Tuesday 20 January 2009

Simu ya Polisi Arusha

Polisi Arusha watoa namba mpya kudhibiti uhalifu

Wakazi wa Arusha wametakiwa kutumia simu namba
0767 750173,
kutoa taarifa za dharura kwa jeshi la Polisi Mkoani humo iwapo kutatokeaa tatizo lolote la uhalifu katika eneo husika.

Akiongea na vyombo vya habari ofisini kwake, Kaimu Kamanda wa Polisi,Mkoa wa Arusha, Roberti Boaz, alisema kuwa, simu hiyo ni maalum kwakutumia ujumbe wa maneno kwa gharama nafuu.

"lengo la kutoa namba hii, kurahisisha utoaji wa taarifa kwa wananchi,wengine wanapata tukio ila wanashindwa kuja polisi kwa umbali, lakinikwa kutumia simu itasaidia kushirikiana" alisema Boaz

(chanzo: Faustine's Baraza)

No comments:

Post a Comment