Friday 15 May 2009

Ikulu yampongeza Mhe. Anne Kilango MB

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425

PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mheshimiwa Anne Kilango (MB), Jimbo la Same Mashariki

YAH: KUTUNUKIWA TUZO YA KIMATAIFA YA WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA MAREKANI KWA WANAWAKE JASIRI (SECRETARY OF STATE’S GLOBAL AWARD FOR WOMEN OF COURAGE)

Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amepokea kwa furaha kubwa habari za kutunukiwa kwako Tuzo ya Mwanamke Jasiri kwa Mwaka 2009 inayotolewa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani. Aidha anakupongeza kwa mafanikio hayo makubwa na ya kujivunia.

Kutunukiwa kwako Tuzo hiyo ni ishara ya kutambuliwa na kuthaminiwa kwa mchango wako katika mapambano dhidi ya rushwa. Aidha, ukiwa Mbunge wa Chama Cha Mapinduzi, Tuzo hii ni tunda la wazi la utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya 2005 kuhusu vita dhidi ya rushwa ambayo Chama Cha Mapinduzi na Serikali yake vimetoa fursa pana zaidi kwa wananchi, wanahabari na viongozi wakiwemo Waheshimiwa Wabunge kushiriki kwa ukamilifu zaidi.
Hongera sana.

Ikulu
Dar es Salaam
27 March, 2009


chanzo: www.tanzania.go.tz

No comments:

Post a Comment