cup Final will be there, barring six feet of snow or something like that". However in December 2005, the builders admitted that there was a "material risk" that the stadium might not be ready in time for the Cup Final[9] and in February 2006, these worries were confirmed by the FA moving the game to Cardiff's Millennium Stadium.

The delays started as far back as 2003. In December 2003, the constructors of the arch, subcontractors Cleveland Bridge, warned Multiplex about rising costs and a delay on the steel job of almost a year due to design changes which Multiplex rejected. Cleveland Bridge were removed from the project and replaced by Dutch firm Hollandia with all the attendant problems of starting over. On 20 March 2006, a steel rafter in the roof of the new development fell by a foot and a half, forcing 3,000 workers to evacuate the stadium and raising further doubts over the completion date which was already behind schedule. On 23 March 2006, sewers beneath the stadium buckled due to ground movement. GMB Union leader Steve Kelly said that the problem had been caused by the pipes not being properly laid, and that the repair would take months. A spokesman for developers Multiplex said that they did not believe this would "have any impact on the completion of the stadium", which was then scheduled to be completed on 31 March 2006.

On 30 March 2006, the developers announced that Wembley Stadium would not be ready until 2007. All competitions and concerts planned were to be moved to suitable locations. On 19 June 2006 it was announced that the turf had been laid. On 19 October 2006 it was announced that the venue was now set to open in early 2007 after the dispute between The Football Association and Multiplex had finally been settled. WNSL, a subsidiary of The Football Association, is expected to pay around £36m to Multiplex, as well as the amount of the original fixed-price contract. This meant that the Wembley Stadium was ready for the 2007 FA Cup Final on 19 May 2007. The official Wembley Stadium website announced that the stadium would be open for public viewing for local residents of Brent on 3 March 2007, however the event was delayed by two weeks and instead happened on 17 March. The keys to the new Wembley stadium were finally handed over to the owners on 9 March 2007 ready to be open and used for upcoming FA Cup football matches, concerts and other events.

A short documentary of its redevelopment can be found on the Queen Live at Wembley '86 DVD. The reconstruction of the stadium is part of the wider regeneration of Wembley.

Although not completed or opened at the time, EA Sports added Wembley Stadium into the video game FIFA 07.

A statue of Bobby Moore—the captain of the England national football team when they won the 1966 Football World Cup at Wembley—was unveiled outside the stadium on Friday 11 May 2007.


Structure

Inside the stadiumThe new Wembley is the largest stadium in the world with every seat under cover.
The stadium contains 2,618 toilets, more than any other venue in the world.
The stadium has a circumference of 1 km (0.6 mi).
At its peak, there were more than 3,500 construction workers on site.
4,000 separate piles form the foundations of the new stadium, the deepest of which is 35 m (115 ft).
There are 56 km (35 miles) of heavy-duty power cables in the stadium.
90,000 m³ (120,000 cu yds) of concrete and 23,000 tonnes (25,000 short tons) of steel were used in the construction of the new stadium.
The total length of the escalators is 400 m (¼ mi).
The Wembley Arch has a diameter greater than that of a cross-channel Eurostar train.

Pitch

Inside the stadium, in the daytimeThe new pitch is 13 ft (4.0 m) lower than the previous pitch. The pitch size is 115 yards (105 m) long by 75 yards (69 m) wide, slightly narrower than the old Wembley Since the completion of the new Wembley, the pitch has come into major disrepute when it was commented on being "no good" and "not in the condition that Wembley used to be known for" by Slaven Bilić before the game between England and the team he managed, Croatia. It was confirmed when the pitch was terribly cut up during the game, which was blamed by some as the reason England did not qualify for UEFA Euro 2008 despite previous results also being blamed by others. The Football Association admitted in April 2009 after the FA Cup semi-finals that improvements are needed to the Wembley pitch after criticism of the surface by Sir Alex Ferguson, Arsene Wenger and David Moyes. The grass has been re-laid five times since the stadium re-opened in 2007 and will be re-laid again in the summer of 2009, ahead of the 2009 Community Shield.


Roof

Detail of the archThe new 6,350 tonne roof covers an area of over 45,000 square metres (11 acres), 4 acres (16,000 m2) of which are movable and rise to 52 m (170 ft) above the pitch. With a span of 317 m (1040 ft), the arch is the longest single span roof structure in the world and is 134 m (440 ft) above the level of the external concourse, and is designed not to cast a shadow on the pitch. Contrary to popular belief, the stadium's roof is not fully retractable, meaning it cannot cover the playing surface in inclement weather.


Tenants
The English national football team is a major user of Wembley Stadium. Given the ownership by The Football Association as of 10 March 2007, the League Cup final moved back to Wembley from Cardiff following the FA Cup final and FA Community Shield. Other showpiece football matches that were previously staged at Wembley, such as the Football League promotion play-offs and the Football League Trophy final, have returned to the stadium, as has the Football Conference play-off final. Additionally, the Rugby League Challenge Cup final returned to Wembley Stadium in 2007. The new Wembley is a significant part of the plan for the 2012 Summer Olympics in London; the stadium will be the site of several games in both the men's and women's football tournaments, with the finals planned to be held there.

The Race of Champions staged their 2007 and 2008 events at the stadium. Should the NFL grant a European franchise, London and Wembley are the preferred location and venue.


Music

The stage at the Live Earth concert held at Wembley on 7 July 2007.Besides football, Wembley can be configured to hold many other events, particularly major concerts. The first concert at the new stadium was given by George Michael on 9 June 2007. Other acts to have performed at the stadium are Westlife, Muse who were the first artists to sell out Wembley, Metallica, Foo Fighters and Madonna. Coldplay, AC/DC, U2 and Oasis are due to perform in 2009.

Two large charity concerts have been held at the new Wembley stadium, the Concert for Diana, a memorial concert ten years after the Death of Diana, Princess of Wales, and Live Earth. Bon Jovi were scheduled to be the first artists to perform at the new Wembley but the late completion of the stadium saw the concerts relocated to the National Bowl and the KC Stadium.


Past concerts
Date Artist
9 June 2007 George Michael
10 June 2007 George Michael
16 June 2007 Muse
17 June 2007 Muse
1 July 2007 Concert for Dian
7 July 2007 Live Earth
8 July 2007 Metallica
6 June 2008 Foo Fighters
7 June 2008 Foo Fighters
11 September 2008 Madonna

On 16 June 2007, Muse became the first performance to sell out the new Wembley Stadium
On 7 June 2008 The Foo Fighters played to a record crowd of 86,000 fans. They had surprise guests of John Paul Jones and Jimmy Page from Led Zeppelin.
On 11 September 2008, Madonna performed to a sell-out crowd of over 74,000 fans and a gross of over $12 million USD and surpassed all previous grosses at both the old and the new Wembley Stadiums.

Firsts at the new Wembley Stadium
This article may contain an excessive amount of intricate detail that may only interest a specific audience. Please relocate any relevant information, and remove excessive trivia, praise, criticism, lists and collections of links. (October 2008)


Football

League Two Play-Off Final 2008The first match at the stadium was a game played behind closed doors between Multiplex and Wembley Stadium staff. The first game in front of spectators was between the Geoff Thomas Foundation Charity XI and the Wembley Sponsors Allstars on 17 March 2007. The Geoff Thomas Foundation Charity XI won 2-0 (scorers Mark Bright and Simon Jordan). The first official match involving professional players was England U21s vs Italy U21s on 24 March 2007, which finished 3-3. Official attendance was 55,700 (although all of the 60,000 tickets that were made available were sold in advance). The first player to score in a FIFA sanctioned match was Italian striker Giampaolo Pazzini after 28 seconds of the same game. Pazzini went on to score twice more in the second half of the match making him the first person to score a hat-trick at Wembley Stadium since Paul Scholes for England in 1999. The first English player to score in a full-scale match was David Bentley with a free kick in the same game.

The first club game, competitive game, and cup final held at the new Wembley took place on 12 May 2007 when Kidderminster Harriers met Stevenage Borough in the FA Trophy final. Kidderminster striker James Constable was the first player to score a goal in a final at the new Wembley. Kidderminster became the first team to play at both the old and new stadium. Stevenage Borough were the first team to win a final at the new Wembley beating Kidderminster 3-2, despite trailing 2-0 at half time. The first players to play at both the old and new Wembley stadia were Steve Guppy (for Stevenage Borough) and Jeff Kenna (for Kidderminster Harriers). Ex-England international Guppy was the first player to win a final at both stadia (with Leicester City, Wycombe Wanderers and Stevenage)

The first penalty save and first red card came in the Conference National playoff final between Exeter City and Morecambe. The penalty was saved by Paul Jones of Exeter City from Morecambe striker Wayne Curtis. The red card was given to Matthew Gill of Exeter for a headbutt on Craig Stanley of Morecambe.

The first FA Cup Final at the new Wembley (between Manchester United and Chelsea) was on 19 May 2007. Chelsea won 1-0 with a goal by Didier Drogba, making him the first player to score in the FA Cup final at the new Wembley. Chelsea goalkeeper Petr Cech also became the first goalkeeper not to concede a goal in a competitive game at Wembley. Chelsea were the last winners of the cup final at the old Wembley and the first winners at the new.

The first game involving the full English national team was a friendly played on 1 June 2007, against Brazil. The match saw captain John Terry become the first England international goal scorer at the new stadium when he scored in the 68th minute. Diego became the first full international player to score for a visiting team when he scored in stoppage time, with the fulltime result being a 1-1 draw. The first competitive senior international was played on 8 September 2007 between England and Israel. This game ended 3-0. The first player to score international goals at both the old and new stadia was Michael Owen when he scored for England against Israel. On 22 August Germany beat England 2-1 to become the first team to beat them in the new Wembley Stadium England's first competitive defeat at the new stadium was on 21 November 2007 when Croatia won 3-2. This match cost England qualification to Euro 2008 and head coach Steve McClaren his job.


Rugby league
The Rugby League Challenge Cup Final had previously been played annually at the old Wembley Stadium since 1929, when Wigan were the victors, and in 2007 the cup final returned to its traditional home after the re-building of Wembley.
When Catalans Dragons played St Helens in the 2007 Challenge Cup Final on 25 August, they became the first non-English rugby league team to play in the final. The result saw St Helens retain the cup by a score of 30-8.
The first Rugby League team to win a game at the new Wembley Stadium, were in fact Normanton Freeston. The West Yorkshire secondary school beat Castleford High School in the Year 7 boys Carnegie Champion Schools final, which was played immediately prior to the 2007 Challenge Cup Final.
The first official try at Wembley was scored by James Roby of St Helens, although there had been several tries scored in the schools game that took place before the 2007 Challenge Cup final.

Rugby union
The first rugby union International at the new Wembley stadium was between the Barbarians and Australia on 3 December 2008.
The first rugby union match at the Wembley stadium was played as part of a school tournament before the first International. The match was won by East Barnet School from North London with a score of 25-0, and the first ever rugby union coach to win at the new Wembley was one Russell David Christie from Christchurch, New Zealand.

American football
On 28 October 2007, the New York Giants defeated the Miami Dolphins by a score of 13-10 in the first NFL regular-season game to be played outside of North America, and first ever to be played in Europe.
The first touchdown scored at Wembley was on a run by quarterback Eli Manning of the New York Giants.


Source: From Wikipedia, the free encyclopedia (This page was last modified on 15 June 2009 at 15:08)

Friday 12 June 2009

Setanta tv financial crisis

Tycoon confirms Setanta rescue bid.
(Tycoon Len Blavatnik has tabled a rescue deal for pay-television firm Setanta)

US tycoon Len Blavatnik has tabled a proposed rescue deal for pay-television firm Setanta, it has been confirmed.

The £20 million offer for 51% of Setanta is aimed at securing the future of the cash-strapped Irish broadcaster by helping it avoid administration.

The Irish-based broadcaster has around 1.2 million subscribers, but that is short of the reported 1.9 million it needs to break even.

Setanta's potential white knight founded Access Industries, a privately owned industrial group, in 1986. It also has interests in Top-up TV, which is Freeview's pay TV service, Israeli television's Sport 5 and online sports provider Perform Group.

Access currently has a holding of less than 5% in Setanta.

A statement from the firm said: "Access Industries can confirm that this morning it submitted a proposal to the board of Setanta to acquire a majority interest in Setanta, refinancing the company.

"The Access proposal is subject to a number of pre-conditions being met.

"Access believes that this proposal would secure the future of the broadcaster for customers, football and employees."

The spokesman said he was unable to disclose the terms of the proposal.

Setanta has TV rights including the FA Cup, World Cup qualifiers, Premier League, Scottish Premier League, and the Blue Square Conference - but is struggling to pay for them as customer numbers have dwindled in the recession.

source: http://uk.news.yahoo.com
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, WAKATI AKIWAHUTUBIA WANANCHI WA DODOMA, NA WABUNGE KWENYE UKUMBI WA KILIMANI, DODOMA TAREHE 10 JUNI, 2009



Waheshimiwa Wabunge;
Ndugu wananchi;
Nawashukuru kwa dhati wazee wangu, Waheshimiwa Wabunge na wananchi wenzangu wa Dodoma, kwa kuitikia wito wangu wa kuja kukutana na kuzungumza nanyi. Nakushukuru Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa na Katibu wa Baraza la Wazee kwa maandalizi mazuri.
Mara kadhaa katika hotuba zangu za siku za nyuma, nimekuwa nikielezea jinsi ambavyo uchumi wa dunia unavyopita katika misukosuko mikubwa na jinsi ambavyo mtikisiko huo unavyoweza kuathiri uchumi wetu pia. Tayari athari zake tumezipata na tunaendelea kuathirika nazo. Nilifanya uamuzi siku za nyuma wa kuunda kikundi kazi cha watalaam chini ya uongozi wa Gavana wa Benki Kuu, Profesa Benno Ndulu, kufanya uchambuzi wa hali ilivyo ili kubaini athari tulizopata na kushauri hatua za kunusuru uchumi wetu na kujenga uwezo wa kujihami na kukuza uchumi.

Ndugu Wananchi;
Wenzetu hao wamemaliza kazi yao na taarifa yao imeshajadiliwa na Baraza la Mawaziri na maamuzi kufanywa. Matokeo yake ni kuwepo kwa mkakati wa Kunusuru Uchumi wa Tanzania dhidi ya Msukosuko wa Uchumi wa Duniani. Katika mkakati huo mpango wa utekelezaji wa malengo na hatua mbalimbali za kuchukua zimeanishwa.

Mtikisiko Katika Mfumo wa Fedha Duniani
Ndugu Wananchi;
Uchumi wa dunia unakabiliwa na matatizo makubwa sana ambayo hayajawahi kutokea kwa zaidi ya miaka 60. Mara ya mwisho uchumi wa dunia ulikuwa na matatizo makubwa katika miaka 1930 lakini nayo hayakuwa makubwa kama ilivyo safari hii. Matatizo ya uchumi wa dunia yana sura mbili. Upande mmoja lipo tatizo la kuvurugika kwa masoko na mfumo wa fedha wa kimataifa. Na, upande wa pili kudorora kwa uchumi wa dunia kulikosababishwa na kuanguka kwa masoko ya fedha na mitaji.

Tatizo hili limeanzia Marekani kutokana na udhaifu katika usimamizi wa mfumo wa fedha na hasa mikopo. Baadae ukaenea Ulaya Magharibi na hatimaye dunia nzima na siye tukiwemo. Kiwango cha athari kinatofautiana kutoka nchi moja na nyingine. Mataifa makubwa kiuchumi ya Marekani, Ulaya na Asia yameathirika zaidi kuliko nchi maskini za Afrika. Hata hivyo, mataifa makubwa yana uwezo mkubwa zaidi wa kukabiliana na athari hizo pamoja na ukubwa wake. Mataifa maskini kama yetu hayana uwezo wa kukabiliana hata na hizi athari ndogo zinazotukabili. Kinachoonekana kidogo kwao, kwetu sisi ni kikubwa.
Mabenki mengi, makubwa kwa madogo, na asasi za fedha kubwa na ndogo katika mataifa tajiri zimeshashuhudiwa zikianguka kibiashara au kufilisika. Masoko ya hisa na mitaji nayo hivyo hivyo yameanguka kwa kiasi ambacho hakijawahi kufikiwa. Makampuni mengi madogo na makubwa yameanguka. Watu wengi wenye hisa wamejikuta wakiharibikiwa na hata kuwa maskini bila kutazamia.
Makampuni mengi yameanguka kibiashara na kufilisika. Watu wamepoteza ajira kwa mamilioni na wengi wamepoteza nyumba na mali walizozipata kwa mikopo kwa sababu ya kushindwa kulipa mikopo. Kwa ujumla hali ya kiuchumi na kimaisha katika nchi hizo ni ngumu kwa makampuni mengi na watu wengi.
Kutokana na hali hii, uwekezaji umepungua, biashara ya ndani na nje imeshuka, uzalishaji viwandani umepungua sana na kwingine umesimama, makampuni madogo na hata makubwa na yenye heshima yamefilisika, ununuzi wa bidhaa umepungua, watu kwa mamilioni wakakosa ajira katika nchi kubwa kiuchumi. Athari hizo bado zinaendelea na matokeo yake ni kuzorota kwa ukuaji wa uchumi wa mataifa hayo makubwa na uchumi wa dunia kwa ujumla. Mwaka 2008, uchumi wa nchi hizi ulikua kwa asilimia 0.9. na mwaka huu inatarajiwa utapungua kwa asilimia 3.8.
Hali hii imezilazimisha Serikali za nchi hizo kuingilia kati na kutumia fedha za Serikali kuokoa makampuni binafsi, kinyume kabisa na falsafa ya soko huria. Vilevile, Serikali za nchi hizo zikalazimika kukopa fedha nyingi kwa ajili ya miradi mingi mikubwa ili kuchochea shughuli za kiuchumi.

Athari kwa Tanzania
Ndugu Wananchi,
Kwa upande wetu hapa nchini mabenki yetu yako salama kwa vile hatujafungamanishwa na masoko ya fedha ya kimataifa. Lakini, kibiashara na baadhi ya shughuli za kiuchumi, tumeathirika hasa zile zinazotegemea masoko ya kimataifa hususan ya mataifa tajiri ya Marekani, Ulaya na Asia. Athari kubwa ya kwanza ni ile ya kupungua kwa bei na masoko ya bidhaa zetu tunazouza nje ya nchi hususan mazao ya kilimo, madini na bidhaa za viwandani. Kadhalika, sekta ya utalii nayo imeathirika na kupungua kwa watalii wanaokuja nchini. Vilevile uwekezaji wa kutoka nje umepungua.
Kwa upande wa mauzo ya mazao ya kilimo napenda nitoe mifano ya pamba, kahawa na hata maua na karafuu. Kwa pamba, kwa kipindi kifupi cha miezi minne kuanzia Septemba 2008 bei ya pamba ilianguka kutoka senti 82 za dola kwa paundi moja mpaka senti 40. Hivyo pamba iliyonunuliwa kwa bei ya juu toka kwa wakulima, ghafla ilibidi iuzwe kwa bei ya chini na nyingine kukosa soko kabisa. Hadi mwezi Aprili 2009 marobota 124,344 ya pamba yalikuwa bado hayajauzwa. Inakadiriwa kuwa hasara iliyopatikana kwa kuuza pamba nje kwa bei chini ya bei ya kununulia ni kadiri ya shilingi bilioni 15 na 18. Unapochanganya tatizo hili na lile la pamba kutokuuzwa, shilingi bilioni 93.6 zilizokopeshwa na CRDB peke yake (bila kujumuisha riba) hazijarejeshwa. Kati ya madeni hayo, shilingi bilioni 4.6 ni ya vyama vya ushirika na TSh bilioni 81.9 ni ya makampuni 24 makubwa yanayofanya biashara ya pamba.
Vilevile, kwa upande wa zao la kahawa, kutoka mwezi Oktoba, 2008 bei zilianza kushuka kutoka wastani wa US$ 140 kwa gunia la Arabica hadi wastani wa US$ 104.21. Robusta nayo ilishuka toka wastani wa US$ 91 kwa gunia hadi dola za Marekani 64 ilipofika mwezi Machi 2009, ikiwa ni anguko la bei la asilimia 26 kwa Arabica na asilimia 29 kwa Robusta. Kahawa iliyokumbwa na msukosuko huo ni kiasi cha kilo 26,645,439 za Arabica zenye thamani ya US$ 55,536,099 na kilo 11,981,710 za Robusta zenye thamani ya US$ 15,469,353.
Kutokana na bei za kununulia kahawa hizo kwa mkulima (farm gate price) kuwa za juu kuliko ile ya kuuzia kwenye soko la dunia, vyama vya ushirika vya kahawa na wafanyabiashara walionunua kahawa wamepata hasara inayokadiriwa kuwa TSh bilioni 4.85.

Ndugu Wananchi;
Hasara waipatayo wanunuzi na ugumu waupatao kuuza mazao yao kunasababisha washindwe kulipa madeni yao Benki na kuwaweka kwenye hatari ya kufilisiwa mali zao walizoweka dhamana. Aidha, kwa ukubwa wa mikopo ambayo haijalipwa na ambayo huenda isilipwe itayafanya mabenki yaliyokopesha kupata hasara. Pia mabenki hayo yanaweza kukataa kuwakopesha wanunuzi wa mazao na kusababisha mgogoro mwingine mkubwa wa mazao ya wakulima kutokununuliwa msimu ujao. Jambo hilo likitokea litafanya wakulima kula hasara na kuwa maskini zaidi.
Shabaha ya mkakati wetu ni kumpunguzia mnunuzi mzigo wa hasara na madeni, kuiepusha benki na hasara na kuwezesha mazao ya mkulima kuendelea kununuliwa.
Kwa upande wa kilimo cha maua na mboga mambo ni hayo hayo. Bei imeshuka kwa asilimia 25 na mauzo yamepungua kwa sababu mahitaji katika masoko ya nje yamepungua kutokana na hali mbaya ya uchumi katika nchi hizo. Kuna hatari kwamba wakulima wa maua watashindwa kulipa mikopo ya mabenki ya Tshs. bilioni 43.4, ajira za watu zitapotea (tayari Mount Meru Flowers imepunguza watumishi 36). Sekta hii inaajiri watu 3,000 na wengi wao ni wanawake. Ni dhamira yetu pia hapa kuwanusuru wakulima, mabenki na ajira.

Madini
Ndugu Wananchi;
Hali ni mbaya pia kwa upande wa bei na masoko ya vito hasa almasi na Tanzanite. Bei ya Tanzanite imeshuka kwa asilimia hamsini na kufikia US$200 kwa karati. Bei ya almasi imeshuka kwa asilimia 26 na kuwa US$8,870 mwezi Septemba. Wachimbaji na wanunuzi wa almasi, Tanzanite na vito vinginevyo wanakabiliwa na tatizo kubwa la madini ambayo wanapata taabu kuyauza.
Bahati nzuri dhahabu haina matatizo hayo. Soko lake ni zuri na bei ni nzuri sana. Mkakati wetu unalenga namna ya kuwasaidia wachimbaji wa vito ambao tusipowasaidia wao na serikali tutaendelea kukosa mapato na wakati huo watu wengine watakosa ajira kwa sababu ya shughuli za uchimbaji kupungua.

Viwanda na Utalii
Ndugu Wananchi;
Viwanda vyetu navyo hasa vya nguo, nyuzi, mavazi na vile vya ngozi vimeathirika na msukosuko wa uchumi wa dunia. Mauzo nje yamepungua sana na kusababisha hasara kubwa. Uzalishaji umepungua, ajira nazo hali kadhalika.
Sekta ya Utalii ambayo ndiyo sekta kiongozi kwa mapato ya fedha za kigeni nayo imebanwa pia. Idadi ya Watalii wanaokuja nchini inapungua. Takwimu zinaonyesha idadi hiyo kupungua kwa asilimia 10. Mapato yatokanayo na utalii ya mwezi Januari – Aprili, 2009 nayo yamepungua na kufikia US$302.1 kutoka US$388.2 milioni mwaka 2008. Hali hiyo inaathari kubwa kwa wawekezaji na kwa mapato ya Serikali na fedha za kigeni hivyo nayo tumeipa uzito stahiki katika mkakati wa kunusuru uchumi.

Mapato ya Ndani
Ndugu wananchi,
Kutokana na matatizo ya kupungua mauzo nje, utalii, uwekezaji n.k mapato ya ndani ya Serikali nayo yameathirika. Sasa hivi, tunakusanya mapato kutoka ushuru wa forodha, kodi za ndani n.k yako chini ya kiwango tulichotarajia. Kama mwenendo wa makusanyo ya kodi utaendelea kama ulivyo sasa, makusanyo ya kodi kwa mwaka 2008/09 yatakuwa chini ya makadirio ya bajeti kwa asilimia 10. Kwa maneno mengine, tutashindwa kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 472.9 ambazo matumizi yake tulishayapangia kwenye bajeti. Katika mkakati huo tumeweka mipango ya kuikabili hali hiyo katika mwaka huu wa fedha na mwaka ujao pia ambapo tunadhani athari zitakuwepo au hata kuzidi.

Mapato ya Fedha za Kigeni
Ndugu Wananchi;
Kwa sababu ya kupungua kwa mauzo ya mazao yetu nje, mapato yetu ya fedha za kigeni yatapungua pia. Inakadiriwa kuwa thamani ya mauzo nje itapungua kutoka US$ 2,891 milioni mwaka 2008/09 hadi US$2,860 milioni mwaka 2009/10. Wakati huo huo mapato ya fedha za kigeni kutokana na utalii yatapungua kwa US$ 186 milioni. Katika mkakati wetu tunayo mipango ya kuziba pengo hilo ili kuepuka matatizo ya upatikanaji wa fedha za kigeni kwa ajili ya manunuzi yetu ya nje.

Uwekezaji kutoka nje
Ndugu Wananchi;
Kwa sababu ya matatizo ya uchumi uwekezaji wa vitega uchumi kutoka nje umepungua. Wawekezaji wamekuwa wanakosa fedha kutoka mabenki na masoko ya mitaji. Matokeo yake ni kuchelewa au kukosa kabisa au kuahirishwa miradi mikubwa ambayo ingetoa mchango muhimu kwa ukuaji wa uchumi wetu na ajira. Kwa mfano: Mradi wa umeme wa MW 300 kule Mtwara kwa sababu ya Barrick Gold Ltd. kujitoa na Artumas peke yake haina uwezo wa kifedha; mradi wa nickel Kabanga, mradi wa aluminium smelter, Mtwara; mradi wa usambazaji umeme mkoani Mtwara, miradi ya viwanda vya saruji na mbolea Mtwara na uwekezaji katika utafutaji wa madini umepungua kutoka US$90 mpaka US$40 milioni.

Ajira
Ndugu Wananchi;
Hali ya ajira nchini nayo itakuwa mbaya kutokana na matatizo haya. Mwaka 2009 ni mwaka ambao athari za msukosuko zimeanza kujitokeza kwa nguvu katika masoko ya ajira na kusababisha watu wengi kupoteza kazi na hivyo kuongeza umaskini wa kipato.
Hadi kufikia Aprili 2009 jumla ya wafanyakazi 48,000 walikuwa wamepoteza ajira zao nchini. Kutokana na kutarajiwa kupungua kwa idadi ya watalii wanaokuja nchini, baadhi ya hoteli zilizotarajiwa kuwapokea watalii hao zimelazimika kupunguza wafanyakazi wao kutokana na kupungua kwa biashara. Kati ya asilimia 20-30 za ajira katika sekta ya utalii Zanzíbar ziko hatarini kupotea kutokana na upungufu wa utalii.
Vivyo hivyo, katika sekta ya kilimo, viwanda na madini, watu wengine wanatarajiwa kupoteza kazi zao.

Kupungua kwa ukuaji wa uchumi
Waheshimiwa Wabunge, Ndugu Wananchi,
Matokeo ya athari zote hizi ni kupungua kwa kasi ya ukuaji wa uchumi nchini. Kama mjuavyo, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, uchumi wetu umekuwa ukikua kwa kiwango cha juu cha wastani wa asilimia 7.2. Tulitegemea mwaka huu uchumi wetu ungekuwa kwa zaidi ya asilimia 8 na kufikia asilimia 10 mwaka 2010 kama tulivyoahidi kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2005. Lakini kama wasemavyo Waswahili, ng’ombe wa maskini hazai. Msukosuko wa fedha na uchumi duniani umesababisha ukuaji wa uchumi wa Tanzania kupungua kutoka asilimia 7.4 mwaka jana hadi kati ya asilimia 5-6 mwaka huu. Kwa upande wa Zanzibar, uchumi wao unategemewa kukua kwa asilimia 4.5 mwaka huu ukilinganisha na asilimia 5.4 mwaka jana.

Mkakati wa Kuhami na Kuunusuru Uchumi
Ndugu Wananchi;
Baada ya kutafakari hali hii, na kuchambua athari hizi nilizobainisha kwa uchumi, ustawi na mipango ya muda mrefu ya maendeleo ya Taifa letu, na kwa kuzingatia azma yangu niliyoitangaza kwenye salamu ya mwaka mpya wa 2009, kwamba mwaka huu ni mwaka wa kuhami na kukuza uchumi, tumebuni na tutatekeleza Mkakati Maalum wa Kuhami na Kuunusuru Uchumi wa Tanzania.
Mkakati huu unazingatia ukweli kuwa msukosuko wa uchumi duniani ni wa kupita. Changamoto ya muda mfupi ni jinsi ya kujinusuru na hatimaye kudumisha juhudi za maendeleo baada ya msukosuko kupita.
Katika kukabili athari hizi nilizozitaja, tunalenga mambo mawili makuu. Kwanza ni kupunguza makali ya msukosuko, na pili, kulinda uwekezaji ambao ni muhimu katika kudumisha ukuaji endelevu wa uchumi katika kipindi cha muda wa kati.
Mkakati wetu wa kuhami na kuunusuru uchumi unalenga kukabili matatizo ya mpito na dharura – hasa ya ukwasi (liquidity) na siyo ufilisi (solvency). Mkakati huu sio mbadala wa mipango ya maendeleo na bajeti ya Serikali ya kila mwaka. Chini ya mkakati huu Serikali imepima matatizo kwa uzito wake na kushughulikia yale tu yaliyojitokeza hivi karibuni kutokana na msukosuko wa uchumi na siyo vinginevyo.

Ndugu Wananchi;
Tumetengeneza Mkakati huu kutimiza malengo makubwa manne:
1. Kulinda ajira na vipato vya wananchi;
2. Kuhakikisha upatikanaji wa chakula;
3. Kulinda uwekezaji muhimu katika miradi ya maendeleo, hususan miundombinu, na
4. Kulinda programu muhimu za kijamii

Ndugu Wananchi;
Kama nilivyosema, lengo kuu la kwanza la mkakati huu ni kupunguza makali au kuhimili shinikizo la msukosuko, hususan kuwalinda wananchi walio katika hatari kubwa zaidi ya kimaisha. Katika kutekeleza hili lengo yako mambo kadhaa ambayo tutayafanya:
(i) Kufidia hasara waliyopata wanunuzi wa mazao msimu wa 2008/09
Serikali imeamua kufidia vyama vya ushirika na makampuni yaliyonunua mazao ya wakulima na kuyauza kwa hasara. Hasara hiyo inayokisiwa kufikia shilingi 21.9 bilioni imepatikana kutokana na bei ya kuuzia mazao hayo kuwa chini sana ya gharama iliyotumika kuyanunua. Serikali italipa madeni yenye thamani ya hasara hiyo, moja kwa moja kwa mabenki yaliyokopesha vyama na makampuni hayo. Lakini tutafanya uhakiki kabla ya kulipa. Napenda kusisitiza kuwa hatutalipa madeni ya zamani ambayo hayahusiki na msukosuko wa uchumi wa dunia.

(ii) Kutoa udhamini wa kuahirisha mikopo ya waathirika
Yapo madeni ambayo wakopaji kwa sababu ya msukosuko wa uchumi wa dunia wanapata matatizo kulipa kwa wakati. Kundi hili linawajumuisha wengi wenye viwanda, wenye shughuli za utalii, kilimo n.k. Madeni hayo yanafikia Shs.270 bilioni.
Serikali itayadhamini madeni na kuyataka mabenki kuahirisha ulipaji wa mikopo hiyo na riba yake wa miaka miwili. Udhamini wa Serikali utatolewa kwa uwiano wa kila shilingi moja kwa shilingi tano na Serikali ikidhamini asilimia 70 ya mkopo. Kwa uwiano huu, fedha zitakazohitajika katika dhamana hiyo ni TSh 45 bilioni. Pamoja na kutoa nafuu kwa makampuni lakini hatua hii pia itayawezesha mabenki kuendelea kutoa mikopo na hivyo shughuli za kiuchumi na biashara hazitaisimama.

(iii) Kutoa mitaji ya uendeshaji (working capital) kwa riba nafuu
Tumeamua vilevile kuchukua hatua za kupunguza upungufu wa mitaji ya uendeshaji (working capital). Kwa ajili hiyo Serikali itayakopesha mabenki fedha kwa riba nafuu ya asilimia 2 ili na wao wawakopeshe wafanyabiashara fedha za mitaji ya uendeshaji kwa riba nafuu. Lengo ni kusaidia walioko kwenye sekta zinazokumbwa na msukosuko wa uchumi waweze kuhimili vishindo. Kwa kila shilingi moja tutakayotoa sisi Serikali, benki husika itatakiwa itoe shilingi moja na nusu (1:1½).
Kwa madhumuni haya, tutaanzisha mfuko maalumu wenye shilingi bilioni 80 ambao utasimamiwa na Benki Kuu na mabenki yatakayoshiriki yatatakiwa kutoa shilingi 120 bilioni. Viwango vya riba kwa wakopaji vitapangwa kwa maelewano ya pamoja baina ya BoT na mabenki na itategemea sekta na shughuli yenyewe.

(iv) Kuboresha Mifuko ya Dhamana:
Chini ya mkakati huu tutaiboresha na kuiongezea fedha mifuko ya kudhamini mikopo (credit guarantee schemes). Mifuko hiyo ni pamoja na Mfuko wa Udhamini wa Uuzaji wa Mazao Nje ya Nchi (Export Credit Guarantee Scheme -ECGS) na Mfuko wa Udhamini wa Mikopo kwa Wajasiliamali Wadogo na wa Kati (SME Credit Guarantee Scheme). Tutaongeza mtaji wa shilingi bilioni 10 kwa kila mfuko katika mwaka wa fedha wa 2009/10. Nyongeza hii itawezesha kuongeza dhamana ya mikopo ya shilingi bilioni 65 kwenye Mfuko wa Udhamini wa Uuzaji wa Mazao Nje ya Nchi na shilingi bilioni 60 kwenye Mfuko wa Udhamini wa Mikopo kwa Wajasiliamali Wadogo na wa Kati katika kuchochea mauzo ya bidhaa nje na uzalishaji. Hivi sasa mfuko wa ECGS una mtaji wa Shs.32.5 bilioni na umekopesha Shs.161.5 bilioni na ule wa SME una Shs.500 milioni na umeshakopesha Shs.6.5 bilioni.

(v) Kupunguza gharama za vito vya thamani:
Katika sekta ya vito vilivyoshuka bei kwa kiasi kikubwa, kama vile Tanzanite na almasi, tunaangalia uwezekano wa kuahirisha ulipaji wa mrahaba (royalty) kwa wachimbaji wa vito. Lengo ni kuwapa muda wa kupumua na kujijenga. Chini ya mpango huu Serikali itaahirisha mapato ya kiasi cha US$ milioni 0.5 kutoka almasi na US$ milioni 2.5 kutoka tanzanite.

(vi) Kuongeza uzalishaji wa Chakula
Ndugu Wananchi;
Lengo lingine muhimu la mkakati huu ni kuinusuru nchi kutokana na athari za upungufu wa chakula duniani zilizochochewa na msukosuko. Katika kutekeleza hili, mkakati huu utahakikisha kuwa miradi yote ya kilimo, hususan ile ya uzalishaji wa mazao ya chakula, inaendelea kugharimiwa bila kuathiriwa na msukosuko. Lengo la kwanza ni kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula ili kujitosheleza kwa chakula na kuuza ziada nje na hivyo kutumia ipasavyo fursa inayotokana na kuadimika kwa chakula duniani.
Chini ya mkakati huu, pamoja na kuendelea kuhimiza na kusimamia yale mambo yote ya kuongeza tija na uzalishaji kwenye kilimo, tumeamua katika kipindi hiki kufanya yafuatayo: (i) kutoa mikopo nafuu na ya muda mrefu ya shilingi 20 bilioni kupitia TIB kwa sekta binafsi kwa ajili ya kuendeleza kilimo (ii) kutoa shilingi bilioni 20 kwa ajili ya mkopo wa riba nafuu kwa zana za kilimo kama matrekta madogo kupitia mpango wa karadha (lease finance), ambapo, kwa kila shilingi ambayo serikali itatoa, mabenki yatakayoshiriki katika mkakati huu itabidi nayo yatoe shilingi moja: na (iii) Kuongeza kiasi na idadi ya wakulima watakaopata mbolea ya ruzuku kwa utaratibu wa vocha. Benki ya Dunia watatupa mkopo wa US$46 milioni na sisi tutatoa kiasi hicho hicho kwenye mfuko wa mbolea katika mwaka ujao wa fedha (2009/10).
Aidha tumeamua sasa tutumie Hifadhi ya Chakula ya Taifa kusaidia kutuliza bei za vyakula kwa walaji. Tunaiboresha sera ya sasa ambapo Hifadhi hungojea ilani ya njaa. Tumesema kupanda sana kwa bei za vyakula vikuu katika soko ni dalili ya upungufu hivyo kupunguza makali kila inapowezekana. Chini ya mkakati huu, tutatoa shilingi bilioni 20 kwa Hifadhi ya Chakula ya Taifa kwa ajili ya kuongeza akiba ya chakula na kudhibiti mfumuko wa bei.

Miundombinu
Ndugu Wananchi,
Kuhusu lengo la kulinda uwekezaji muhimu, hasa katika miundombinu, ya umeme na reli tumekubaliana kuwa tuendeleze juhudi za kutafuta mikopo kutoka Benki ya Dunia na mashirika mengine ya fedha. Kwa ajili hiyo tutatumia fedha za IMF kukwamua mradi wa usambazaji umeme Mtwara. Zinatakiwa US$ 7 milioni. Kuhusu Shirika la Reli, sisi tuchangie sehemu yetu, yaani US$43 milioni, kuongezea US$ 40milioni za Benki ya Dunia kuimarisha reli yetu. Wakati huo suala la uendeshaji tulitafutie jawabu muafaka.
Kadhalika tumekubaliana kuwa taendelee kuwekeza katika ujenzi wa barabara na miradi ya elimu, afya na maji. Suala la hati-fungani ambalo liliahirishwa kwa sababu ya matatizo ya soko la fedha tulitafutie vyanzo mbadala.

Ndugu Wananchi;
Tumekubaliana pia katika mkakati huu, kuwa lazima kuhakikisha kuwa utulivu wa uchumi unakuwepo ili kuhimiza ukuaji endelevu wa uchumi na kuvutia sekta binafsi kushiriki. Vilevile tuongeze kasi ya kuharakisha uimarishaji wa TIB na uanzishwaji wa Agricultural Development Bank.

Ndugu Wananchi;
Kuhusu lengo la Mkakati la kulinda programu muhimu za kijamii, Serikali itahakikisha kuwa mipango yote ya kijamii haitaathirika, hata ile ambayo itakosa fedha za kutosha kutoka kwa wafadhili. Hii inajumuisha mipango ya utoaji wa ruzuku kwa dawa za kurefusha maisha kwa wagonjwa wa UKIMWI, vyandarua vya kuzuia malaria, programu za kifua kikuu, na nyingine za kusaidia juhudi za vijana na kulinda makundi ya wanyonge.

Ndugu Wananchi;
Pia zipo hatua kadhaa nyingine za kisera ambazo Serikali inaziandaa katika kukabiliana na athari za msukosuko huu. Katika miezi inayokuja, Wizara mbalimbali zitatangaza hatua za kisera zenye nia ya kuzihami sekta hizo na athari hizi na kuchochea ukuaji wa sekta mbalimbali kama vile utalii na viwanda. Miongoni mwa hatua tunazoziandaa sasa ni kupunguza gharama za visa kwa watalii kutoka dola 100 na 200 na kuwa dola 50. hazina inaangalia uwezekano wa kufanya hivyo.

Namna Serikali Itakavyolipia Gharama za Programu Hii
Ndugu Wananchi;
Kutekeleza Mkakati huu ni gharama kubwa. Zitahitajika kiasi cha shilingi bilioni 1,692.5. Tumetenga pesa hizo katika Bajeti yetu ya mwaka wa fedha utakaoanza Julai, 1, 2009. Sehemu kubwa ni fedha zetu lakini pia tutapata misaada kutoka kwa marafiki zetu wa maendeleo hasa Benki ya Dunia, IMF, EU na India.

Hitimisho
Ndugu Wananchi,
Sasa nimefika mwisho wa hotuba yangu. Nawashukuru tena kwa kukubali wito wangu. Kwa nchi yetu ambayo bado ina safari ndefu katika maendeleo, hatua tuliyochukua hapa ni kubwa na ya kihistoria. Katika kuchukua hatua hii, tumezingatia mahitaji ya dhamana tuliyopewa na wananchi katika kuwaongoza na kusimamia maendeleo na ustawi wao na wa nchi yetu. Lakini vilevile, tumezingatia mafundisho ambayo historia ya nchi yetu imetupatia. Kwa mkakati huu, tumedhamiria kuepuka hali iliyojitokeza miaka ya 1980 ambapo kutokana na kushindwa kukabili kwa dhati na wakati muafaka, athari za kupanda kwa bei za mafuta na hali mbaya ya uchumi wa dunia iliyofuatia, zilisababisha nchi kupoteza miongo miwili ya ukuaji wa uchumi na mafanikio yaliyokuwa yamepatikana katika nyanja za jamii na miundombinu.
Mwisho kabisa, nawasihi viongozi wenzangu na wananchi kwa ujumla, tuwe wavumilivu na tuiunge mkono Serikali katika kutekeleza mkakati huu. Tangu mwaka 2006, mambo hayakuwa mepesi sana, tumepitia misukosuko mikubwa kwa uchumi wetu: mgao mkubwa wa umeme, njaa, bei kubwa ya mafuta na bei kubwa za vyakula na sasa msukosuko huu wa aina yake. Kwa kila tatizo tumepambana nalo kiume na kwa umakini mkubwa na kuvuka salama. Mshikamano wetu, umoja wetu ndiyo uliotufikisha hapo.
Napenda kuwahakikishia wananchi wa Tanzania kwamba Serikali yao inawajali na inafanya kila lililo ndani ya uwezo wake kutimiza wajibu wake katika kuwatumikia.
Sisi katika Serikali tupo kwa ajili yenu na tutaendelea kuwatumikia kwa nguvu zetu zote. Tutaendelea kutengeneza mipango na mikakati ya kukabiliana na matatizo na changamoto zinazowakabili wananchi wa Tanzania walioko katika kila kona ya nchi yetu. Tuliyaweza yale naamini na haya tutayamudu!!
Asanteni sana kwa kunisikiliza!
Mungu Ibariki Afrika!
Mungu Ibariki Tanzania!

Thursday 11 June 2009

Hotuba ya Rais: Hatua za kuokoa uchumi

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425

PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mambo makuu katika Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Jakaya Mrisho Kikwete kwa Taifa kutoka Ukumbi wa Kilimani, Dodoma, – jumatano, Juni 10, 2009.

1. Rais ameelezea hali ya mtikisiko wa uchumi duniani, chimbuko la mtikisiko huo na athari za hali hiyo kwa uchumi wa Tanzania. Athari hizo ni kama ziafuatazo:

(a) Bei na mahitaji ya bidhaa za Tanzania kwenye masoko ya kimataifa yamepungua. Mifano ni mazao ya pamba, kahawa, karafuu,mwani na mazao mengine

(b) Mahitaji na bei za madini ya vito ya Tanzania pia vimepungua kwenye masoko ya kimataifa

(c) Mahitaji ya mazao ya kilimo ya Tanzania kama vile maua na mboga yamepungua pia na mauzo yake nchi za nje yameshuka kwa asilimia 25

(d) Viwanda vya ngozi, nguo, nyuzi na mavazi pia vimeathirika na hivyo kuathiri pia upatikanaji wa ajira nchini

(e) Sekta ya utalii ambayo ndiyo kubwa kwa uingizaji wa fedha za kigeni pia imeathirika kwa watalii wanaokuja nchini kupungua

(f) Mapato ya Serikali pia yamepungua na hivyo kuathiri mapato ya ndani na mapato ya fedha za kigeni

(g) Uwekezaji kutoka nje umepungua pia na baadhi ya makampuni yaliyokuwa yanataka kuja kuwekeza Tanzania, ama yameahirisha ama yamefuta mipango yao ya uwekezaji. Mifano ni mradi wa uwekezaji katika nickel pale Kabanga, Ngara, Kagera na miradi ya umeme, saruji, mbolea na aluminium smelter mkoani Mtwara

(h) Hali ya ajira nchini imekuwa mbaya zaidi kwa sababu ya matatizo hayo ya uchumi na hadi Aprili, mwaka huu, kiasi cha watu 48,000 walikuwa wamepoteza ajira

(i) Vile vile kasi ya kukua kwa uchumi wa Tanzania inakadiriwa kuwa itapungua kutoka kwenye asilimia 7.4 kama ilivyobashiriwa mwaka huu hadi kufikia asilimia 5 hadi 6



2. Kutokana na hali hiyo, Rais Kikwete ametangaza mkakati wa kuhami na kunusuru uchumi wa Tanzania kwa malengo makuu manne yafuatayo:



(a) Kulinda ajira na vipato vya wananchi

(b) Kuhakikisha upatikanaji wa chakula

(c) Kulinda uwekezaji muhimu katika miradi ya maendeleo, hususan miundombinu

(d) Kulinda programu muhimu za kijamii



3. Kutokana na hali hiyo, Rais ametangaza hatua zifuatazo katika kutekeleza mkakati huo wa kuunusuru uchumi (rescue package):

(a) Serikali imeamua kufidia hasara waliyopata wanunuzi wa mazao kwa msimu uliopita wa 2008/2009. Hasara hiyo ni kiasi cha bilioni 21.9 na Serikali italipia hasara hiyo ambayo imetokana na kushuka ghafla kwa bei ya mazao ya Tanzania kwenye soko la kimataifa

(b) Serikali itatoa udhamini kwa kuahirisha mikopo ya walioathirika ambao ni pamoja na viwanda, utalii, kilimo na sekta nyingi za uchumi kwa muda wa miaka miwili. Serikali imeyataka mabenki kutokutoza riba kwenye mikopo hiyo katika miaka hiyo miwili

(c) Serikali itatoa mitaji ya uendeshaji (working capital) kwa riba nafuu na itayakopesha mabenki kwa riba ndogo ya asilimia mbili na mabenki hayo yatatakiwa kuwakopesha wahitaji kwa riba ndogo zaidi kuliko ilivyo sasa.

(d) Serikali imedhamiria kuboresha mifuko ya dhamana ikiwa ni pamoja na mifuko ya kukopesha biashara ndogo ndogo kwa kuiongezea fedha zinazoweza kukopwa na wananchi

(e) Serikali imeamua kuongeza kasi ya uzalishaji chakula kwa kutoa mikopo ya thamani ya bilioni 20 kupitia Benki ya TIB, na pia kutoka kiasi kingine cha sh bilioni 20 kwa ajili ya mikopo yenye riba nafuu kwa ajili ya ununuzi wa zana za kilimo kupitia taasisi za karadha, na kuongeza idadi ya wakulima watakaopata mbolea ya ruzuku na kiasi cha bilioni 90 kwa ajili ya mboleo hiyo. Vile vile, Serikali imeamua kuanza kuutumia Mfuko wa Hifadhi ya Chakula (SGR) kupunguza bei ya vyakula kwa wananchi na hifadhi hiyo itaongezewa fedha za kununulia chakula zaidi

(f) Serikali imeamua kukwamua mradi wa kusambaza umeme mkoani Mtwara na pia kuboresha Reli ya Kati kwa kiasi cha dola za Marekani milioni 43.

(g) Serikali imeamua kuhakikisha kuwa programu zote za kijamii kama maji, elimu na afya kama vile ya kupambana na magonjwa ya ukimwi, kifua kikuu na malaria haziathiriki kwa sababu ya msukosuko wa sasa wa kiuchumi.

(h) MPANGO wote huu utaigharimu Serikali kiasi cha sh bilioni 1, 692.5 (karibu sh trilioni 1.7). Fedha hizo zimetengwa katika Bajeti ya Serikali ya mwaka 2009/2010 inayoanza Julai Mosi, 2009.

Sehemu kubwa ya fedha hizo ni za ndani ya nchi ingawa kutakuwapo na michango ya wabia wa maendeleo kama Benki ya Dunia, Shirika la Fedha Duniani (IMF), Serikali ya India na Umoja wa Ulaya (EU).


chanzo: www.tanzania.go.tz

Monday 8 June 2009

Apprentice 2009 Candidates

Anita Shah Fired: Week 1
"My CV is strong. I am articulate. I can deal with questions and make impactful statements. Many lawyers can’t. People want to chat with me."

Ben Clarke Fired: Week 9
"To me making money is better than sex."

Debra Barr Fired: Week 11
"When I set my sights on something I have to make sure I get it. I am very cautious and only let the people that I can trust see the softer side of me."

Howard Ebison Fired: Week 10
"I am a credible businessman who wants to go far. I'm incredibly ambitious. If I don't go far down this route I shall go far down another route."

James McQuillan Fired: Week 11
"I'm astute and shrewd and smart... maybe blunt at times."

Kate Walsh "My CV speaks for itself. I've always excelled academically and I have really achieved within a corporate environment across sales, marketing and a number of different aspects of business."

Kimberly Davis Fired: Week 5
"I bring honesty and integrity to the table, I don't lie, cheat or backstab. I am not the stereotypical New Yorker and it's a stereotype I've faced."

Lorraine Tighe Fired: Week 11
"I've fought against all the odds. I'm a single mum with no education and I've had a very hard time. It is tough, but to have the confidence I have I should be very proud of myself."

Majid Nagra Fired: Week 3
"I think that business is the backbone to this world. Without companies buying and selling there wouldn't be any economy."

Mona Lewis Fired: Week 8
"I knew I would be selected, not to sound big-headed... I've succeeded in the companies I've worked for because I work hard and I'm honest."

Noorul Choudhury Fired: Week 6
"I have always been ambitious and driven and I've got the capabilities to deliver. I am not all talk... I can manage a team of people, total strangers even, because I am feisty and have attitude."

Paula Jones Fired: Week 4
"I am the girl with a plan. I have great wit and strength of character, and I am resilient to the core."

Philip Taylor Fired: Week 7
"Business is the new rock 'n' roll and I'm Elvis Presley"

Rocky Andrews Fired: Week 2
"For me business is about hard-work, attention to detail, being willing to make mistakes and learning from these mistakes."

Yasmina Siadatan "Business is about a simple formula. Make more than you spend. That's what I do, I keep business simple and it works. I'm good at it."

Friday 5 June 2009

Hotuba Bora (100%) kutoka kwa Rais Kikwete

HOTUBA YA MHE. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, KWENYE UZINDUZI WA KIVUKO CHA MV. MAGOGONI 4 JUNI 2009



Mheshimiwa Dk. Shukuru Kawambwa (Mb), Waziri wa Miundombinu,

Waheshimiwa Mawaziri,

Ndugu Viongozi na Watendaji wa Serikali,

Viongozi wa vyama vya siasa,

Ndugu Wananchi wenzangu,

Wageni waalikwa,

Mabibi na Mabwana,



Awali ya yote, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa kunialika kuja kujumuika nanyi hapa katika uzinduzi wa kivuko kipya cha Mv. Magogoni.

Nawapongeza sana wananchi wa Kigamboni na wa jiji la Dar es Salaam kwa jumla kwa kupata kivuko kipya kiitwacho MV. Magogoni. Kivuko hichi kipya, kikubwa na cha kisasa tumekinunua kutoka Ujerumani kwa gharama ya shilingi 8.5. bilioni. Kimetatua tatizo kubwa lililokuwa linawasumbua watu waliokuwa wanavuka kutoka au kwenda Kigamboni.

Kwa muda mrefu, wananchi wa Kigamboni wamekuwa wakipata adha ya usafiri, maisha yao kuwa hatarini na usalama wa mali zao kuwa mashakani. Vivuko vilivyokuwepo MV. Alina na MV. Kigamboni vilikuwa vimechakaa sana hivyo kushindwa kufanya kazi ipasavyo. Kwa kweli vilikuwa tishio kwa kila hali. Wakati wa kampeni za uchaguzi wa mwaka 2005, Chama cha Mapinduzi kiliahidi kupitia Ilani yake kutatua tatizo la vivuko kadhaa nchini, kimojawapo kikiwa hiki cha Kigamboni. Leo hii tunasherehekea kutimia kwa ahadi yetu kwa wananchi wa Dar es Salaa hasa wale waishio na waendao Kigamboni.

Kadhalika tumeshatimiza ahadi kwa wananchi wa Mwanza kwa kivuko cha Busisi (MV. Misungwi), kivuko cha Kisiwa cha Kome (MV. Kome) na kivuko cha kati ya Bugorora na Ukara (MV. Nyerere). Kwa wananchi wa Ruvuma kuna kivuko cha MV. Ruhuhu na wa Morogoro kivuko cha mto Kilombero.

Kivuko hiki tunachokizindua rasmi leo ndicho kikubwa kuliko vivuko vyote nchini. Kina uwezo mkubwa wa kubeba tani 500 yaani Magari 60 na abiria 2000 kwa wakati mmoja. Kwa kuwa na kivuko hiki tatizo la usafiri sasa siyo gumzo tena. Ifikapo mwezi Septemba, 2009 tatizo litakuwa limekwisha kabisa pale kivuko cha MV. Kigamboni kitakapoanza kazi. Hivi sasa kivuko hicho kinafanyiwa matengenezo makubwa kukirudisha katika kiwango cha juu cha ubora. Kadhalika kule Bususi, Mwanza nako matengenezo ya kivuko cha MV. Sengerema yatakapokamilika shughuli ya uvushaji watu kati ya Kigongo na Busisi katika Ziwa Victoria itakuwa imeimarika sana.



Ndugu Wananchi,

Nimefurahi kusikia kuwa ujenzi wa Kivuko Mv. Magogoni umefanyikia hapa Dar es salaam eneo la Bandari na kuweza kuwapatia ajira vijana 30 ambao wamejifunza na kupata maarifa na ufundi mpya wa ujenzi wa vivuko na hata maboti. Ninaamini kwa uzoefu walioupata wataweza kujiajiri wenyewe kwa kujenga vivuko na boti ndogondogo za uvuvi ili kujipatia riziki na kuboresha hali ya maisha yao.

Serikali itaendelea na utaratibu huu wa kujenga vivuko hapa nchini ili kutoa huduma nzuri ya usafiri wa majini na kuendeleza teknolojia ya ufundi wa kutengeneza vivuko hapa nchini, na kukuza ajira kwa vijana wetu.



Ndugu wananchi,

Ziko sehemu nyingi za nchi yetu ambako kufikika kwake ni kwa vivuko tu. Serikali imedhamiria kuhakikisha kuwa vivuko vyote nchini vinakuwa vya uhakika na salama kwa matumizi ya wananchi kwa kuvikarabati na kununua vipya pale vinapohitajika kadri uwezo wa bajeti ya serikali unavyoruhusu.

Katika kutekeleza hayo, Serikali kwa sasa inakarabati vivuko viwili vya Mv. Kigamboni hapa Dar es Salaam, na Mv. Sengerema huko Mwanza. Aidha, tumenunua vivuko vipya sita vya Kilombero huko Morogoro, Kivuko cha Mv. Nyerere kinachohudumia kati ya Bugorora na Ukara Mkoani Mwanza, Mv. Ruhuhu Mkoani Ruvuma, Mv. Misungwi kinachohudumia kati ya Kigongo hadi Busisi huko Mwanza na Mv. Kome II kinachofanya kazi kati ya Kisiwa cha Kome kwenda Nyakalilo. Vilevile, tutanunua vivuko vipya vya Musoma kwenda Kinesi Mkoani Mara ambapo wananchi wa Kinesi watakwenda Musoma mjini kwa kutumia kivuko kwa muda wa dakika 30 badala ya kuzunguka Kilometa 54, pia tunanunua vivuko vingine vipya vya Rugezi hadi Kisorya Wilayani Ukerewe, Utete mkoani Pwani na Pangani mkoani Tanga.

Vilevile, katika mipango ya miaka mitatu ijayo, Serikali inatarajia kununua vivuko vifuatavyo kuanzia 2009/10:

1. Kivuko cha tani 50 katika maeneo ya Kilambo - Mtwara. Kivuko hiki kitarahisisha usafiri eneo la mwambao wa kati ya Mtwara Tanzania na Msumbiji



2. Kivuko cha tani 50 kitakachotumika kati ya Msanga Mkuu na Mtwara Mjini ambapo kitapunguza usumbufu wa wananchi kuzunguka Km 20 kufika Mtwara.



3. Kivuko cha Mto Rusumo – Ngara Kagera ambapo kitapunguza Km 60 za kuzunguka kuja Bukoba Mjini.



4. Kivuko cha Kyela – Itungi Port wananchi watatumia nusu saa kusafiri kwa kivuko badala ya kuzunguka kwa Km 70 kufika Kyela.



Ndugu wananchi,

Kuna sehemu ambazo tunatumia vivuko kwa sababu ya kujenga madaraja haiwezekani kwa jinsi maumbile yake yalivyo. Lakini zipo sehemu ambazo tunatumia vivuko lakini madaraja yanawezekana kujengwa. Tunachelewa kujenga madaraja kwa sababu ya gharama kubwa na uwezo wetu mdogo wa fedha. Tunayo dhamira ya kujenga madaraja kidogo kidogo katika sehemu hizi.

Moja ya madaraja ambayo tumeshafanya uamuzi wa dhati kabisa kujenga ni Daraja la Kigamboni. Mipango ya ujenzi wa daraja hili imekuwapo tangu uhuru. Lakini sasa tumedhamiria kufanya. Tumeahidi katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM Ibara ya 44 (f) kwamba, katika kipindi cha miaka mitano tuwe tumeanza maandalizi ya ujenzi wa daraja hili. Nafurahi kwamba tutatimiza ahadi hiyo. Na tutafanya hivyo kwa kushirikiana na wenzetu wa sekta binafsi.

Tuko kwenye hatua nzuri za maandalizi. Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) lipo kwenye mchakato kumpata Mtaalam Mshauri ili atayarishe nyaraka za zabuni. Matumaini yetu ni kwamba, ifikapo mwezi Septemba mwaka huu, nyaraka hizo zitakuwa tayari. Mambo yote yakienda kama yalivyopangwa, basi ujenzi wa daraja unaweza kuanza katika mwaka wa fedha wa 2010/2011. Daraja hili litafungua kwa kiasi kikubwa fursa za uchumi na uwekezaji huko Kigamboni.

Vilevile, kwa sasa, tunafanya usanifu wa ujenzi wa daraja tuliloliahidi kwenye ibara ya 44 (i) ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM wa 2005, yaani Daraja la Mto Kilombero ili kuunganisha Wilaya za Kilombero na Ulanga.



Ndugu wananchi,

Hata hivyo, kujenga daraja kuvuka ng’ambo pekee hakutoshi kama barabara za Kigamboni haziko katika hali nzuri. Kwa kutambua hilo tunajenga barabara kwa kiwango cha lami kutoka Kivukoni hadi Mjimwema mpaka Kongowe. Barabara nyingine tutakayojenga kwa lami ni ya kutoka Kivukoni hadi Tungi na nyingine ni ile ya kutoka Mjimwema hadi Pembamnazi. Wakati tunajenga barabara hizi kwa lami, tutaendelea kuimarisha barabara nyingine za Kigamboni, kama ile ya Tungi hadi Kibada.



Ndugu wananchi,

Ukiacha hili la Kivuko ambalo tumelitimiza na barabara za Kigamboni, Serikali inaendelea na jitihada za kupunguza matatizo ya ya usafiri na usafirishaji katika Jiji la Dar es Salaam. Hivi sasa tunaelekeza nguvu zetu katika kujaribu kupunguza msongamano wa magari katika barabara za Dar es Salaam.

Kwa ajili hiyo, zipo barabara ambazo tunazifanyia ukarabati mkubwa ili zirudi katika hali yake ya zamani, kama tufanyavyo kwa barabara ya Mandela. Baadhi tunazijenga upya na kuzipanua kama ilivyo kwa barabara ya Sam Nujoma na barabara ya Kilwa. Nyote ni mashahidi wa kazi inayoendelea kufanyika katika barabara hizo.

Vilevile ziko barabara kadhaa za Dar es Salaam ambazo hivi sasa ni za udongo ambazo tumeamua tutazijenga kwa kiwango cha lami. Nia yetu kuu ni kupunguza msongamano katika baadhi ya mabarabara kwa kutoa fursa kwa magari kuchepukia barabara hizo. Tumekwishatoa kiasi cha shilingi bilioni 20 kwa ajili ya ujenzi na upanuzi wa barabara hizi. Baadhi ya barabara hizo ni pamoja na zifuatazo:

1. Barabara ya kutoka Ubungo Bus Terminal hadi Kigogo Roundabout, na kutoka Kigogo Roundabout hadi Mtaa wa Twiga Jangwani. Maombi yangu ni kwamba wasiue viwanja vya michezo vya Jangwani.



Nimeambiwa kuwa mikataba ya ujenzi wa barabara hizi itasainiwa wakati wowote wiki ijayo na ujenzi kuanza mara moja.



2. Barabara nyingine ni ile ya kutoka Tabata Dampo hadi Kigogo;



3. Vilevile iko barabara ya kutoka Ubungo Maziwa hadi Mabibo External;



4. Barabara ya kutoka Jet Club hadi Vituka hadi Davis Corner ya umbali wa kilomita 12;



5. Barabara ya kuanzia Mbezi Mwisho hadi Barabara ya Nyerere Ukonga Banana kupitia Malamba Mawili na Kinyerezi. Barabara hii itawezesha magari yanayotoka viwandani maeneo ya Nyerere Road kuweza kuanza safari za mikoani au nchi jirani bila kupitia Ubungo.



6. Barabara ya kutoka Tegeta Kibaoni hadi Mbezi Mwisho (Morogoro Road) kupitia Goba. Barabara hii itawawezesha wachukuzi wa saruji kutoka kiwandani Wazo Hill kwenda mikoani au nchi jirani bila kupitia mjini. Vilevile itawezesha wakazi wengi wa maeneo ya Bagamoyo Road, Tegeta na Mbweni kuweza kusafiri mikoani bila kupitia mjini.



7. Tunao mpango wa kutengeneza kwa lami barabara kutoka Tangi Bovu hadi Goba



8. Vilevile tunao mpango wa kupanua njia mbili kipande cha barabara kutoka njia panda ya Morocco hadi Kawe kuungana na barabara ya Bagamoyo kupitia Shoppers Plaza, kupitia Mikocheni na Mlalakua ili kupunguza msongamano mkubwa wa kipande kile cha barabara. Pia kuunganisha kipande cha kutoka Tume ya Sayansi hadi Msasani kwa Mwalimu Nyerere kwa barabara ya njia mbili.



9. Pia barabara ya Kimara Kinguruwe hadi Mabibo External nayo tutaijenga kwa lami. Barabara hii ya kilomita 9 itawezesha watu kupita kuja na kutoka mjini bila kupitia Ubungo;



10. Vilevile, ipo mipango ya kutengeneza kwa lami barabara ya Kimara Baruti hadi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kupitia Msewe na Changanyikeni.



11. Tumefanya mazungumzo mazuri na Serikali ya Japan wakati wowote tutapata majibu kuhusu utoaji fedha kwa ajili wa upanuzi wa barabara ya kutoka njia panda ya Morocco Road hadi Tegeta Kibaoni ambayo itapunguza sana msongamano wa magari Jijini.



Ndugu wananchi,

Nimeona niwape taarifa ya barabara hizi ili mjue hatua tunazochukua kupunguza tatizo la usafiri Dar es Salaam.



Usalama wa Vyombo vya Majini

Ndugu wananchi,

Hali ya usalama wa vyombo vya majini imekuwa siyo ya kuridhisha hata kidogo. Matukio ya ajali za vyombo vya majini hapa nchini yamekuwa mengi mno. Katika kipindi cha kuanzia Januari, 2006 hadi Desemba 2008 yamekuwepo matukio 28 ya ajali zilizo sababisha vifo vya watu 149 na 240 kuokolewa. Majuzi tena kumetokea ajali ya Meli ya Mv. Faith iliyopinduka katika Bandari ya Malindi kule Zanzibar.

Tathmini zinaonyesha kuwa ajali hizo zimekuwa zinasababishwa na ubovu wa vyombo unaochangiwa na umri mkubwa na matengenezo yasiyoridhisha, makosa ya kibinadamu na hali mbaya ya hewa. Wakati mwingine pia uelewa mdogo wa umuhimu na matumizi ya vifaa vya kuokolea umechangia vifo vya watu.

Serikali iliunda SUMATRA kwa nia ya kuboresha usimamizi wa uendeshaji wa vyombo vya majini ili kuongeza usalama wa usafiri majini. Tunaipongeza SUMATRA kwa kazi kubwa na nzuri ambayo imekuwa inafanywa tangu kuundwa kwake mpaka sasa. SUMATRA imeweka maafisa wasimamizi katika maeneo mbalimbali nchini ikiwa ni pamoja na Mwanza, Bukoba, Sumbawanga, Kigoma na Dar es Salaam. Hata hivyo, lazima SUMATRA waongeze udhibiti wa vyombo vinavyosafiri majini. Wawe makini zaidi katika kusimamia ubora wa vyombo hivyo, ujuzi wa manahodha na wafanyakazi wake, ubora wa huduma stahiki kwa abiria ikiwamo zile za kuokolea abiria panapotokea ajali.

Aidha SUMATRA iendelee kutoa mafunzo kwa wamiliki na waendesha vyombo vya usafiri majini ili kuwaongezea ufahamu juu ya umuhimu wa kuzingatia taratibu na kanuni zinazosimamia uendeshaji wa vyombo hivyo.



Ndugu wananchi,

Katika kuimarisha uwezo wetu wa kuzuia na kukabiliana na majanga kwenye maji, Serikali imejenga mnara wa kuongozea meli katika eneo la Magogoni ambao una kituo cha kuratibu shughuli za utafutaji na uokoaji pamoja na kuratibu matukio ya uharamia baharini. Kituo hiki kimezinduliwa mwezi Machi, 2009 na kwa muda mfupi wa uwepo wake, kimeweza kuratibu zoezi la utafutaji na uokoaji wa meli ya Comoro iliyopata ajali ikiwa safarini kutoka Dar es salaam kwenda Comoro tarehe 16 Aprili, 2009. Katika zoezi hilo watu 77 waliokolewa.



Ndugu wananchi,

Kabla sijamaliza, naomba niongelee uvumi ambao umeenea sana ndani ya jamii yetu, hasa kwa wakazi wa Kigamboni. Kumekuwa na upotoshaji mkubwa kwamba eneo zima la Kigamboni limeuzwa kwa wawekezaji. Wapo wanaodai kuwa Kigamboni imeuzwa kwa watu maarufu wa Marekani na wapo wanaodai kwamba imeuzwa kwa watu maarufu kutoka Uarabuni. Mwanzoni niliposikia maneno hayo niliyapuuza. Lakini nikagundua kuwa yameenea sana na yanaaminiwa na watu wengi hata wale ambao ungedhani wana uelewa wa juu wa mambo. Nikamuagiza Waziri wa Ardhi atoe ufafanuzi.

Ningependa nami kurudia kwamba hakuna ukweli kabisa katika uvumi huo. Ninachokijua mimi ni kuwa Jiji Dar es Salaam likishirikiana na Serikali Kuu (Wizara ya Adhi, Nyumba na Makazi) inao mpango kabambe wa kuufanya Kigamboni kuwa Mji Mpya. Hii ni kwa maana ya kwamba uwe umepangwa na kujengwa kisasa. Nia ni nzuri ya kuendeleza Kigamboni na jiji la Dar es Salaam kwa jumla hasa sasa ambapo kutajengwa daraja hivyo kushawishi watu wengi zaidi kupenda kuhamia na kuishi huko.

Tatizo kubwa la Dar es Salaam ni kuwa na nyumba nyingi kujengwa maeneo yasiyopimwa na kupangwa vizuri. Hali hii haikubaliki, tusiiache iendelee hivi. Na tusiiache Kigamboni nayo ikawa hivyo. Mwelekeo huo tayari upo. Ndiyo sababu ya uamuzi huo wa Jiji na Wizara ya Ardhi ambao nia yake ni njema, naomba tuwape ushirikiano na msaada unaostahili.



Ndugu Wananchi,

Naomba sasa nimalize kwa kuwakumbusha wenzetu wa Wizara na hasa TEMESA kuhakikisha kuwa kivuko hiki kunatunzwa ipasavyo. Kinafanyiwa matengenezo ya mara kwa mara kwa mujibu wa ratiba yake. Hamzidishi magari, abiria na mizigo kupita uwezo unaostahili. Tukifanya hayo kitadumu na kutuhudumia kwa miaka mingi kama ilivyokusudiwa. Tuukumbuke daima msemo wa Waswahili usemao “Kitunze Kidumu” na Kitunze Kikutunze” Tusifanye kinyume chake.

Baada ya kusema hayo, sasa niko tayari kwa uzinduzi wa kivuko hiki kipya cha Mv. Magogoni.



ASANTENI SANA KWA KUNISIKILIZA

Saturday 30 May 2009

CCM still powerful - Research

Friday, May 29, 2009
CCM bado ina nguvu Tanzania-Tafiti

The Revolutionary State Party (CCM) is clearly the dominant political party in Tanzania, according to a poll by REPOA, Michigan State University, and Afrobarometer.
79 per cent of respondents would vote for the nominee of the CCM in the next presidential election.
The candidates representing the Civic United Front (CCW) and the Party for Democracy and Progress (CHADEMA) are far behind, with four per cent each.
Only one per cent of respondents would support the candidate of the National Convention for Construction and Reform (NCCR).
Tanzania held presidential and legislative elections in December 2005.
The CCM’s Jakaya Kikwete won the ballot with 80.2 per cent of the vote. His party also won most of multilateral level.
If a presidential election were held tomorrow, which party’s candidate would you vote for?Revolutionary State Party (CCM) 79%
Civic United Front (CUF) 4%
Party for Democracy and Progress (CHADEMA) 4%
National Convention for Construction and Reform (NCCR) 1%
Source: REPOA / Michigan State University / Afrobarometer Methodology:
Face-to-face interviews with 1,208 Tanzanian adults, conducted in June and July 2008. Margin of error is 2 per cent.

(Angus Reid Global Monitor) - kama nilivyochukua kutoka http://charaz.blogspot.com/


source: lukwangule.blogspot.com

Friday 29 May 2009

Starting a Business

Starting a business

Thousands of people set up their own businesses every year. Some do it because they want to work for themselves, others because they have a great idea and have spotted a gap in the market. And of course there are those that think they can make lots of money.

These are all valid reasons for starting a business. Commitment and motivation are vital and whatever it is that drives you to make it a success good.
Although enthusiasm is important, good planning is a must. Without a good business plan you could struggle to make a go of it.

There are many issues to think about:
1. What will the business do?
2. Where can it operate?
3. Will I need premises?
4. Do I need people to make it happen, or will I be flying solo for some time?
5. Can I fund the business myself, or do I need financial support?
6. How long will it take to get the business into profit?
7. Have I got what it takes to make it work?

There is no right or wrong type of person to run a business. If you are determined to make it succeed, and are prepared to work long hours, then you have the ingredients for success.

If you look at top business people, the one thing they have in common is determination. They do not give up at the first hurdle and they keep going until they succeed.


Be your own boss

Obstacles and setbacks
There will be many of these but how you overcome them will be critical to deciding whether or not you will ultimately succeed. If you are not the sort of person who responds well to setbacks, you ought to ask yourself whether you are the right person to be trying to get a business off the ground.

Finances
You need good advisers - usually an accountant and a lawyer - when you are handling complex issues such as finances, tax and business law. All businesses require a certain amount of administration and you will have to spend time going through paperwork. If you tend to bury your head in the sand and ignore detail, you need a good right-hand person who will concentrate on the detail. Not all great business leaders were good at the small print, but all good business people have someone close to them who is.

(source: www.thisismoney.co.uk/help-and-advice)
.........................................................

ONE RED PAPERCLIP BUSINESS!!
My name is Kyle MacDonald and I traded one red paperclip for a house. I started with one red paperclip on July 12 2005 and 14 trades later, on July 12, 2006 I traded with the Town of Kipling Saskatchewan for a house located at 503 Main Street.

That's right, Dom and I are trading the red paperclip house. With who? For what? Well that's where things get interesting:

We have no idea yet.

I'm not looking for anything in particular in exchange for the house, other than maybe several 1990 Burgundy Dodge Caravana with low miles. That aside, it would be great to trade with somebody who:

-Plans to live or operate a business in the house.
-Understands the house is a tourist attraction in Kipling, and important to the community.
-Also, if you know who these guys are, it will come in handy in a tie-breaker situation. -- Watch this video!.

If you'd like to make a trade offer for the house, please contact me at oneredpaperclip@gmail.com or call the number in the contact section of this website.

Really, I'm looking for nothing in particular, just to make a trade and see where this goes. So if you have anything you'd like to offer in exchange for the house, and I mean anything, be sure to send in your offer!

Details about the red paperclip house:
Located at 503 Main Street in Kipling Saskatchewan Canada
Fully furnished.
Two floors + basement
Three bedrooms
Two bathrooms
Refinished hardwood floors.
Fridge, stove, sinks, drawers, shelves...all the regular kitchen stuff.
Electricity!
Large grass front yard + large grass backyard.
Gas hot water tank + gas furnace.
close proximity to schools, restaurants, grocery stores, hospital, etc. Kipling has most services in town.
Giant red paperclip on the front lawn.
located a stone's throw away from the world's largest red paperclip.
Click on thumbs to see more pics of the house:


Once again, if you'd like to make a trade offer for the house, please contact me at oneredpaperclip@gmail.com or call the number in the contact section of this website.

Have fun,

Kyle


Labels: kipling, one red paperclip, oneredpaperclip, red paperclip, saskatchewan, who are these guys

6/17/2008 01:48:00 PM - permalink 76 comments links to this post

How to make an offer for the house To make an offer for the house, please:

1. Send your offer via email to oneredpaperclip@gmail.com

or

2. Call my cell in the contact section of this website.

You can read more about the house by clicking here.

Thanks!

Kyle

6/16/2008 12:50:00 AM - permalink 24 comments links to this post

franglais ***UPDATE: It looks like the video link is down. If anyone has a copy of the link, let me know!****

So I wound up in France on TV to promote the release of the french version of the one red paperclip book, which is called "un trombone rouge." The producers weren't comfortable with my learned-while-drinking-with-friends anglo-quebecois french, so they opted for the live french dub. The effect makes it pretty much impossible to understand what's going on, although my comprehension of french isn't exactly 100%, but the monsieur who did the live voice over has a very nice accent. Highlights of this video include the seemingly rude phenomenon of a guy answering live questions on french TV in english, sharing the stage with Jean Claude Van Damme, and giving the "who are these guys" guys not one, but two plugs. How sweet would it be if Jean Claude Van Damme starred in the one red paperclip movie, and those guys were the bad guys?


source: onepaperclip.blospot.com, by Kyle Macdonald

Business Communication

Working together: business communications

Effective communication is an essential part of a smoothly running business organisation. Communication involves the transmission of information from a source (or a number of sources) to receivers. The information is communicated in the form of a message. In the modern organisation there will be multi-channel flows of communication. For example a customer may request a new part from a supplier, with information on how to use that part in a piece of equipment. The supplier will then communicate with the customer setting out instructions for using the part, as well as sending a delivery note, invoice, and further sales literature. Increasingly these interactions will be carried out by electronic media such as through a sales website, e-mail communications and other means.

The effectiveness of communications depends on:

1.The clarity of the message.

2.The quality of the medium used to transmit the message. The medium is the means of communicating e.g. e-mail, telephone, letter, etc.

3.Any distracting 'noise' that prevent the message from effectively getting through. For example, if the recipient receives lots of e-mail messages, they may fail to give proper attention to the sender's message.

3.The ability of the receiver to decode the message. For example, they may not be able to understand the instructions given.

There are two main forms of business communication:
1.Internal communication, i.e. communication within the business.
2.External communication, i.e. communication outside the business.


Internal communication

Typical forms of internal communication include:

Electronic mail. This has rapidly become the most common form of written communication within an organisation.
Company websites. A website will typically involve a portal or section dedicated to internal communication with and between employees.
Company databases. In most large organisations including banks like Abbey, employees will be able to access a number of company databases e.g. to access details of customers accounts when dealing directly with customers.
Face-to-face interactions. Dealing directly with other employees in an organisation is a regular occurrence and provides an excellent way for sharing ideas and for working co-operatively.
For example, in an Argos store an essential ingredient of processing customer orders is interaction between customer service staff.
At the Inland Revenue, a major aspect of working together is being 'approachable and understanding at all times' in dealing with colleagues.
Meetings can either be of a formal or informal nature.
In manufacturing companies like Nissan teams of employees regularly meet to discuss issues about quality.
Phone communications are another important form of oral communication with most large companies having a low cost internal telephone system.
An internal memo (memorandum) is a short brief message to another member of the same organisation. Typically memos today are sent by e-mail.
Staff magazines, notices and posters on staff notice boards provide other means of internal communications.

Typical forms of external communication include:
1. Written communication in the form of letters, and advertising material such as leaflets, brochures, posters, etc.
2. Oral communication in the form of phone calls, and
3. direct face to face interactions.


Online communications

Oral communication is very important in service industries and staff in organisation like banks, insurance companies etc are specially trained for such work. Oral communication through call centers is particularly important as a poorly trained operator may lose a business millions of pounds worth of sales or custom.
Online communications - have become particularly important with the development of e-commerce. Most large companies have commercial websites enabling customers to buy online.
The Inland Revenue has created a website which enables customers to fill in their tax return online, Cummins the engine manufacturer has an extensive website enabling customers to find out information about servicing and maintaining their engines online. Help is provided to customers through pop-up help facilities.

Television advertising - is another important source of visual communication, and companies like Kraft and Cadbury-Schweppes typically launch new products through exciting television advertising campaigns.

The Times 100 is a good example of a modern business that uses online communication to reach its target audience. The Times 100 provides real case studies about leading business organisations both in an online format and in photocopiable resource packs which are sent out to every school in the UK. Today, thousands of students from all over the world study The Times 100 online, browsing and printing off the case studies, examining theory topics, and testing their knowledge through quizzes and activities. A great advantage for the student is that they are rapidly able to access the parts of the resource that most interest them, as well as being able to interact with the resource in the manner that is most suitable to them.

Email - electronic mail carried on the Internet. Online - being connected to a network - typically on the Internet. You can also refer to a resource being online when it is available on a website. Portal - is a website that leads you to other websites.



(source: www.thetimes100.co.uk/theory/theory--working-together-business-communications---388.php)

Tuesday 26 May 2009

Sir Matt Busby (100 years!)

Sir Matt remembered
One of English football's greatest-ever managers was born 100 years ago this Tuesday (26 May) in the Scottish village of Orbiston.

A former Manchester City and Liverpool player, Matt Busby accepted the position of United manager on 19 February 1945, and then joined the club full-time on his demobilisation from the armed forces in October 1945.

Together with his loyal assistant manager Jimmy Murphy, Busby created a team good enough to win the FA Cup in 1948 and to challenge for the League Championship. After finishing runners-up four times, Busby's men won the title in 1952.

Far from being blinded by their success, Busby and Murphy had the foresight to plan ahead and prepare for the day when their first great team would need replacing. The club's scouting system was expanded and reorganised, soon yielding a young team that won the title again in 1956 and 1957 and reached the FA Cup final in 1957. This young team was christened the 'Busby Babes.'

Busby trailblazed the way for English clubs by entering the European Cup in 1956/57 - initially against the wishes of the Football League. United reached the semi-finals, losing to eventual winners Real Madrid.

The following season, 1957/58, bristled with promise and United were still challenging in all three competitions by February when disaster struck. On 6 February 1958, the aeroplane bringing the team home from a European Cup match against Red Star Belgrade crashed after refuelling in Munich. Twenty-three people were killed, including eight of Busby's players and three club officials.

Busby almost lost his life as well - he was twice given the last rites while lying gravely ill in a German hospital. Fortunately, he survived and returned to Manchester 71 days after the crash. Taking up the managerial reigns again in August 1958, Busby began to rebuild United, bringing in some big money purchases to add to his homegrown talent. The new group of players reached the FA Cup final in 1963 and beat Leicester City 3-1 to claim the club's first trophy after Munich.

League titles followed in 1965 and 1967, giving Busby the chance to conquer Europe in the following seasons. In 1965/66, United reached the semi-finals, just as they had done in 1956/57 and 1957/58. But in 1967/68 they went further, to the final at Wembley where they faced Portuguese side Benfica.

On another night of great emotion, United triumphed 4-1 after extra-time to win the European Cup. It was a fitting tribute to the players and staff killed and injured 10 years before and was Busby's crowning achievement as United manager. Busby retired at the end of the following season, but stayed on as general manager while Wilf McGuinness became the man in charge of the team on a day-to-day basis. The new arrangement lasted little more than a year - on 28 December 1970, Busby was invited by the Directors to return to his old job and replace McGuinness until the end of the season.

A respected figure throughout his career, Busby was awarded the CBE in 1958. Ten years later, was knighted following United's European Cup triumph. In 1993 Warwick Road North, the road which runs past Old Trafford, was renamed Sir Matt Busby Way in honour of the man described as 'Mr Manchester United'.

When, after a short illness, Sir Matt died on 20 January 1994, thousands of people lined the streets of Manchester and similar numbers of shirts, wreaths, pictures and scarves were laid in tribute at Old Trafford. A bronze statue of Sir Matt was unveiled at the stadium on 27 April 1996, as a permanent memorial to the man who epitomised the club.

Five years after Busby's death, United won the European Cup for the first time since 1968. Poignantly, the date of that triumph for Sir Alex Ferguson's side, 26 May 1999, would have been Matt's 90th birthday.


source: www.manutd.com 25/05/2009 07:10 BST
(This article is an extract from Sir Matt's profile on ManUtd.com. Read his full profile in our Players & Staff section. -man utd)

Monday 18 May 2009

Mbagala: wahanga mlipuko wa mabomu

Wapangaji walalamika kubaguliwa


Wakati serikali imesitisha zoezi la kuandikisha nyumba na mali za watu walioathirika kwa mabomu yaliyolipuka katika kambi ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Mbagala, jijini Dar es Salaam, baadhi ya watu waliokuwa wamepanga katika nyumba hizo wamelalamika kuwa mali zao hazijaorodheshwa kwa ajili ya kufanyiwa tathmini.

Tangu mabomu ya JWTZ yalipolipuka Aprili 29, mwaka huu na kuua raia 20 na wanajeshi sita, nyumba zipatazo 7,241 zimekwishafanyiwa tathmini na Kamati ya Kutathmini Mali za Waathirika, iliyoundwa kufanya kazi hiyo. Watu wapatao 200 walijeruhiwa baada ya milipuko hiyo.

Kamati hiyo iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi, ilitakiwa kutoa ripoti ya awali jana, lakini kutokana na kutokamilika, imeongezewa muda hadi mwishoni mwa mwezi huu.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Cleophace Rweye, alisema kuwa zoezi la kuandikisha nyumba na mali limesitishwa rasmi na jambo wanalofanya sasa ni kumalizia kazi ya kuthaminisha mali hizo.

Rweye alisema zoezi hilo linaendelea vema na wanatarajia kumaliza katika muda waliopewa.

Alisema wanachofanya kwa sasa ni kuandikisha na kuthaminisha nyumba mpya ambazo ziliharibiwa na milipuko ya mabomu iliyotokea Jumatano iliyopita wakati askari wa jeshi hilo walipokuwa wakiteketeza mabomu ambayo hayakuwa yamelipuka katika ajali ya kwanza.

Wakizungumza na Nipashe jana, baadhi ya wenye nyumba na wapangaji walilalamikia zoezi zima la uandikishaji wakidai kuwa mali zao nyingi zilikuwa zimeachwa bila kuandikishwa.

Mchungaji wa Kanisa la African Inland (AIC), Ezekiel Mahalu, alisema wathamini hao wameandikisha kanisa tu na kuacha vifaa vya muziki vilivyoharibika vyenye thamani ya Sh. milioni 10.

Alisema wathamini hao hawakuandikisha mali zozote licha ya kutakiwa kufanya hivyo.

Mpangaji Joshua Kishiwa, alisema wakati Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alipotembelea Mbagala baada ya milipuko hiyo, aliwaahidi kwamba nyumba na mali zote zilizoharibiwa zitaorodheshwa na kuthaminiwa kwa ajili ya kuwalipa fidia wahusika.

Kishiwa ambaye alidai kuwa mali zake zimeharibiwa kabisa, alisema hakuna hata moja ambayo imeorodheshwa kwa ajili ya kufanyiwa tathmini.

“Wamechukua picha ya mwenye nyumba wangu na kuandikisha nyumba yake, lakini sikuulizwa kuandikisha mali zangu. Nilifikiri kwamba walikuwa wanaanza kwanza kuandikisha nyumba na baadaye kuandikisha mali. Nimeshitushwa sana kusikia kwamba zoezi hilo limefungwa rasmi,” alisema.

Mustapha Muhidin, alisema haikuwa sahihi kwa wathamini kuzingatia tu suala la nyumba kwa sababu katika nyumba waliyokuwa wakiishi kulikuwa na wapangaji watano na hakuna hata mmoja aliyetakiwa kuandikisha mali zake.

Muhidin alihoji kitendo cha wathamini kwenda kinyume cha agizo la Waziri Mkuu kwa sababu mali zao zote zilikuwa zimeharibiwa na sasa hakuna hata mmoja aliyekwenda kuandikisha mali zao.

Aliiomba serikali kufuatilia zoezi zima kwa sababu mwisho wa siku kutakuwa na malalamiko mengi kutoka kwa wapangaji.

Said Mohamed aliwalalamikia wathamini hao kwa kukataa kuandikisha televisheni yake moja, seti ya DVD pamoja na samani. Alisema kwa sasa hana kazi, hali ambayo itamuwia vigumu kupata vitu hivyo katika siku za hivi karibuni.

“Kama zoezi la uandikishaji limefikia mwisho na mali zangu hazijaandikishwa, ina maana kwamba sitaweza kuwa na televisheni tena,” alisema.

Wakati huo huo, Diwani wa Mbagala Kuu, Anderson Chale, alisema walimkamata mtu mmoja akijaribu kuandikisha nyumba yake ambayo ilikuwa katika hatua ya ujenzi.

Alisema mara baada ya kubaini ukweli kwamba mkazi huyo alikuwa na lengo la kuwadanganya wathamini, jina lake liliondolewa katika orodha ya watu wanaotakiwa kulipwa fidia. Alisema serikali itaendelea kutoa chakula kwa waathirika hadi hapo watakapolipwa fidia.


CHANZO: NIPASHE 18th May 2009

Friday 15 May 2009

Ikulu yampongeza Mhe. Anne Kilango MB

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425

PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mheshimiwa Anne Kilango (MB), Jimbo la Same Mashariki

YAH: KUTUNUKIWA TUZO YA KIMATAIFA YA WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA MAREKANI KWA WANAWAKE JASIRI (SECRETARY OF STATE’S GLOBAL AWARD FOR WOMEN OF COURAGE)

Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amepokea kwa furaha kubwa habari za kutunukiwa kwako Tuzo ya Mwanamke Jasiri kwa Mwaka 2009 inayotolewa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani. Aidha anakupongeza kwa mafanikio hayo makubwa na ya kujivunia.

Kutunukiwa kwako Tuzo hiyo ni ishara ya kutambuliwa na kuthaminiwa kwa mchango wako katika mapambano dhidi ya rushwa. Aidha, ukiwa Mbunge wa Chama Cha Mapinduzi, Tuzo hii ni tunda la wazi la utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya 2005 kuhusu vita dhidi ya rushwa ambayo Chama Cha Mapinduzi na Serikali yake vimetoa fursa pana zaidi kwa wananchi, wanahabari na viongozi wakiwemo Waheshimiwa Wabunge kushiriki kwa ukamilifu zaidi.
Hongera sana.

Ikulu
Dar es Salaam
27 March, 2009


chanzo: www.tanzania.go.tz

Tuesday 12 May 2009

Usitumie pesa kama chambo!

Vitu ambavyo wanawake hupenda mwanamume awe navyo


Sifa moja kubwa kwa wanawake ni ule uwezo wao wa kuzifanyia kwa vitendo hisia zao na mara nyingi huwa wawazi wanapovutiwa au kuchukizwa na kitu lakini huonyesha hisia zao kwa vitendo.

Kwa mfano mwanamume unaweza kukutana na mwanamke na kukubaliana kupeana namba za simu, unapompigia siku nyingine anakubali kutoka na wewe na siku inapowadia mwanamke huyo hatokei, unapompigia anakuambia jambo lingine lililojitokeza. Jambo kama hilo kwa kweli limewatokea wanaume wengi na wameishia kuumia na kuchukia na wengi hata kuwaita wanawake waongo na kwamba hawaaminiki.

Ninachotaka kusema ni kwamba wanawake wengi wanaweza kusema kitu na kufanya kingine na kuona sawa tu kwa vile huwa mara nyingi wanafuata hisia zao. Wanaume wanachotakiwa kufahamu ni kwamba ni mara chache sana wanawake hubadili tabia kama hiyo, hivyo cha kufanya ni wao kujitahidi kuwajengea hisia ili hata wanapopanga miadi ya kuonana, wawe na hisia hizo.

Na hapo ndipo mada yetu inapoanzia ambayo ni kuelezea vitu ambavyo wanawake wanavitaka kwa mwanamume na kuwavutia hisia zao kiasi kwamba mwanamume mwenye sifa hizo anapowekeana nao miadi hawawezi kutohudhuria. Wengi wa wanaume hufikiria kwamba wanawake wengi huvutiwa na wanaume wanaojulikana, matajiri na wenye sura au mwonekano wa kuvutia lakini ukiangalia kiundani hilo linaweza likawa halina ukweli thabiti.

Nasema hivyo kwa kuwa inawezakana kabisa baadhi ya wanawake wakawa hawafahamu ni kitu gani kinachowavutia kwa mwanamume anayemtaka, kwa maneno mengine ni kwamba mambo ya fedha au kujulikana kwa mwanamume kunaweza kutowavutia. Hivyo hata kama mwanamume si tajiri au mwenye sura ya kuvutia anaweza kuwavutia wanawake kulingana na namna atakavyofanikiwa kuzivuta hisia zao.

Jambo la msingi ambalo wanaume wanapaswa kujua kuhusu wanawake ni kwamba wengi wao hutafuta wanaume ambao wanaweza kuzigusa hisia zao bila kujali sura wala fedha walizonazo hayo ni mambo ya nyongeza tu. Japokuwa si wanawake wengi ambao wako tayari kueleza ukweli kuhusu hili, wengi ukiwauliza ni mambo gani wanayatarajia kwa mwenza wao watakwambia kijana mtanashati, mkweli, mwenye mafanikio na mwenye mvuto.

Lakini katika hali halisi kama akifanikiwa kukutana na mwanamume mwenye sifa kama hizo halafu kwa bahati mbaya ikatokea kijana huyo akawa king’ang’anizi ambaye anamfuatafuata mwanamke huyo kila anapokwenda bila kumpa uhuru, basi hawezi kujenga naye uhusiano.

Na kwa upande mwingine mwanamke huyo huyo kama akikutana na mwanamume ambaye hana sifa alizokuwa anazitarajia lakini akafanikiwa kumvuta hisia zake basi anaweza kujenga uhusiano naye tena wa maana. Hivyo basi linapokuja suala la mvuto wa mapenzi kwa mwanamke haliangalii kama mwanamume ni tajiri au masikini, mzuri au anatisha ilimradi tu aweze kuzivuta hisia za mwanamke huyo.

Kinachotakiwa ni mwanamume kujua kutumia lugha na mwili wake pamoja na mbinu nyingine za mawasiliano ambazo zinaweza kumvutia mwanamke badala ya kumkimbia. Si jambo la ajabu siku hizi kwa mwanamume kumpata mwanamke au hata kufanikiwa kuzungumza naye ambaye hapo awali alijiona hatoweza kufanikiwa hilo.

Jaribuni kujiamini na acheni kabisa kutumia fedha kama kigezo cha kumvutia mwanamke kwani wengi wenu fedha zenu zitatumiwa na faida yoyote msiipate. Kumbukeni kuwa anachokitaka mwanamke kwa mwanamume ni tofauti kabisa na kile ambacho kitamvutia kwa mwanamume huyohuyo, hivyo unaweza kuwa na sifa zote lakini kama hukucheza karata zako vizuri ukashindwa kumteka moyo mwanamke unayemtaka.

Dimbwimahaba@dailynews-tsn.com


...............................
chanzo: habari leo Mei 12, 2009.
Imeandikwa na Halima Mlacha; Tarehe: 12th May 2009 @ 07:50

Tuesday 5 May 2009

Ajali ya mlipuko wa mabomu: Wanajeshi waliopoteza maisha

Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa imewataja wanajeshi watano na ofisa wa jeshi hilo mmoja waliopoteza maisha wakati wakiwa ndani ya ghala la kuhifadhia silaha lililolipuka wiki iliyopita. Wanajeshi hao waliopoteza maisha wakiwa ndani ya ghala hilo wakifanya kazi zao za kawaida na kupoteza maisha ni pamoja na Meja A. M Muhidin, Sajini Amelye Mbeyale, Koplo Phinias Mwambashi, Koplo Mohamed Seif na Koplo Bernard Mbilo. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi alimtaja mwingine aliyepoteza maisha kuwa ni Ofisa Mteule Daraja la Kwanza, Timothy Mtweve ambaye alikwenda eneo la tukio kwa ajili ya kuzima moto na kuwaokoa walioumia katika mlipuko huo.

Alifariki dunia alipofikishwa hospitalini kwa matibabu. Dk. Mwinyi alisema katika tukio hilo, wanajeshi wawili waliokuwa nje ya ghala hilo la kuhifadhia silaha walijeruhiwa. “Wengine mwanajeshi na mpishi walikuwa nje ya ghala walifanikiwa kukimbia baada ya kusikia mlipuko na hao tunawategemea kutusaidia kutoa maelezo ya chanzo cha mlipuko huo,” alisema Dk. Mwinyi.

Dk. Mwinyi alisema kuwa Baraza la Uchunguzi limeshaundwa kuchunguza tukio hilo ambalo lina wajumbe tisa na linaongozwa na Meja Jenerali Sylvester Chacha Rioba. Wajumbe wa baraza hilo ni pamoja na wataalamu wa milipuko, wakemia, maboharia, Ofisa wa Polisi, Ofisa wa Idara ya Zimamoto na Ofisa Mhakiki Mali. Hadidu rejea kwa baraza hilo ni pamoja na kuchunguza na kubaini chanzo, madhara, hasara na kupendekeza hatua za kuchukuliwa ili kuzuia tukio kama hilo lisitokee tena. Sambamba na baraza, hatua za ziada zinachukuliwa kuepusha tukio kama hilo lisitokee katika maghala mengine.

Tahadhari ya usalama inatolewa kwa wananchi wote wasiokote au kuficha chuma chochote kilichotokana na mlipuko, silaha, risasi zilizosambaa eneo la mlipuko na kwenye makazi. Vitu vya aina hiyo vitolewe taarifa kwa timu ya wanajeshi wanaovikusanya au kituo cha Polisi, ni kosa la jinai kama mtu atapatikana anahifadhi silaha, risasi au mlipuko wa aina yoyote”, alisisitiza Waziri huyo.

Waziri huyo alisema kazi ya kusafisha eneo la makazi ya wananchi kwa kuondoa vipande vya mabomu na mabaki ya makombora inaendelea na kuwataka wananchi watoe ushirikiano kwa wanajeshi kuwaonyesha yalipo mabaki. Aprili 29, mwaka huu, ghala lililokuwa limehifadhi silaha ndogondogo, mabomu, makombora na risasi katika kambi ya Jeshi Mbagala lililipuka na kusababisha vifo vya wanajeshi hao na raia 18 sambamba na nyumba kadhaa kuharibika.

Wakati huohuo, serikali imesema kwa mujibu wa tathmini kaya 3,750 za wakazi wa eneo la Mbagala Kuu hazina mahala pa kuishi baada ya nyumba zao kuharibiwa vibaya na milipuko hiyo ya mabomu. Aidha, Sh milioni 660.2 zimechangwa na watu mbalimbali ikiwamo serikali kwa ajili ya kusaidia ununuzi wa chakula, maji, mahema, nguo na mahitaji mengine muhimu.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kupokea msaada wa Sh milioni 5.2 kutoka kwa Jumuiya ya Mabohora Dar es Salaam, iliyoongozwa na Makamu Mwenyekiti wake, Zainuddin Adamjee, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi alisema kwa mujibu wa tathmini hiyo mpaka sasa nyumba 4,636 zimeharibika vibaya. “Tunajaribu kufanya kila tunaloweza kuwasaidia waathirika wa tukio hili na tayari serikali imetoa mifuko 3,750 ya mchele ambapo kila kaya itapewa mfuko mmoja wa kilo 30 na maharage kilo 10,” alisema Lukuvi.

Alisema pamoja na hayo wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwamo ya ukosefu wa mahema ambayo mpaka sasa yamepatikana 87 wakati mahitaji halisi ni mahema 550. “Hapa Tanzania hakuna mahala pa kununua mahema hivyo tunategemea kuazima, tumeaongea na Shirika la Umoja wa Mataifa la Wakimbizi (UNHCR) bado tunasubiri,” alisema. Alisema kwa sasa kinachoendelea ni tathmini ambapo timu za wathamini zimeanza kazi lakini zimeongezewa nguvu na wathamini kutoka Morogoro, Pwani na Tanga na wamezungumza na Mkuu wa Chuo cha Ardhi ambaye ameahidi kuongeza wahitimu 20 wa tathmini katika timu hiyo ili kuweza kufanya tathmini ya nyumba lakini pia pamoja na mali.

Akizungumzia wagonjwa, alisema hadi sasa katika Hospitali ya Temeke wapo 12 na wengine 15 wameongezeka jana ambao kati yao tisa wamelazwa, waliokufa ni raia 18 na maiti zote zimetambuliwa ikiwapo iliyoopolewa jana katika mto Mzinga na kati ya maiti hizo 15 zimezikwa Dar es Salaam moja Singida. Kwa upande wa misaada, Lukuvi alisema serikali imetoa Sh milioni 200, Ofisi ya Waziri Mkuu Sh milioni 200, Bakhresa Sh milioni 100, Quality Group milioni 30, Mwenyekiti wa IPP Reginald Mengi Sh milioni 25, Vodacom Sh milioni 20, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Sh milioni 20, manispaa zote tatu Ilala, Temeke na Kinondoni Sh milioni 60 na Mabohora Sh milioni 5.2.

Alisema fedha hizo zimetumika kulipia gharama za mazishi, kununulia vyakula, maji, nguo kama vile mablanketi na vyandarua, posho za wathamini, mafuta ya magari na posho za askari Polisi 100 wanaolinda eneo la kambi. Naye Meya wa Manispaa ya Temeke, Jerome Bwanausi, alisema kutokana na malalamiko ya baadhi ya waathirika kwamba misaada haiwafikii mengi ni ya uongo na kwamba timu iliyopangwa kugawa misaada hiyo inagawa kulingana na tathmini inayofanywa na idadi ya kaya. Wakati gazeti hili likiwa eneo la maafa, lilishuhudia kikosi cha askari wa JWTZ kikifukua kifusi cha nyumba zilizobomoka huku kikitoa tahadhari kwa watu kukaa mbali kutokana na kuwapo uwezekano wa mabomu ambayo hayajalipuka



(chanzo: www.habarileo.co.tz,
Imeandikwa na Maulid Ahmed na Halima Mlacha; Tarehe: 5th May 2009 @ 08:48)